IGP Mangu: Lugumi ilitekeleza mkataba wake na Jeshi la Polisi

IGP Mangu: Lugumi ilitekeleza mkataba wake na Jeshi la Polisi

Mkuu wa Jeshi la Polisi – Inspekta Jenerali (IGP), Ernest Mangu amekanusha madai ya wabunge na hata taarifa zinazosambaa mitandaoni na kwenye vyombo vya habari kuhusu kampuni ya Lugumi kushindwa kufunga mashine kwenye vituo vya Polisi 108 kama mkataba wake ulivyomtaka.

Akizungumza mwishoni mwa wiki, IGP Mangu alisema anashangazwa na habari hizo na kueleza kuwa kampuni ya Lugumi ilitekeleza mradi wa kufunga mashine hizo kama ilivyokubaliana na serikali.

“Siyo kweli, watu wana ugomvi wao, lakini nakueleza wazi kwamba, tembelea vituo vyote tulivyokubaliana, utakuta mashine zipo. Inawezekana zingine hazifanyi kazi kwa sababu ya kukosekana kwa intaneti,” aliongeza mkuu huyo wa polisi.

Alipoulizwa mwenye jukumu la kufunga mtandao wa intaneti ni nani, IGP alijibu, “...ni TTCL (Kamuni ya Simu) ingawa sehemu nyingi ofisi zetu zimekatiwa huduma hiyo kwa kuwa jeshi halijalipa.”

Naomba kujua hicho unachosema kilitekelezwa ni halali? Kilifuata sheria? Ni kweli thamani yake ndiyo hiyo? Ni nini kwanza kilichotekelezwa? Hata ndege ya raisi na radar zilinunuliwa na zilikuwa zikifanya kazi.

Mangu acha kujihami. Acha wataalamu wafanye kazi yao.

Wewe ni mtuhumiwa na hivo huwezi kuwa mtoa taarifa. Wewe(ofisi yako) na Lugumi ni watuhumiwa na hatutegemei taarifa kutoka kwenu tukaimani bila kujiridhisha. Tungeelewa kama ungetuambia "Lugumi alitkeleza mkataba alioingia na Polisi bla bla............................. ambao ulitekelezwa kwa fedha zilioztoka mifukoni mwa wafanyakazi wa jeshi la polisi. Hazkuwa fedha za serikali".
 
Nahofia isije kuwa kama ya mama Kilango
Mkuu huwezi fananisha Mkuu wa mkoa na IGP. IGP ni next level rais hawezi kulala na kuamka akawatumbua watu wanaoitwa IGP, generari au Mkuu wa TISS. Hizo ni taasis nyeti kuzid hata zaid neno nyeti na maana yake
 
Hapa ndipo IGP amejipalia mkaa na asipokuwa makini hii story itamletea maneno mengi mpaka atajuta kusema hadharani, hivi Thamani ya hivyo vifaa ni bilion 34 ? Uchunguzi uliofanyika kwa kiina Thamani ya Hizo mashine haifiki hata bilion 1 , pesa nyingi ilizidishwa ikaliwa na wajanja wakagawana na sasa ndiyo inatumika kuwanunua wote wanaotumwa kulichunguza hilo sakata, Rushwa imetembea sana na baadhi ya mashine zimefungwa chapchap kwenye Vituo ili kumlinda Said mwema na hii Aibu , lakini Ukweli harisi pesa aliyopewa Lugumi haiendani na Thamani ya hizo mashine bali pesa nyingi imeliwa na wajanja wachache kisha kuleta vifaa ili kuwahadaa Watanzania.
humu ndani kuna watu wana akili sawa na watumishi hewa wanaopokea mishahara ya kazi ambazo hawajazifanya. wewe umejigeuza valuator kwanza nikuulize hizo mashine zinaitwaje ? nitajie specification wakati zinanunuliwa na pia gharama za ufundi ikiwepo na VAT kisha baada ya hapo ndo uje uropoke ! usijifanye kama wale wabunge wanaoamini kwa kuwa wao wameambiwa watunge sheria za nchi hii basi wanajifanya wanajua kila kitu wanajua mpaka thamani ya madaraja wanajua mpaka dawa zilizotumika muhimbili ! hii nchi ikiendelea hivi ...
 
Sasa wanawekaje vifaa vinavyohitaji internet kwenye vituo ambavyo havina internet?hapa ni jipu, aliyebuni mradi huo kabla ya kuhakikisha internet inapatikana ndio jipu lenyewe.
Kwa hiyo unasem Lugumi sio jipu bali aliyebuni mradi sio?
 
Mimi ni IT proffesional na sizdhani kama hizo biometric system ili zifanye kazi zinahitaji internet connection wala sio kweli Mangu anaongea mambo asiyo yajua. Only LOcal area network inahitajika kwenye hiyo system. Anajaribu kutetea uovu huyu Mangu
Huitendei haki IT yako
IT ni zaid ya hicho ulichonacho kichwani mwako
 
Hizi ni sarakasi zilizozoeleka serikali iliyopita, sijui kama serikali hii itakubariana na hili la funika kombe mwanaharamu apite ngoja tuone mwisho wa picha.
 
Mimi ni IT proffesional na sizdhani kama hizo biometric system ili zifanye kazi zinahitaji internet connection wala sio kweli Mangu anaongea mambo asiyo yajua. Only LOcal area network inahitajika kwenye hiyo system. Anajaribu kutetea uovu huyu Mangu
****
Troubleshooter I salute you!
VIFAA 108 TU, VYA BIOMETRY THAT COST 37 BILLIONS

SIO MTAALAM LAKINI DOH!?.
KAZI IPO TUIACHIE TUME.
37,000,000,000÷108=???
kila BVR 1 ILINUNULIWA KWA KIASI CHA SHS 343 MILLION.
KAZI IPO!/
 
Hao watakamatwa tu hawana ujanja labda magu aamue tu kufumba macho. Kama ni uongozi wa sheria na haki fumba na kufungua akina babu seya na kamishna kitilya wangekutana huko magereza na hao viongozi wa jeshi la polisi
 
Mnategemea magufuli ndo abadilishe nch??? huyu anaefanya maamuzi jukwaani.. Kaz mnayo
 
Hata Kama wangepeleka Asikari wote kusomea hizo mashine isingefika hizo gharama kubali ukatae kuwa pesa nyingi imepigwa kupitia huo mladi wa kifisadi.
Kwa kozi ambayo haizidi hata 45 minutes?!
 
Umebadili nyimbo toka hakuna mpaka thamani kubwa.

Umesahau kubadili chorus kuwa mikataba ya vifaa kama hivyo huhusisha mafunzo kwa watumiaji ambayo thamani yake inaweza kuwa kubwa sana kuliko kifaa.

Haya sasa kabadili chorus.

Baadhi ya nchi nyingine mafunzo kama haya ni online based trainings haiwezi kuzidi hata dola 20!!
 
Vyombo vya ulinzi havitumbuliwi hovyo hovyo,tuulize kwanini wanaogopa
 
Kwa hiyo unasem Lugumi sio jipu bali aliyebuni mradi sio?
Kama waliingia mkataba wa yeye kupeleka tu hivyo vifaa kisha akavidump huko vituoni bila kutumika basi Lugumi hatakuwa na kosa maana yeye atakuwa ametimiza sehemu ya mkataba wake lakini hao waliohusika kubuni mradi wa kipuuzi namna hiyo ndio wenye kosa na watapaswa kuwajibika kwa matumizi mabaya ya ofisi zao.

Lakini kwa sababu wana akili na wamefanya uamuzi wa kijinga namna hiyo basi kutakuwa na namna wamenufaika na mradi huo, hapo ndipo atakapoingilia Lugumi, rushwa.
 
Jamani nimeona hapa kuna watu wanajaribu kuonyesha wao ni wataalam wa IT. Mtu akishamiliki laptop akajua kucoonect modem na kupost vitu kwenye mitandao basi naye tayari anajiona ni mtaalam IT. Kuna tofauti kati ya "intranet" na "internet". Hapa watu msijitie kujua, hakuna ulazima wa internet ku centralise data zao, bali intranet inatosha.
Mkuu rudia tena kujua tofauti na mahusiano ya internet na intranet, let assume kifaa kipo Nachingwea Mtwara,na ukaingiza fingerprint pale kisha hiyo data inakuwa processed kwa identification au storage kwenye central database ambayo ipo Dar es Salaam, sasa hiyo connection ya kifaa kilichopo Nachingwea na Database iliyopo Dar es Salaam ni nini hapo?ni internet.

Japo hiyo system itakuwa ni maalum kwa network tu ya jeshi la polisi tu kwa case ya fingerprint, hakuna hapo google wala jamiiforums, hapo ndipo inapokuja maana ya intranet.
 
mkuu huo mladi ulibuniwa kwa lengo la kupiga pesa hizo mashine Thamani yake harisi ni kidogo sana.
Mmmmh funza wewe ni Mkurya? Kwenye "r" unawekaje "l" na panapohitaji "l" unawekaje "r"? Ukweli mradi wa LugumiPolisi ni wizi mtupu na hela yote hiyo imeingia mfukoni mwa familia mbili ambazo ni DUGU MOYA! Nizitaje? JIONGEZE NA WEWE!! Sasa huyu naye anaropoka hadharani? Ina maana kamati ya bunge ni waongo? MAGUFULI NJOO HUKU KUNA JIPU LIMEIVA! Anafikri bado ni wakati wa "business as usual?"
 
Baadhi ya nchi nyingine mafunzo kama haya ni online based trainings haiwezi kuzidi hata dola 20!!



Ukisoma vizuri hii mada utaona kuwa hadi hii leo sehemu nyingine zilizofungwa hizo mashine hakuna hata access ya Internet, sasa elezea watajifunzaje online hata kama ni bure.

Nnashauri saa nyingine utumie kichwa chako kufikiri japo kiduchu na si kukiwacha kama mzigo tu juu ya mabega yako.
 
Back
Top Bottom