IGP Sirro tafakari sana maneno ya mtu aliewaua Polisi aliposikika akisema "Nawatafuta Polisi"

IGP Sirro tafakari sana maneno ya mtu aliewaua Polisi aliposikika akisema "Nawatafuta Polisi"

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Nimesema mara nyingi sana humu JF, kwamba namna ya utendaji wa Polisi wa Tanzania ni ile ambayo inazalisha chuki na wananchi badala ya kukuza uhusiano mzuri. Watu wengi sana wana chuki na Polisi kutokana na vitendo vyao, iwe suala la rushwa, kubambikiwa kesi, matumizi ya nguvi isivyostahili, upendeleo kwa chama tawala nk.

Je umewahi kushuhudia ndugu yako, mtu wa karibu, akipigwa, akikamatwa bila kosa, akinyanyaswa na Polisi? Ulipata hisia gani dhidi ya Polisi? Polisi wametengeneza tabaka la Watanzania ambao hata kama huyu jamaa angesikika akisema kesho naenda kuua Polisi, wasingetoa taarifa kwa Polisi!

Polisi wanajisahau sana na kuwa na utendaji unaowatukuza watawala na kuwakandamiza au kuwapuuza raia, na hili linasababisha watu wengi kuwachukia Polisi. Kuna nchi ambazo raia huwaona Polisi kama rafiki lakini sio Tanzania. Polisi mngejenga uhusiano mzuri na raia, msingehitaji kuahidi zawadi kwa atakaetoa taarifa juu ya huyu mtu, watu wangejitokeza bila hata ahadi ya zawadi.

Kuna wakati hata niliuliza kwamba, hivi kuna mtu yeyote alie upande wa vyama vya upinzani ambae anawaona Polisi kama marafiki? Na nikasema, Polisi hawaoni kwamba ni tatizo kubwa kuwa na idadi kama hiyo inayowachukia?

Naamini kwa dhati kabisa tukio lililotokea la mauaji ya Polisi limetokana na hasira na chuki dhidi ya Polisi kwa mambo fulani waliyomfanyia huyu mtu (inasemekana walimdhulumu dhahabu waliyomkuta nayo) au hata ndugu yake. Ikafikia mahali huyu mtu ali "snap", akapata uenda wazimu wa ghafla (temporary insanity) na kuamua kutafuta Polisi ili awaue.

Sasa hili ni jambo Polisi hawapaswi kulichukulia upande mmoja, kwamba Polisi wenzao wameuwawa, bali wajiulize kwa makini sana kwa nini wameuwawa, na kama linaweza kujirudia. Sintashangaa kama huko nje kuna watu wenye hasira pia dhidi ya Polisi ambao wanaona huyu mtu kafanya kitendo cha ujasiri, na wao pia kwa hasira waliyonayo dhidi ya Polisi wakaona hata wao wanaweza!
 
Hawa Polisi wetu wamekuwa wakatili sana.
Na kila kitendo cha ukatili au wonevu wanachofanyiwa watu au wanachokisoma watu, kinakuza hasira na chuki dhidi ya Polisi.

Hakuna mtu anaependa kuona ndugu yake, rafiki yake, mwanachama mwenzake, akionewa na kunyanyaswa na Polisi. Watu wengi sana moyoni wanasema ningekuwa na uwezo na mimi ningewapiga risasi Polisi. Huo ndio ukweli.
 
mi nilichoshangaa jamaa alikua mmoja ila hilo mbilinge lake jeshi la polisi watu kama wote.Hivi wangekua km watano ingekuwaje?si lingetoka jeshi lote la dar?
Una unacho kifahamu mzee, mengine hacha kama yalivyo... Kama kungekuwa kuna back up ya waalifu na mmoja ndio amejionesha pekee...?

Vipi kibaka uliye muona ndani ya uzio wako wa nyumba, lakini bila kujua nje au njiana kuna wengine ambao wapo kumpa msaada kibaka mwenzao... Huku una jidanganya ni huyu huyu hakuna kibaka mwingine au majambazi wengine!?
 
Ninaamini kwa dhati kabisa, kwamba kama huyu mtuhumiwa wa mauaji ya Polisi angekuwa hapa amevaa nguo ya Chadema na sio ya CCM, IGP Siro saa hizi angekuwa anafanya sherehe na kusahau kwamba kuna Polisi wake watatu wameuwawa, na hata angekuwa anafikiria kuipeleka hiyo picha mahakamani ikatumike kama ushahidi katika kesi ya ugaidi dhidi ya Mbowe

1629912808056.png
 
mi nilichoshangaa jamaa alikua mmoja ila hilo mbilinge lake jeshi la polisi watu kama wote.Hivi wangekua km watano ingekuwaje?si lingetoka jeshi lote la dar?
Ndio maana nikasema watu wanapaswa kutafakari sana juu ya zile kauli za Polisi kwamba kulikuwa na mpambano kati ya Polisi na majambazi sita wenye silaha, na polisi wakafanikiwa kuwaua wote bila kujeruhiwa. Nani, hawa polisi wa kwetu hawa waue majambazi sita ya silaha bila hata wao kupata mchubuko? Thubutu!

Leo hii mtu mmoja anawahenyesha kundi la polisi zaidi ya saa nzima, na kufanikiwa kuua watatu, halafu wanatudanganya tumeua majambazi sita wenye silaha nzito!
 
Back
Top Bottom