IGP Simon Sirro, kwanini askari polisi wanatumwa field na silaha nzito wamevaa kiraia? Kwanini unatuma askari na silaha nyingi tukio dogo la kiraia?

basi ujue hawaji kwenu peke yenu.wanazurula maeneo mbali mbali yenye wajuaji zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati mwingine kama ni mapambano labda ya adui ana silaha zinasaidia maana ukivaa gwanda kijeshi tunaita "mng'ao"hivyo inakuwa rahisi kwa adui kukuona
 
Wewe hata huo u-private hustahili, maana unajibu bila hata kuelewa somo.
 
Hawatokei??
Ushawahi skia majambazi na polisi wamejibizana kwa risasinafu majambazi wakashinda?
Hao jamaa usiwachukulie poa

Sent using Jamii Forums mobile app
Ukisikia polisi wameua majambazi katika mpambano mara nyingi ni wamba polisi wamewageuka watu kwenye mchoro. Visa vya mpambano wa kweli kati ya polisi na majambazi ni vichache sana - kwa kuwa polisi huwa wanaogopa kwenda eneo la tukio

Sasa hivi si kuna polisi anasubiri kunyongwa hadi kufa kwa "kupambana na majambazi" wafanya biashara ya madini?
 
Wewe hustahili hata huo u koplo waliokupa. Yaani mwanamke aliyetoroka kambi ya Corona atajiandaa kwa silaha kupambana na polisi wakija kumchukua?

Hivi ndivyo intelijensia zenu zinavyofanya kazi? I say sijaona majipu upuou kama haya mawazo

Kwa hiyo mnaona raha kubeba silaha hata pale zisipohitajika? Unajua kwa nini Nyerere alikataa askari utembea na bastola kama nchi nyingine - hadi leo bastola sio sehemu ya vazi la kawaida la askari. Kwa nini?

Tatizo mnaangalia sinema za kina Robocop na mnataka muonekane kama wao mitaani! Upumbafu mtupu.
 
Kweli wewe mtoto eti mazingira ya kawaida Tanzania hujui Kama Ile Ni kazi professional au unataka kusema hawajui kazi yao wewe ndio unajua
Wangekuwa professional wasingeenda na nguo za kiraia na masilaha yote hayo. Hao ni show off tu wametoka kuangalia movie za Rambo nao wanataka waonekane kama Rambo mitaani. Hawana lolote!
 
Sasa hapa umejibu nini kwa mada iliyopo? Umechanganya mambo utafikiri macho yaliamka kabla ya ubongo. Yaani wewe hata kuwa askari hustahili. Mwepesi kuongea, mzito kuelewa.

Yaani wewe subiri tu uwe unapokea amri maana huna uwezo wa kuelewa.
 
Wangekuwa professional wasingeenda na nguo za kiraia na masilaha yote hayo. Hao ni show off tu wametoka kuangalia movie za Rambo nao wanataka waonekane kama Rambo mitaani. Hawana lolote!
Kwa hiyo kwa akili zako kwenda na nguo za kiraia na silaha unajua wamevunja taratibu na kanuni za jeshi la polisi Tanzania?
 
Pole Mwananchi Mwenzngu kwa upeo mdogo juu ya jambo hili.
Hicho ni kikosi cha kupambana na Ujambazi na dharula zote hivyo muda wote wanatembea wakiwa kamili kupambana ndiyo maana hata ukisikia Mtoto katupwa jalalani watakuja hivyo hivyo na hizo ndizo Laptop zao. Hiyo miwatu inaitwa Ant Robbery ni moja ya vitengo ndani ya Idara ya Upelelezi na ndiyo maana wakifika eneo la tukio wanakusanya Mpaka vielelezo na kuhoji Mashaidi. Hao ndiyo watu wa Mwanzo wanaojenga kesi au kuibomoa. Kwa ufupi ni watu wenye Nguvu za kupambambana kibunduki na kiakili na Shule yao imeelemea kwenye Upelelezi .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa ngoja nikuambie kitu cha kufanya kwa askari wasomi.

Si unasema wanaweza kupata pingamizi? Basi unaweka response team standby mahali sio mbali na tukio. Pale unaenda na ambulance na askari wawili tu, labda mmoja ndio ana silaha kama SMG. Na una radio. Kukitokea pingamizi au vurugu ndio unaita kwenye radio - response unit move in.

Ndivyo askari professional wanavyofanya kazi. Wana avoid antagonistic responses wanaposhughulika na raia.

Ila kama wewe ni askari kama hao najua hayo maneno hapo nimeshakuchanganya
 
Hivi nyie makoplo mna tatizo gani?

Hata kama hicho ndio kikosi cha kuwakamata Al-Queda sio tatizo. Tunachosema haikuwa akili kwa mtu kukitumia kwenda kumkamata mwanamke aliyetotoka kambi ya korona. Unaenda kama vile una respond tukio la ujambazi? Kwani hicho ndio kikosi pekee cha kufanya kazi za uaskari Iringa nzima? Mna ubongo wa aina gani hadi muweze kusoma jambo na kuelewa issue inayojadiliwa.

Unajua jinsi mnavyotoa pointi zenu humu ndio mentality ile ile ya kusema hili lijamaa linaitwa Maiko halafu kwenye fomu limeandika Mikaeli!
 
Nimekuwa nikijibu comment za watu kwenye hii thread ambazo ni wazi zinatoka kwa wana JF ambao ni askari. Kwa kweli tuna tatizo. Yaani ni utumbo mtupu wanaongea, hakuna lojiki wala hoja, ni mibwabwajo tu, ooh, kikosi maalum, ooh silaha sehemu ya kazi. Ni wazi tuna kazi kubwa sana ya kulibadili jeshi letu kama hawa ndio watu tunaita askari wetu.

Tatizo sasa, unakuta mtu mwenye kushindwa kufikiri kama huyu kapandishwa cheo na wanasiasa kwa sababu ya kitu cha kawaida tu kama kumkamata mwenyekiti wa chama cha upinzani kwa kuchelewa kumaliza mkutano, halafu unasikia eti sasa ndio amekuwa OCD au RPC!

Namwambia Magufuli na Sirro waziwazi - kwamba tatizo moja wapo kubwa sana kwenye jeshi letu la Polisi ni kwamba kuna maofisa walipanda vyeo kwa vigezo vya kisiasa au kufurahisha wanasiasa na sasa wengi wana vyeo na mamlaka makubwa na wanaliharibu sana jeshi la Polisi kwa kuwa na mavyoe lakini hawana busara ya kielimu wala experience ya kazi. Ndio wanaofanya maamzuzi kama haya ya Iringa

Au Kasesera ndio aliomba kikosi kilichokamilika kisilaha kifuatane nae? Hilo nalo ni tatizo - wanasiasa kuwa ndio makamanda wa polisi. Amri za operation za polisi kutolewa na wanasiasa wasio na ujuzi wa polisi.

Ujinga na upumbavu mtupu.
 
Umeambiwa kikosi cha dharula zote. Ndiyo maana mnasema polisi wanawaonea kumbe umbuumbu wenu. Ukiangalia magari ya Polisi yote yana silaha kubwa muda wote na hawaruhusiwi kutembea bila silaha. Sasa unataka wakakamate kwa kutumia fimbo? .Umeambiwa kikosi cha kupambambana na Ujambazi inamaana majambazi hawezi kujitokeza alipojificha Mgonjwa wa Corona?. Jiulize hiyo bunduki Kubwa inazuia nini Polisi kukamata.Maana hawajaitumia kumpiga Mgonjwa. Akili ndogo wewe unafikiri ujambazi unatoa taarifa kuwa leo tutapiga kwa Mgonjwa wa Corona?. Haya umejiuliza kwanini huyo mgonjwa amekimbia karantini?. Ujinga tu unakusumbua unajifanya unaujua ulinzi wa Nchi kumbe Mbumbumbu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Physiological disturbing....
Ndo maana umeleta huu uzi coz ulipata usumbufu kisaikolojia na hukutamani kuwa miongoni mwa watakaosambaratishwa na ile siraha.

Ujumbe umefika...thats the objective!
Sikiliza wewe private. Umeathirika na kuvuta ile harufu mbaya ya kwenye vituo vya polisi kwa muda mrefu.
 
Kwa hiyo hata dharura hujui maana yake tukueleweshe? Kwenda kumkamata huyu mama lilikuwa tukio la dharura katika operation za polisi?

I say nyie watu wa kuhurumiwa sana.
 
Umesahau kuna watu wamechukizwa na alichofanya huyo Mgonjwa. Au uwajui wananchi wenye hasira Kali wangefanya nini. Mwanajamiiforums mwenzangu muda mwingine uwe anaangalia na kukaa kimya. Maana umbumbumbu wako ni mkubwa hujawahi hata kuwa kupewa nafasi ya kuongoza watoto wenzako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…