Ijue formula rahisi ya kujua jambo kama ni baya au zuri

LIKUD

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
18,037
Reaction score
33,681
Ukitaka kujua kama jambo ni baya au zuri andika herufi U kabla ya jina la jambo hilo. Jina utakalo lipata baada ya kuweka herufi U ndilo litakalo kupa majibu kama jambo hilo ni zuri ama sio zuri.

Natoa mifano kadhaa.

1. Dini.

Ukiweka herufi U kabla ya neno Dini unapata neno UDINI.

Maana yake ni kwamba DINI sio jambo zuri. Na kweli dini sio nzuri. Hakuna kitu kimeleta matatizo mazito duniani kama dini.

2. Kabila.

Ukiweka herufi U kabla ya neno kabila unapata UKABILA.

UKABILA sio mzuri . KWA hiyo kabila sio kitu kizuri. Makabila hayafai kuwepo.


3. Tajiri= UTAJIRI.

UTAJIRI ni mzuri KWA hiyo kuwa tajiri ni kitu kizuri ( hakikisha unakuwa tajiri)

4. Tanzania = Utanzania.

Hakuna kitu kizuri KWA mtanzania kama Utanzania. Mtu akifanya jambo baya utasikia " jamani huu sio Utanzania"


Tafsiri yake ni kwamba Tanzania ni nchi nzuri. That's why I love Tanzania.

Dini yako tupa kule. Kabila lako tupa kule. Kanda unayo toka tupa kule.

GET DOWN WITH UTANZANIA.

EMBRACE UTANZANIA


Ongeza mifano YAKO mingine
 
U
Ujinja wa kutuletea formula zisizo kua na scientific proofs hatutaki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…