IGP Sirro: Kipindi cha kampeni nilimtafuta Tundu Lissu aje kuhojiwa lakini hakuja

Kwa nini uhoji jirani wakati mwenye tukio yupo?
Nani mwenye taarifa sahihi kati ya jirani na Lisu?
Kwa hiyo hicho ni kisingizio cha kutofungua jalada? Kwa taarifa yako, zipo taratibu zinazowezesha polisi kumhoji yeyote mahali popote duniani. Ila hapa kuna mbinu na mikakati ya kutetea maagizo feki ya Magufuli kuzuia uchunguzi, ndio maana vinatolewa visingizio vya ajabu.

Kwa hiyo, kama ushahidi wa anayeshambuliwa ni wa lazima, polisi hawafungui jalada kama mlengwa kauwawa?
 

..swali lingine ni kwanini jeshi la Polisi halikumkamata TL baada ya kukaidi wito wa kwenda kutoa ushahidi?

..kwa uelewa wangu kukaidi wito wa Polisi ni kosa ambalo mhusika anaweza kushtakiwa mahakamani.
 
Huyu mjinga je angekuwa TL marehemu angemuhoji Nani ? Anajitahidi kukwepa kwa hoja za kitoto sana

Sent from my Nokia 3.2 using JamiiForums mobile app
 
Wakati tupo kwenye group la watu kutoka mataifa mbalimbali.

Mimi nikawa na jisifu kuhusu usalama wa nchi yetu kuanzia jeshi la wananchi na polisi, japo mengine sijui!

Ila jamaa kaniuliza swali moja mpaka nimetoka nduki!

Swali: Mbona mpaka sasa waliompiga lissu risasi hawa jawahi kupatikana na upelelezi wowote maana hicho kitendo sio kesi ndogo kwa nchi na mtu mwenye kutambulika serekalini “

[emoji23] mimi nimebaki kimya
 
Jibu rahisi tu mbona

Waliompiga tundu lisu risasi walijipanga kwa zaidi ya miaka 10 ndo wakafanya shambulio. Hivyo najeshi litahitaji zaidi ya miaka kumi kuja kuwabaini.
 
Waambie hakuna nchi ambayo imemaliza kila kesi, mambo ni mengi ya kufatilia
 
Swali:”mbona mpaka sasa waliompiga lissu risasi hawa jawahi kupatikana na upelelezi wowote maana hicho kitendo sio kesi ndogo kwa nchi na mtu mwenye kutambulika serekalini “

[emoji23] mimi nimebaki kimya

Muulize mbona huko kwao wanapigana risasi sisi hatuwaulizi?
 
Kwa kuonesha wewe ni Mtanzania ungejibu swali kwa swali. Yaani ungemuuliza 'kwenu hakuna mauaji ambayo mpaka leo muuaji hajapatikana?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…