severinembena
JF-Expert Member
- Jun 2, 2018
- 2,435
- 2,402
Nyota sio uchawi...ni sayansi. Kama ulisoma physics o level ipo pia shule ya msingi ipo elimu ya nyota (unajimu)Tusioamini mambo ya uchawi, unatushaurije mkuru?!!
Wote mtakua makuliNa kama ukipata mpenzi ambaye mnanyota nae sawa hii itakuwaje? Mfano wote ni Punda au wote ni Samaki
Utamaduni wa kaa huwa ni wa kupuuzwa na shauku kubwa ya ng'e na kaa huwa muaminifu zaidi, wivu wa ng'e ni wa hasira, ustahamilivu wa kaa humfanya ng'e kujihisi yupo kwenye mikono salama. Kaa hupenda nguvu alizonazo Ng'e na Ng'e hujihisi yupo kileleni kwa mapenzi ya kaa muda wote, zote ni nyota zenye hisia zinazohitajika kwa mwingine pamoja hawa wanaweza kujenga maisha mazuri katika mapenzi yao. Mahusiano haya ni mazuri na humo ndani utakuta ni upendo,furaha na amani na kila jambo linalotokea huwazidishia mapenziMkuu mimi ni kaa alafu mpenzi wangu ni nge je kuna future
Namaanisha akiwa na watu hao au siku zinazotawala nyota hizo anaweza kufanikisha hayo kirahisi sanaHivi unamaanisha nini unaposema mtu nyota yake ni Punda ila nyota ya kujifurahisha ni Simba, nyota ya kumsaidia kipesa ni ng'ombe, nyota inayomsaidia kikazi ni Mbuzi, nyota inayomsaidia kiubunifu ni Simba?
Hapana ninaposema nyota hii ni ya kike namaanisha negative na nikisema kiume namaanisha positive hizi ni kama kwamba nyota ambayo ni kiume mara nyingi huwa ni nyota ya mabavu na kiburi na uchangamfu wakati kike ni nyota pole yenye subira na fair play, hakuna fair play kwa nyota ambazo ni chanyaHivi unamaanisha nini unaposema walozaliwa April 20 hadi may 20 hali yao ni ya kikekike? Inamaana mwanangu Wa kiume alozaliwa muda huo ana hali ya kikekike?
Ndio nikiwa namaana kuwa hiyo nyota ni rafiki kwake pale tu kwenye point iliyotajwa hakuna pengineKuna sehemu mfano unasema Nyota za watu ambao haelewani nao ni nyota ya ng'ombe halafu hapohapo unasema nyota inayomsaidia kikazi ni nyota ya ng'ombe?
Haya ni majina ya mwenyezi Mungu katika lugha ya Kiarabu mfano J ni Jabbar yaani mwenyezi Mungu mwenye Nguvu, hivyo kama ni mtu wa kiroho anaweza kuwa akimsifu Mungu wake kwa sifa hiyo na kufanikisha analohitajiNa unaposema herufi yake ya jumamosi ni Z inatumikaje?