Uchaguzi 2020 Ikiwa Dkt. Magufuli atafanikiwa kushinda, aachane na agenda za kuminya Upinzani

Uchaguzi 2020 Ikiwa Dkt. Magufuli atafanikiwa kushinda, aachane na agenda za kuminya Upinzani

Chief Ortambo Ikumenye

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2017
Posts
247
Reaction score
503
Mimi kama mwana CCM moja ya matamanio yangu ni kuona CCM ikiendelea kushika dola ya Tanzania.

Ila kati ya jambo ninalotamani litokee kwenye muhula wa pili wa Rais Magufuli endapo akifanikiwa kushinda, ni kuacha kabisa kuwachokonoa wapinzani.

Wapinzani waachwe na kuishi maisha yao na ku play part yao kama kusudi la kuwepo kwa mfumo wa vyama vingi.

Binafsi pamoja na kuegemea upande wa CCM ila sijafurahishwa kabisa na baadhi ya matukio ndani ya miaka mitano iliyopita ya kukandamiza upinzani.

Tukio la kupigwa risasi Lisu, hila za kununua viongozi wa upinzani, vitabaki kama doa lisilofutika kwa utawala wa kwanza wa Magufuli. Ni moja wapo ya mbinu chafu za kisiasa karne hii ya utandawazi.

Kwa hizi wiki chache za ujio wa Lissu na mapokeo yake, ni kama vile upinzani umekuwa na nguvu maradufu pamoja na hila zote hizo chafu.

Najua wanadamu hukosea, Magufuli rais wangu kweli hapo ni mahali alikosea, lakini ana uwezo wa kuparekebisha endapo akichaguliwa tena.

Awaache upinzani waishi maisha yao kama maana ya kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi nchini.
 
Sikilza wewe mwana CCM. Magufuli hashindi uraisi mwaka huu. Raisi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania 2020 - 2025 ni Tundu Antipas Lissu!

Kama wewe unasoma Biblia nenda kasome hadithi ya Mfalme Saul na Mfalme Daudi alafu Njoo hapa niambie kama umeona tofauti yeyote kati ya yanayoendelea baina ya Magufuli na Tundu Lissu!
 
Wapinzani ni watu, ni ndugu zako, ni rafiki zako na ni Watanzania wenzako. Ukitaka kuua upinzani ni kwamba uko tayari kuwaua Watanzania wenzako na kwa hilo jitihada zake zimeonekana, Watanzania wengi wameumizwa.

Awali Watanzania walikuwa watu wa amani na wakarimu na walijulikana hivyo duniani kote hadi mwaka 2015. Maisha yao yalipoanza kuwa hatarini kwa sababu ya kiongozi moja aliyetaka kuua upinzania, matokeo ndiyo haya.

Watanzania kwa umoja wao wamekataa hizo hila za kuwagawa na mwezi Oktoba nina hakika wataonesha kwa vitendo kwamba ukatili na uonevu si jadi yetu. Watakataa dhulma na ukandamizi kwa mgongo wa hapa kazi tu.

Watarudi kwa ile misingi aliyoianzisha baba wa taifa, Mwalimu Kambarage Julius Nyerere ya uhuru na kazi, uhuru na haki, uhuru na usawa. Madikteta uchwara na malimbukeni watapewa haki yao kwa kurudishwa wanakostahili.
 
Kuminya demokrasia ya uhuru wa vyombo vya habari, freedom of expression, uhuru wa mikutano ya siasa imefanya watu kuwa na hamu/shauku na usongo mkubwa wa kukusanyika na kusikia yale yalivyokuwa yananong'onwa je ni kweli?
 
Mkuu ni kuwa na washauri wabovu.

Unafikiri angewaacha waendelee na harakati zao leo hii wangeongea nini?

Sasa kinachotokea wanayo mengi ya kuongea waliyofungwa kwa miaka mitano. Ukijumlisha na walivyokuwa missed.

Hatari tupu!
 
Sikilza wewe mwana CCM. Magufuli hashindi uraisi mwaka huu. Raisi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania 2020 - 2025 ni Tundu Antipas Lissu!

Kama wewe unasoma Biblia nenda kasome hadithi ya Mfalme Saul na Mfalme Daudi alafu Njoo hapa niambie kama umeona tofauti yeyote kati ya yanayoendelea baina ya Magufuli na Tundu Lissu!
kushinda Urais sio kama kuokota nazi ndugu! , endeleeni kuota ,huu uchaguzi kwenye Urais msijidanganye , pambanieni ubunge tu!.. maan si vibaya kuishi kwa matumaini !.
 
Shida sio Magufuli, ila ni wshauri wake. Hivi leo una weza kuzuia redio na tv kweli? Zisitangaze habari fulani? Su wao Ccm ndio wana jidanganya hizo habari hazionekani?? Mambo ya utopolo kabisa
watu wanaongezeka kwenye mikutano ya Lissu kutaka kujua ni vitu gani hivyo ambavyo serikali haitaki tuvisikie kwenye vyombo vya habari.
 
Tukio la kupigwa risasi Lissu, hila za kununua viongozi wa upinzani, vitabaki kama doa lisilofutika kwa utawala wa kwanza wa Magufuli. Ni moja wapo ya mbinu chafu za kisiasa karne hii ya utandawazi.


Jr[emoji769]
 
Shida sio Magufuli, ila ni wshauri wake. Hivi leo una weza kuzuia redio na tv kweli? Zisitangaze habari fulani? Su wao Ccm ndio wana jidanganya hizo habari hazionekani?? Mambo ya utopolo kabisa

..huwezi kuwatupia lawama wasaidizi.

..kama unamfuatilia kwa umakini Magufuli wakati akiwa Waziri ungeona viashiria kwamba akipata mamlaka makubwa atakuwa na tabia hizi tunazozishuhudia sasa hivi.

..Raisi wa Tanzania ana mamlaka makubwa ya Kikatiba, wasaidizi basically wanampeleke Raisi kule anakotaka kuelekea.

..Kama ni mtu MKATILI, basi wasaidizi watamuwezesha awe mkatili kwelikweli. Kama ni mtu wa HAKI wasaidizi watamuwezesha awe mtenda haki wa kweli.

..Lingine linalomharibu ni chama chake kuwa na WABUNGE wengi kiasi kwamba hawahitaji kushirikiana na wabunge wa vyama vingine.

..Na la mwisho ni kwamba yeye ndiye MWENYEKITI wa chama, kwa hiyo yuko juu ya kila mtu.
 
Kwanza jomba wewe sio mwana CCM nina ushahidi.

Pili nikwambie tu Magufuli hakatai upinzani nyingi hamumuelewi akili zenu zikoje..anachotaka upinzani uwe wa kizalendo ,heshima demokrasia kiheshimiana na zaidi ya yote kunadi Sera kuwashawishi wananchi wawape kura...
Maendeleo yakwao sio ya kwetu mana kwetu maendeleo hatujayaona

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
Kama kuna mtu Magufuli na CCM wanapaswa kumlaani ni yule aliyetoa wazo la kumpiga risasi Lissu. Huyo ndo mwanaCCM Mpumbavu kuliko wote japokuwa wakati anatoa wazo lake la kipumbavu aliungwa mkono.
 
Back
Top Bottom