IGP Wambura: Polisi hatuhusiki na matukio ya utekaji watu

IGP Wambura: Polisi hatuhusiki na matukio ya utekaji watu

Mungu wa Mbinguni muumba wa mbingu na ardhi. Ukawajaze hekima na neema wanangu. Wasijekufikiria wala kuwaza wala kushawishika kuwa maaskari polisi, katika Jina na damu ya Yesu kristo Amen.
 
Wazee wa kazi naona wanajichanganya wanakosea kujibu kama wapo rumande..
 
Unamkoseaje adabu mtu asiye na adabu?, jeshi la polisi limefeli pakubwa sana, huwezi kumshikiria mtu kinyumee na sheria mwezi mzima ,ndugu wametoa taarifa polisi nakupewa RB, polisi wanaanza kutafuta mtu mwisho wa siku wanakuja kukiri wanamshikiria, hivi wana adabu hawa ambao wanadai wana adabu?
 
Hakuna haja ya kuongeza neno, Taarifa yake hii hapa.
---
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura amesema jeshi hilo halihusiki na matukio yanayodaiwa kuwa ni ya utekaji, kwani jukumu lake la msingi na la kikatiba ni kuhakikisha linalinda usalama wa raia na mali zao.

IGP Wambura amesema hayo leo Jumatatu Julai 15, 2024 akiwa mkoani Simiyu katika ziara ya kuzungumza na maofisa, wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali.

Hivi karibuni, Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni akiwa bungeni alitaja vyanzo vya matukio ya utekaji na kupotea kwa watu kuwa ni wivu wa mapenzi, ushirikina, kugombania ardhi, urithi, kujiteka, visasi na utapeli.

Mwaka huu, Mwananchi limeripoti matukio ya watu zaidi ya 10 kutoweka na wengine baadaye kuelezwa kuwapo mikononi mwa Polisi.

Jana Julai 14, 2024 Polisi Mkoa wa Tanga lilikiri kumshikilia kada wa Chadema, Kombo Mbwana (29) kwa tuhuma za matumizi mabaya ya mtandao aliyetoweka siku 29 zilizopita.

TOA MAONI YAKO
Hapohapo wanae mwananchi waliomteka karibu mwezi mzima...afya ya akili inahusika hapo
 
Mungu atakulaani , utakufa mikononi mwa shetani
Baada ya kustaafu Omari Mahita, Aliyekuwa IGP wa Tanzania alikamatwa na kushitakiwa kwa kesi ya Aibu ya kumbaka House girl wake mwenyewe kisha kumjaza mimba, na kukataa matunzo ya mtoto

Aliburuzwa kwenye Mahakama ya Kinondoni mchana kweupe pee bila huruma yoyote, chama chake cha CCM kiliminya kimyaa kama vile hakimjui!
 
Hakuna haja ya kuongeza neno, Taarifa yake hii hapa.
---
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura amesema jeshi hilo halihusiki na matukio yanayodaiwa kuwa ni ya utekaji, kwani jukumu lake la msingi na la kikatiba ni kuhakikisha linalinda usalama wa raia na mali zao.

IGP Wambura amesema hayo leo Jumatatu Julai 15, 2024 akiwa mkoani Simiyu katika ziara ya kuzungumza na maofisa, wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali.

Hivi karibuni, Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni akiwa bungeni alitaja vyanzo vya matukio ya utekaji na kupotea kwa watu kuwa ni wivu wa mapenzi, ushirikina, kugombania ardhi, urithi, kujiteka, visasi na utapeli.

Mwaka huu, Mwananchi limeripoti matukio ya watu zaidi ya 10 kutoweka na wengine baadaye kuelezwa kuwapo mikononi mwa Polisi.

Jana Julai 14, 2024 Polisi Mkoa wa Tanga lilikiri kumshikilia kada wa Chadema, Kombo Mbwana (29) kwa tuhuma za matumizi mabaya ya mtandao aliyetoweka siku 29 zilizopita.

TOA MAONI YAKO
Hawa jamaa wanaweza hata kuanza kupanga matukio kujiteka kujustify kauli ya Boss wao
 
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Camillius Wambura kwa mara ya kwanza amezungumzia taarifa zilizopo ambazo zimekuwa zikihusisha jeshi la Polisi kuhusika katika matukio ya utekezaji wa watu mbalimbali hapa nchini, akibainisha kuwa Jeshi hilo halihusiki na matukio hayo.

IGP Wambura ametoa kauli hiyo leo, wakati akizungumza na waandishi wa Habari, mara baada ya kuweka jiwe la Msingi jengo la Mkuu wa Polisi Bariadi Mkoani humo pamoja na kuzungumza na Askari wa Jeshi hilo katika kituo kikuu cha Polisi Bariadi.

Wambura amebainisha kuwa Jeshi hilo haliwezi kuhusika na matukio hayo, ambapo ameeleza katika baadhi ya matukio wamebaini kuwa watu wamekuwa wakijiteka kisha kutoa taarifa za uongo kuwa wametekwa.

“ Haya matukio ya watu kutekwa au kupotea yamezungumzwa sana na viongozi mbalimbali akiwemo Waziri wa Mambo ya ndani, niseme hapa Jeshi la polisi halihusiki hata kidogo na matukio haya, na wale wote ambao wamekuwa wakitoa tuhuma hizo dhidi yetu wanatukosea heshima na adabu,” amesema IGP Wambura…..

“ Kuna matukio Mwanza, Mbeya na sehemu nyingine watu wamepotea wametekwa, na baada ya kufuatilia tumegundua wamejiteka na wanatoa taarifa kuwa wametekwa, jambo hili siyo jema na tutawachukulia hatua wale wote wanaofanya vitendo hivyo,” ameongeza IGP Wabura.

Mkuu huyo wa Polisi nchini, aliwataka wananchi kuacha tabia za ajabu za kujiteka kisha kulisingizia jeshi la polisi kuhusika katika matukio hayo na badala yake wabadilike kwa kuacha kutoa taarifa za uongo.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Jeshi la Polisi, aliwahakikishia wananchi usalama wa kutosha wakati wa zoezi la uchaguzi Mkuu na uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu.

Chanzo: Global TV
Kenya wao wana chombo maalumu cha kuwasimamia na kuchunguza utendaji wa jeshi lao la police.
 
Back
Top Bottom