Mateo Kovasic
JF-Expert Member
- Aug 9, 2022
- 420
- 334
(13) Kujaza kwa niaba ya Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa, nafasi za uongozi zitakazokuwa wazi, isipokuwa ya Mwenyekiti wa CCM na Makamu wa Mwenyekiti wa CCM.
(14) Kuunda Kamati au Tume kwa shughuli maalum bila kuathiri majukumu ya Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa.
(15) Kupokea na kujadili taarifa za Tume na Kamati Maalum za CCM, Kamati ya Wabunge wa CCM, na Kamati ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wa CCM.
(16) Kuweka kiwango cha kiingilio katika CCM, ada za Uanachama na michango maalum.
(17) Kusimamisha kwa maslahi ya CCM utumiaji wa kifungu chochote cha Katiba ya CCM au kuruhusu kifungu kutumika kabla ya kuingizwa ndani ya Katiba. Uamuzi huo sharti uungwe mkono na theluthi mbili ya Wajumbe kutoka Tanzania Bara na theluthi mbili za Wajumbe kutoka Zanzibar. Hata hivyo Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa itafikisha uamuzi wake mbele ya Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa kwa uamuzi wa mwisho.
(18) Kushughulikia uhusiano kati ya CCM na Jumuiya mbalimbali za wananchi na kuziorodhesha Jumuiya za CCM.
(19) Kutengeneza na kurekebisha Muundo wa CCM katika maeneo na nyanja mbalimbali kwa kadri itakavyoonekana inafaa.
(20) Kumsimamisha Mwenyekiti wa CCM au Makamu Mwenyekiti wa CCM iwapo mwenendo na utendaji wake wa kazi vinamwondolea sifa za uongozi. Hata hivyo Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa itafikisha mapendekezo yake mbele ya Mkutano Mkuu wa CCM wa Taifa kwa uamuzi wa mwisho.
(21) Kumwachisha au kumfukuza Uongozi kiongozi yeyote ambaye uteuzi wake wa mwisho ulifanywa na Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa.
(22) Kuunda Kamati ya Usalama na Maadili.
(23) Kuidhinisha Kanuni za Kamati za Wabunge wote wa CCM, Wawakilishi wote wa CCM, Madiwani wote wa CCM; Katiba/Kanuni za Jumuiya za CCM na kuidhinisha marekebisho ya Katiba/ Kanuni hizo.
(24) Halmashauri Kuu ya Taifa yaweza kukasimu madaraka yake kwa Kamati Kuu kuhusu utekelezaji wa kazi zake kwa kadri itakavyoona inafaa.
Maandishi makubwa kama tuna matatizo ya macho