Ijue Jamhuri ya Watu wa SOGODO, Kinondoni

Ijue Jamhuri ya Watu wa SOGODO, Kinondoni

kaka ndo tulikozaliwa na kukulia huko kuanzia kino mkwajuni a.k.a kino moscow vuka barabara pita kuzungukia vijana shuka na mwananyamala. had uibukie mwananyamala shule urud kino bwawan ya chini nnyooaha had hadi kwa mzee kikwete kwa kaka yake pale kino

uvuke biafra ukatize kama unaenda ada estate ila kula chocho nyuma ya biafra sec ibukia kino shamba uje hadi nyuma ya open university pita juu kwa juu tokea shule ya muslim vuka ingia soko la tx pita kanisa katoliki tokezea baa ya Chez Temba a.k.a shetembaa ilipozaliwa ngwasuma band ya kina mkweji a.k.a Jose (Hozee) mara enz hizo ndo wanafanyia mazoez pale Mara rud kati ibukia lang'ata kino makaburi njoo american chips vuka pita kati uibukie kino mahakamani /shule bwanan pale vuka njoo kanisa la waluteri nyoosha urudi sogodo

ndo mitaa ya kujidai enzi hizo
Dah...hizo docho ulizozitaja umenikumbusha mbali

Ova
 
Nakumbuka mtaa wa first in ulikuwa unaitwa mahakama ya simu..njia panda ya kwenda manzese,..
Mwizi,mkabaji aliyesumbua mbaya kipande hicho alikuwa smbdy kidile...
Jamaa alipora kaba sana watu...
Wazee walimngoaga
Jamaa alikuwa anapiga sana mpira sema mhuni

Ova
 
Pawa wakati analinda Bills mwanae alikua DJ pale.

Sasa kumkuta Pawa na mwanae wako kwenye sofa kila mmoja anashona goma lake lilikua jambo la kawaida tu.

Hata hivyo stori nyingi kuhusu maeneo zinakuzwa.

Kwa mimi mkazi wa maeneo hayo nakuambia kwamba eneo hatari lilikua Chaukucha na kundi hatari lililoundwa na watoto lilikua Majani Unit. Hawa Panya Road walizunguka maeneo ya huko Mwenge na Sayansi sisi tukajiorganize kuwasubiri pale Uwanja wa Sparta.

Aliyewatonya wasije aliwaokoa.
Aisee!
 
Kwa wakongwe kama Mshana Jr, mitaa ya Dizonga anainyaka vyema, kwani kakaa huko hadi pale alipohahamishwa na jini lililo mnasa vibao akitaka kulinanilihiiii kwenye nyumba ya wageni, akaona isiwe taabu, akahamia Masaki.

Sogodo ni eneo linalopatikana Mwananyamala Bwawani, nyuma ya mahakama ya Kinondoni, kanisa la KKKT Kinondoni, linasambaa hadi jirani na kwa Pawa, baba yake Jaki, alikuwa baunsa wa Billicanas Club Zama zile za kale.

Sogodo Empire, ilikuwa na watu wa hatari, watu wa Shari, wagomvi, watemi, waliojikataa, ambao wako tayari kwa lolote.

Watu wa jamhuri hiii walikuwa ni tishio kiasi kwamba walikuwa na mahakama yao, polisi wao na mamlaka yao wenyewe.

Ukiiba unapelekwa kwa Pawa, Pawa anakusikiliza mhalifu na washitaka wako, baada ya hapo anatoa hukumu.

Hukumu ikitekelezwa hamna kupelekana Polisi wala Nini. Kesi imeisha hiyo.

Sogodo Empire waliishi hivyo kwa miaka mingi.
Kinondoni huko kulikojaa mashoga, mapunga au kinondoni ipi?
 
Raia hawafai mzee
Zamani kulikuwa na bonding mmja anaitwa Paul siza,wakati huo vijanq tunasafirisafiri ukirudi unangaa cheni shingoni,chini raba kali
Yeye siza alikuwa analinda langata pale
Ukienda chooni anakuja nyuma yako
Anakugusa Bega ukiegeuka kitasa anakupa
[emoji23][emoji23][emoji23]
Sema uzuri wengine ule alwatan ulikuwepo
Kuna siku nko mtungi nko chooni kuchek nyuma siza..ahh nkamwambia mjomba vepe hata mm tena[emoji23][emoji23][emoji23]akacheka sana
Siza alipoona kukaba hakumfai akaingia robbery
Kna siku walienda iba mahali raia waliwagumia
Walipiga hadi kuuaaa
Ila naye alishaonywaaa

Siku zote nasema usicheze na raia au kuwachukulia mafala siku wakikuamulia hutoki

Ova
Paul Siza, Duh! Kinondoni B. Biafra. Namkumbuka sana huyu Big brother. Kumbe ndivyo alivyofariki? Kama namuona vile mitaa ya Lang'ata akiwa Bouncer. Ndio tatizo la maisha ya uhalifu, yanaanza kimasihara, baadae unaanza kufanya kweli. Na mwisho wake sio mzuri.
 
Kuna mwizi mmoja,mkabaji alikuwaga maarufu sana mitaa ya mwananyamala kisiwani alikuwa anakaa bonding kule unapotekea tsndale
Alikuwa anaitwa mashkurumbwe
Alimkabaga jamaa yetu mmja alikuwa ofisa,tukasema ngoja mabaharia tukirudi tutamfanyia operation maalum
Tukamuandalia team ya wahuni wa Moscow,kinondoni wagumu,na wahuni wa msisiri...tukamwinda sana,sasa kuna siku tukamgumia gheto, ebwana si tikamkuta ananyonyoa kunguru anataka kumfanyia mafekeche ampike amle[emoji23][emoji23][emoji23]
Tukabaki hoiii...ila kipondo alikula

Ova
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Paul Siza, Duh! Kinondoni B. Biafra. Namkumbuka sana huyu Big brother. Kumbe ndivyo alivyofariki? Kama namuona vile mitaa ya Lang'ata akiwa Bouncer. Ndio tatizo la maisha ya uhalifu, yanaanza kimasihara, baadae unaanza kufanya kweli. Na mwisho wake sio mzuri.
Yah kweli kabisa....alijitakiaga mwenyewe

Ila alishaonywa

Ova
 
Tulioishi mitaa ya kuanzia kwa mbonde,suka,mbezi shule,mbezi kibanda cha mkaa,temboni,kibamba hospitali, kibamba kwa mangi, kibamba ccm,gogoni, kiluvya kwa komba Hivi ilikua ni Dar au tulikua tunaishi nje ya mji enzi zile za miaka ya 95 kuja mpk 2000. Maana gari tulikua tunapanda zinazotoka Msata zinaishia kariakoo.Haahaaaaaa
 
Yah kweli kabisa....alijitakiaga mwenyewe

Ila alishaonywa

Ova
Nilimfahamu sana enzi zile. Alikuwa anaishi maeneo ya Kinondoni B, karibia na Care Boys. Tabia yake ya kuvizia walevi chooni mitaa ya Lang'ata Disco yalikuwa yanajulikana sana mitaani Kinondoni.

Baadae nikaondoka Dar na sikuwahi kujua yaliyotoke. Taarifa za kifo chake nilizipata miaka kadhaa baadae, lakini sikujua alikufa vipi, mpaka ulivyoelezea hapo juu. Asante sana mkuu [emoji120][emoji120]
 
Tulioishi mitaa ya kuanzia kwa mbonde,suka,mbezi shule,mbezi kibanda cha mkaa,temboni,kibamba hospitali, kibamba kwa mangi, kibamba ccm,gogoni, kiluvya kwa komba Hivi ilikua ni Dar au tulikua tunaishi nje ya mji enzi zile za miaka ya 95 kuja mpk 2000. Maana gari tulikua tunapanda zinazotoka Msata zinaishia kariakoo.Haahaaaaaa
Nyie mlikuwa mnaishi BARA
 
Kwa wakongwe kama Mshana Jr, mitaa ya Dizonga anainyaka vyema, kwani kakaa huko hadi pale alipohahamishwa na jini lililo mnasa vibao akitaka kulinanilihiiii kwenye nyumba ya wageni, akaona isiwe taabu, akahamia Masaki.

Sogodo ni eneo linalopatikana Mwananyamala Bwawani, nyuma ya mahakama ya Kinondoni, kanisa la KKKT Kinondoni, linasambaa hadi jirani na kwa Pawa, baba yake Jaki, alikuwa baunsa wa Billicanas Club Zama zile za kale.

Sogodo Empire, ilikuwa na watu wa hatari, watu wa Shari, wagomvi, watemi, waliojikataa, ambao wako tayari kwa lolote.

Watu wa jamhuri hiii walikuwa ni tishio kiasi kwamba walikuwa na mahakama yao, polisi wao na mamlaka yao wenyewe.

Ukiiba unapelekwa kwa Pawa, Pawa anakusikiliza mhalifu na washitaka wako, baada ya hapo anatoa hukumu.

Hukumu ikitekelezwa hamna kupelekana Polisi wala Nini. Kesi imeisha hiyo.

Sogodo Empire waliishi hivyo kwa miaka mingi.
Kwa sasa kinondi tunaita "nyumba za uridhi" vijana hawataki kuhama wala kufanya kazi wanasubira madingii wadanje wauze nyumba.
 
Pawa wakati analinda Bills mwanae alikua DJ pale.

Sasa kumkuta Pawa na mwanae wako kwenye sofa kila mmoja anashona goma lake lilikua jambo la kawaida tu.

Hata hivyo stori nyingi kuhusu maeneo zinakuzwa.

Kwa mimi mkazi wa maeneo hayo nakuambia kwamba eneo hatari lilikua Chaukucha na kundi hatari lililoundwa na watoto lilikua Majani Unit. Hawa Panya Road walizunguka maeneo ya huko Mwenge na Sayansi sisi tukajiorganize kuwasubiri pale Uwanja wa Sparta.

Aliyewatonya wasije aliwaokoa.
Hilo eneo Sogodo nalifahamu vyema sana, pale uswahili hasa ila hapakuwahi kuwa tishio.
Ila na ushenzi kishenzi, eneo lolile ni la wazi, pia ni bonde na dampo watu wakalivamia wakavifuta vyote.
Ila sasa hivi nyumba zinazidi kudidimia kila mwaka. Nyingine madirisha yameshafika usawa wa ardhi.
 
Hilo eneo Sogodo nalifahamu vyema sana, pale uswahili hasa ila hapakuwahi kuwa tishio.
Ila na ushenzi kishenzi, eneo lolile ni la wazi, pia ni bonde na dampo watu wakalivamia wakavifuta vyote.
Ila sasa hivi nyumba zinazidi kudidimia kila mwaka. Nyingine madirisha yameshafika usawa wa ardhi.
Ndio pale yule Diwani SONGORO MNYONGE wa CCM kajimilikisha [bwawani-mwananyamala]
 
Back
Top Bottom