IGP Wambura: Polisi hatuhusiki na matukio ya utekaji watu

IGP Wambura: Polisi hatuhusiki na matukio ya utekaji watu

Kama polisi hawahusiki, wanajeshi hawahusiki basi itakua wale wavaa suti nyeusi...


Cc: Mahondaw
 
Hakuna haja ya kuongeza neno, Taarifa yake hii hapa.
---
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura amesema jeshi hilo halihusiki na matukio yanayodaiwa kuwa ni ya utekaji, kwani jukumu lake la msingi na la kikatiba ni kuhakikisha linalinda usalama wa raia na mali zao.

IGP Wambura amesema hayo leo Jumatatu Julai 15, 2024 akiwa mkoani Simiyu katika ziara ya kuzungumza na maofisa, wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali.

Hivi karibuni, Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni akiwa bungeni alitaja vyanzo vya matukio ya utekaji na kupotea kwa watu kuwa ni wivu wa mapenzi, ushirikina, kugombania ardhi, urithi, kujiteka, visasi na utapeli.

Mwaka huu, Mwananchi limeripoti matukio ya watu zaidi ya 10 kutoweka na wengine baadaye kuelezwa kuwapo mikononi mwa Polisi.

Jana Julai 14, 2024 Polisi Mkoa wa Tanga lilikiri kumshikilia kada wa Chadema, Kombo Mbwana (29) kwa tuhuma za matumizi mabaya ya mtandao aliyetoweka siku 29 zilizopita.

TOA MAONI YAKO

PIA SOMA

- Kuelekea 2025 - Sativa: Nilitekwa na Jeshi la Polisi wakiwa na lengo la kuniua, hata nikipotea kesho Jeshi la Polisi litakuwa limehusika

- Mahakama yaamuru Polisi kuwatafuta viongozi wa BAVICHA (kina Deusdedith Soka) waliopotea

- Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana



"We were forced to form a Paramilitary Wing of uMkhonto we Sizwe within the ANC because the Government of Whites Minorities of South Africa was terrorising us by using the State Security Forces."

Oliver Reginald Tambo, former President of African National Congress (ANC) from 1967 to 1993.
 
Back
Top Bottom