IGP Sirro: Ukiwa na mtoto mhalifu halafu usitoe ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama wewe ni tatizo kwa Watanzania

IGP Sirro: Ukiwa na mtoto mhalifu halafu usitoe ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama wewe ni tatizo kwa Watanzania

Itabidi hadi trafiki wanaongoze magari na silaha za kivita kama Wataliban, ukikosea tu wanakumiminia za kutosha
 
Mbona kama Vile ametangaza vita?

ni mwendo wa kuliana timing saivi au?

au mwandishi ndio kaiwasilisha vibaya?
View attachment 1911601
Wakati nchi makini wanatumia technolojia kama jicho muhimu katika masuala ya ulinzi na usalama, jeshi letu la polisi lipo "busy" kudhiti wapinzani na kukusanya hongo kutokana makosa ya barabarani. Jeshi letu ni lazima lijiongeze ili kuendana na matakwa ya wakati.

Siro asianze kutafuta visingizio ili kuficha dhuluma ambayo ipo nyuma ya pazia kuhusu vijana wake dhidi ya Hamza. Mbona siku nyingine katika matukio kama haya huwa anaunda tume ya uchunguzi mbona katika hili yupo kimya!?

Badala ya kufikiria kuanza matumizi ya kamera maalumu ikiwa kama jicho makini na mbadala ili aweze kufuatilia kwa kificho matendo ya kihalifu, yeye anaona ni vyema kuwajaza askari wetu mitaani na pengine kuanza kuuwa watu fulani waliowakusudia kwa makusudi kwa kisingizio cha tukio la Hamza. Siro uzee ndio huo unakunyemelea, na umepitwa na wakati, ni vyema ukampisha mtu mwingine atumie 'state of art technology" ili kuimarisha masuala ya ulinzi na usalama hapa nchini.
 
Kauli hii, endapo itadababisha polisi kuingiza gia ya mauaji "Killing Spree", ICC inamhusu huyu kamanda.

Sina hakika alichomaanisha huyu kamanda wetu, lakini inaweza kuwa ni kuwatia hamasa askari waue raia bila kufuata taratibu za kisheria zinazotambulika.

Tuombe heri, labda Sirro, siku zijazo atalazimika kukemea mauaji yatlnayotarajiwa kuendeshwa kwa maagizo yake. Tuombe Uzima.
Binafsi huwa nashangaa watu wanaotajataja ICC
 
"Huwa nawaambia siku zote, usicheze na mtu wa hovyo hovyo, usimwamini kila mtu. Walipomuona huyu mtu wa hovyo hovyo Hamza anawasogelea, walijua ni Mtanzania wa kawaida, kumbe alikuwa na pistol na akafanya alichofanya."- IGP Simon Sirro katika ibada ya kuaga miili ya askari wanne

=========

IGP Sirro

Watanzania wenzengu, Kwa niaba yangu mwenyewe na kwa niaba ya Jeshi la Polisi niwape pole sana wafiwa nawapa pole sana waombolezaji hili tukio ni kweli ni kubwa lakini ndio kazi yetu sisi askari, lakini tukio kama hili linapotokea sisi Askari tuna kitu cha kujifunza, wananchi wana kitu cha kujifunza lakini pia wafiwa wana kitu cha kujifunza.

Watanzania wenzangu ukishakuwa na mtoto mhalifu, ukishakuwa na mtoto mwizi. ukishakuwa na mtoto gaidi, ukishakuwa na mtoto mwenye tabia mbayambaya, usiposhirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama, maana yake kuna namna mbili Moja kubwa anaweza akaleta madhara kwa watanzia lakini pia anaweza akapoteza uhai wake yeye mwenyewe.

Sasa huyu Hamza aliyofanya kama ndugu zake wangewajibika vizuri leo tusingekuwa hapa sasa. Lakini watanzania wenzangu waele siku zote askari polisi na vyombo vingine vya usalama vipo kwa ajili ya kulinda Watanzania na ndio maana tumeapa kufa kwetu kwa risasi tumeapa kwa Amiri jeshi Mkuu hatuoni tabu juu ya hilo lakini watanzania wajue kuwa na sisis tuna familia zetu.

Kwa hiyo kuna kitu cha kujifunza kwamba ukishakuwa kwenye familia yako kuna mhalifu ujue wewe ni tatizo kwa Watanzania tulitegemea Watanzania wazae mtoto aje kuwa Waziri aje kuwa IGP aje kuwa Mwalimu, lakini ukizaa mtoto akawa mwizi akawa kaluwanja ni tatizo kwa Watanzania.

Lakini kwa wafiwa kuna kitu cha kujifunza, Askari wetu hawa hawakuwa gaidi, hawakuwa wezi, hawakuwa majambazi wamekufa wakiwa wanatetea watanzania hivyo kifo chao ni kwa heshima ya Watanzania wamekufa wakiwa wanalinda Watanzania kwa hiyo tusapate huzuni sana tuwaombee, tusipate huzuni sana kwa sababu walikuwa wanalinda Watanzania.

Lakini kwa Poliai ofsa na sisi viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama kuna kitu cha kujifunza kwa askari wetu hawa kufa kwa risasi kwa kupigwa na risasi kichwani. Siku zote huwa wanawaambia usicheze na mtu wa ovyo ovyo, usimwamini kila mtu hii yote ni kwa sababu ya imani, walipomuona huyu mtu wa ovyo ovyo Hamza anakuja walijua ni Mtanzania wa kawaida anakuja lakini kumbe alikuwa na pisto na akafanya alichofanya.

Lakini tumejifunza ukizubaa usilaumu jeshi, ukizubaa usilaumu serikali, askari mna mafunzo ya kutosha ni Hightime, tuna challange, tuna changamoto si kila mtu ni rafiki lakini niseme kwamba kama jeshi tumepoteza vijana wadogo sana sis ambao tunakaribia kustaafu tunaamini hawa ndio wangeendesha jeshi lakini kwa sababu ni sehemu ya maisha yetu askari ninaamini wale mnaobaki mnajifunza sasa si kila mtu anapenda Askari polisi, si kila mtu anapenda vyombo vya dola.

Wakati mwingine tunaambiwa tunatumia nguvu kubwa sana sio au hatutendi haki sio? Lakini yanapotekea hapa hatusikii mtu anasema habari ya haki ya polisi maana yake nini msiwe na Double Standard. Kazi hii ni ngumu sana mtu akiiona hivi anajua ni kitu rahisirahisi tu lakini kudeal na mhalifu sio jambo dogo!.

Sisi tuwaombee sana waliotangulia na sisi tuko nyuma yao tunafata. Na ninyi mliofiwa si kwamba mmefiwa peke yenu na sisi ni ssehemu ya tatizo pia kwa sababu vijana wetu wametangulia na kijana wetu wa SGA najua kazi yetu ni moja ndio maana huwa nasema sisis ambao tuvaa buti kazi yetu ni moja. Mhalifu anapotuoona hajui huyu ni wa kampuni binafsi anajua kazi yetu ni moja ni ya kulinda maani, na ndio maana huwa nasema acheni kubaguana sijui huyu ni wa kampuni ya ulinzi hapana kazi yetu ni moja kwa hiyo tuheshimiane.

Lakini wafiwa niseme tutajitahidi kwamba vijana wetu hawa wanapata haki zao, kama wana familia zao tutajitahidi kulingana ya kanuni zetu kuhakikisha wanapata haki zao niwashukuru sana asanteni sana.
View attachment 1911814
Askali wangejuaje kama hamza wa hovyo
 
Awaase watu wake waache dhulumati sio wao pekee ndo wenye shida ya pesa
 
Dogo angekuwa gaidi ile Eicher isingeachwa vile


Inategemea!

Mbona magaidi wa Nigeria wanatekaga wanafunzi wa Shule mabinti mara nyingi?

Kwanini wasiteke watu wowote bila kujali jinsia wala umri?!
 
Msomali amefanya jambo la kikatili sana !

Kuua watu wetu ? ! [emoji24][emoji24][emoji24]

Kwanini??? [emoji24][emoji24][emoji24]
 
Ukiwa na mapolisi wezi, vibaka, madhulumati na usiwachukulie hatua basi jeshi lote huenekana wote ni wezi na majambazi kama ilivyotokea
 
Huyu baba huyu! Kama alivyofanya kwa Mbowe. Anamalizia kabisa hukumu. Kakosa ethics kabisaa, ndio maana jeshi linakwenda bora liende.
Kinachoogopesha ni kuona raia wamepoteza imani na jeshi la polisi huku polisi wakionesha kujiamini kulikopoteza mvuto! Inaogopesha zaidi pale Hamza anapoonekana shujaa huku polisi wakionekana waonevu dhidi ya raia. Nadhani tuliandika humu mara kadhaa idara hii ijitathmini ili uwepo ushiririkiano wa dhati usio na mashaka baina yake na raia kwa ajili ya ustawi wa nchi na watu wake.
 
Back
Top Bottom