Ikikuuma Kajinyonge, ila ukweli ni kwamba 85% Moses Phiri anaenda Yanga SC Dirisha Dogo au Msimu Mpya ujao

Ikikuuma Kajinyonge, ila ukweli ni kwamba 85% Moses Phiri anaenda Yanga SC Dirisha Dogo au Msimu Mpya ujao

Screenshot_20231027-082303.jpg
 
GENTAMYCINE nimeandika Threads za kutosha hapa Kuuonya Uongozi wa Simba SC juu ya Kocha Mkuu Roberto Oliveira anachomfanyia Mshambuliaji wangu Bora ndani ya Simba SC Moses Phiri ila nikapuuzwa.

Mpaka nikaja hapa JamiiForums Kumuonya Kiongozi Mmoja Mwandamizi wa Simba SC kuwa Yeye ndiyo Kisababishi Kikuu cha Mshambuliaji HATARI Moses Phiri kutopangwa Kimakusudi na Kocha Mkuu Roberto Oliveira.

GENTAMYCINE ukiniuliza ni Mshambuliaji gani ambaye kwa Simba SC hii ya sasa ana Namba yake ya Kudumu na anatakiwa Kuanza kutokana na Uwezo mkubwa ( hasa katika Ufungaji ) haraka bila ya Kuchelewa nitamtaja Mshambuliaji Mzambia Moses Phiri.

Muda si mrefu GENTAMYCINE nimetoka kumsikia Mmoja wa Waandamizi ndani ya Yanga SC ( mwenye Kuheshimika ) kote kote ( Uraiani na Bungeni ) akiwa amekuja katika Ofisi za Kampuni Moja Mikocheni akimthibitishia niliyekuwa na Miadi nae Saa 2 hii Asubuhi kuwa mpaka sasa wana 85% za Kumsajili Mshambuliaji Moses Phiri na kwamba hata Kocha Mkuu wa Yanga SC Miguel Gamondi 'Master' anamuhitaji akiamini kuwa kwa Mpira mwingi wa Pacome Zouzoua, Aziz Ki, Max Zengeli huku nyuma yao akiwepo Doctor Khalid Aucho basi Mshambuliaji Moses Phiri atafunga Magoli mengi hadi mengine Kuyakinai na kuwapa akina Onana, Boko na Baleke nao wawe nayo.

Moses Phiri kwa Upuuzi ulioko Simba SC na kwa Chuki Kubwa ya huyo Kiongozi ndani ya Simba SC na kwa Unafiki mkubwa anaokufanyia Kocha Mkuu Roberto Oliveira Mimi GENTAMYCINE nimebariki kwa Moyo Mmoja na Mkunjufu Wewe kwenda / Kusajili Yanga SC Mkataba wako ukiisha na nimedokezwa kuwa unaisha au Wiki hii au Mwezi huu kama sijakosea.

Nikiwaambia Mimi ni Nabii msibishe.
Ikiwezekana aje Yanga, anakaribishwa
 
Nitakuja mwanangu, hizi tabu za kujitakia sitaki, we phiri anaozea benchi linacheza li JOHN BOKO kweli. Timu ifungwe mie niumie si kuumizana kwa makusudi huku. 😂 Alipo Atoto nami nipo.
Woyoooooo nakupenda tena na tena💚💛💚💛💚💛
 
Kama Kuna wakati viongozi na kocha wa Simba walinikera, basi ni pale walivyomtendea HAMIS TAMBWE na kisha baadae jamaa akatimkia YANGA. Yaani walimwacha top scorer kwa sababu za kijinga, na mimi nilifurahi alivyokuwa akitunyoosha alipoenda Yanga ambako nako aliibuka top scorer.

Jambo hili linaenda kujirudia kwa MOSES PHIRI. Namtakia kila la heri kokote kule atakakoenda (hata kama haitakuwa Yanga). Na ikikupendeza Mwenyezi Mungu nakuomba umsaidie ili aje kuinyoosha Simba, maana wewe ni Mungu usiyependa uonevu na dharau.

Hata akina SHABAAN CHILUNDA watafute pa kwenda kulinda vipaji vyao maana wachawi akina Bocco wana kila dalili ya kuongezewa mikataba mingine.
Na wewe ikibidi kasajiliwe Tanga,Kwa I huko yanga wanacheza wote? Gift Fred anacheza? Nkane na Ngushi wanacheza? Toeni ushamba ktk football
 
GENTAMYCINE nimeandika Threads za kutosha hapa Kuuonya Uongozi wa Simba SC juu ya Kocha Mkuu Roberto Oliveira anachomfanyia Mshambuliaji wangu Bora ndani ya Simba SC Moses Phiri ila nikapuuzwa.

Mpaka nikaja hapa JamiiForums Kumuonya Kiongozi Mmoja Mwandamizi wa Simba SC kuwa Yeye ndiyo Kisababishi Kikuu cha Mshambuliaji HATARI Moses Phiri kutopangwa Kimakusudi na Kocha Mkuu Roberto Oliveira.

GENTAMYCINE ukiniuliza ni Mshambuliaji gani ambaye kwa Simba SC hii ya sasa ana Namba yake ya Kudumu na anatakiwa Kuanza kutokana na Uwezo mkubwa ( hasa katika Ufungaji ) haraka bila ya Kuchelewa nitamtaja Mshambuliaji Mzambia Moses Phiri.

Muda si mrefu GENTAMYCINE nimetoka kumsikia Mmoja wa Waandamizi ndani ya Yanga SC ( mwenye Kuheshimika ) kote kote ( Uraiani na Bungeni ) akiwa amekuja katika Ofisi za Kampuni Moja Mikocheni akimthibitishia niliyekuwa na Miadi nae Saa 2 hii Asubuhi kuwa mpaka sasa wana 85% za Kumsajili Mshambuliaji Moses Phiri na kwamba hata Kocha Mkuu wa Yanga SC Miguel Gamondi 'Master' anamuhitaji akiamini kuwa kwa Mpira mwingi wa Pacome Zouzoua, Aziz Ki, Max Zengeli huku nyuma yao akiwepo Doctor Khalid Aucho basi Mshambuliaji Moses Phiri atafunga Magoli mengi hadi mengine Kuyakinai na kuwapa akina Onana, Boko na Baleke nao wawe nayo.

Moses Phiri kwa Upuuzi ulioko Simba SC na kwa Chuki Kubwa ya huyo Kiongozi ndani ya Simba SC na kwa Unafiki mkubwa anaokufanyia Kocha Mkuu Roberto Oliveira Mimi GENTAMYCINE nimebariki kwa Moyo Mmoja na Mkunjufu Wewe kwenda / Kusajili Yanga SC Mkataba wako ukiisha na nimedokezwa kuwa unaisha au Wiki hii au Mwezi huu kama sijakosea.

Nikiwaambia Mimi ni Nabii msibishe.
hivi kwanini wanamchukia phiri?
 
Back
Top Bottom