Ikiwa Kanisa lina mlinzi ambaye ni mwanadamu iweje Watu waombe Ulinzi kwa mungu aliyeshindwa kulinda nyumba yake?

Ikiwa Kanisa lina mlinzi ambaye ni mwanadamu iweje Watu waombe Ulinzi kwa mungu aliyeshindwa kulinda nyumba yake?

Lzm kanisa lilindwe Tena na kampuni pendwa ya g4s security solution au Garda warda

Una taka mashetanj waje wanye na kujisadia kanisani na kutupa matakataka Yao

Kimara korogwe wapo walinzi na camera za CCTV iko kila Kona

Na bado kanisa linajaribiwa mno

Ni muhimu kumlindia mungu nyumba yake
Periods

Basi hata huko anakoishi huyo mungu wenu hakuna usalama.
Kama mwanadamu anaweza kulinda nyumba ya mungu wake hiyo inatoa picha kuwa huyo mungu ni dhaifu
 
We aliekwambia Mungu anahitaji jengo nan.. unajua maana ya kanisa...

Imeandikwa.. wakutanapo watu wawili au watatu wakayanena na kufundishana niliyowaagiza kuyafanya na kuomba pamoja kwa kulitaja jina langu basi mimi nipo katikati yao..

Kanisa sio jengo hata mkikaaa chini ya mti mkasali hilo ni kanisa.. binadam ndo mmeamua kujenga majengo na kuweka mali ndan mnaweka walinzi sababu mna hofu ya mali zenu.. vilivyopo ndan ya kanisa sio mali ya Mungu ni zenu nyie

Mungu alipompa binadam Maarifa ya kuitawala dunia maana yake alimpa
Uwezo wa kutambua mema na mabaya..
Sasa ni swala La binadam Kuamua akengeuke ama awe safi..

Unachosema ni sawa na mwalimu amfundishe mwanafunzi na kumpa maarifa kisha siku ya mtihan mwalimu aamue kumsaidia mwanafunzi kufanya mtihan ili Asifeli

Hujui ulichoandika.
Nenda kamfuatilie Daudi na Suleiman Mungu aliwaambia nini kuhusu nyumba yake ambayo unasema Mungu hana nyumba
 
Chungeni kauli zenu zisije kuwaponza siku moja.
 
Mkuu nenda ka google kitu kinaitwa,"TERROR MANAGEMENT THEORY" najua wewe sio mvivu wa kusoma, utapata majibu yote ya maswali yako ukiielewa hiyo nadharia ya mtu aliyewahi kujibu swali lako tuletee thread ingine kwa kiswahili ili walio wengi waelewe ni ombi lakini
Kwa hii comment
Uzi ufungwe
 
Kwema Wakuu!

Moja ya mambo yaliyozidi kunipa mashaka kwenye suala la dini ni pamoja na suala la ulinzi na usalama.

Ukienda Kanisani sio ajabu ukakuta Milango. Na kama utaenda siku ambayo sio ya ibada sio ajabu ukakuta Milango imefungwa na kufuli kabisa.
Kama hiyo haitoshi, Makanisa makubwa huwekwa Walinzi wa kulinda Kanisa na mali zilizomo Kanisani.

Sijui ni lini swali hili lilizuka akilini mwangu. Na sijui kwa nini lilizuka.
Ikiwa Mungu wa majeshi, kwake kuna ulinzi na usalama kwa nini Watu waweke Walinzi kwenye nyumba za miungu yao wakati mungu anauwezo wa kulinda nyumba yake mwenyewe?

Je mwanadamu anauwezo wa kulinda nyumba ya mungu wake ili vitu vya Mungu wake visiibiwe na mwanadamu mwenzake?

Nafahamu Mungu ni Mkuu, Muweza wa yote. Lakini hana nyumba duniani na Mungu hana makazi kwa sababu yeye sio kiumbe.

Ijumaa Kareem
Kwa kuwekewa ulinzi kanisani ina maana moja kubwa sana.
Pamekuwa sehemu ya kukutanikia wahalifu wasiotaka kubadilika, yaani wauaji, wazinzi, majambazi, malaya, waongo, walozi na wadhambi wengine kwa minajili ya kufanya money loundry kwa kumsingizia Mungu ambaye alisema tutoe tuwape maskini. Sasa wananunua vitu vya thamani na kuvificha humo wakiamini wamemnunulia Mungu ambaye ni mmiliki wa vyote.

Neno langu halikuja nitakavyo bali nimevuviwa.

Mwenye akili na afahamu
 
Hii mada umeanzisha ili tuu uendelee kupata popularity au ni kweli hujui the concept behind your qns?



You have typically based on material things. Na juu ya mwamba huu nitajenga kanisa langu. Umeelewqje hapo? Kanisa is not all about majengo na materials inside it. It's spiritual. Ulinzi wa Mungu ni wa kiroho. Hizo Mali za kushikika mtazilinda wenyewe
Kama mungu analinda kiroho na si kimwili. Huoni anafeli?

Embu assume hapo wanapolinda watu wawe wanavamia mara kwa mara au chukulia zile nchi ambazo waasi wanavamia na kuua watu kanisani.

Tunasikiliza vipi hilo meno huku tukijua maisha yetu yapo hatarini na mungu huyo yeye kazi yake kulinda kiroho?

Embu fikiria tena na wewe?
 
Uko sahihi kusema MUNGU hahitaji nyumba, yeye ni Roho, kwenye agano jipya yeye hukaa ndani yetu. Mwili ni hekalu lake.

Kuhusu ujenzi wa Nyumba za ibada ni kurahisisha kutaniko la waumini! Na ulinzi unatakiwa kimwili na kiroho, hata nyumbani kwako huwezi kuacha mlango wazi.

Kiranga anazidi kujipatia wafuasi!!
 
Kwema Wakuu!

Moja ya mambo yaliyozidi kunipa mashaka kwenye suala la dini ni pamoja na suala la ulinzi na usalama.

Ukienda Kanisani sio ajabu ukakuta Milango. Na kama utaenda siku ambayo sio ya ibada sio ajabu ukakuta Milango imefungwa na kufuli kabisa.
Kama hiyo haitoshi, Makanisa makubwa huwekwa Walinzi wa kulinda Kanisa na mali zilizomo Kanisani.

Sijui ni lini swali hili lilizuka akilini mwangu. Na sijui kwa nini lilizuka.
Ikiwa Mungu wa majeshi, kwake kuna ulinzi na usalama kwa nini Watu waweke Walinzi kwenye nyumba za miungu yao wakati mungu anauwezo wa kulinda nyumba yake mwenyewe?

Je mwanadamu anauwezo wa kulinda nyumba ya mungu wake ili vitu vya Mungu wake visiibiwe na mwanadamu mwenzake?

Nafahamu Mungu ni Mkuu, Muweza wa yote. Lakini hana nyumba duniani na Mungu hana makazi kwa sababu yeye sio kiumbe.

Ijumaa Kareem
Ndugu, Kanisa ni watu wa Mungu ambao bado wanaishi duniani. Watakapoenda mbinguni kukaa na Mungu huko ndo hawatahitaji walinzi lakini duniani bado shetani ana ufalme wake na anaweza kufanya madhara kwa watu wa Mungu akipewa nafasi.

Waefeso 4:27 "wala msimpe Ibilisi nafasi."
Kama watu wataacha mali za kanisa bila ulinzi wowote huku wakijua wako duniani ambamo kuna wezi, majambazi, waporaji n.k. huko ni kumpa Ibilisi nafasi.

Ukumbuke Mungu ni Mfalme, huwezi kumwacha akufanyie vitu ambavyo viko katika uwezo wako kuvifanya. Hata hivyo bado atakulinda na kukulindia mali zako kama alivyoahidi kwa namna ambayo bila msaada wake usingeweza kulinda.

Zaburi 127:1 "Bwana asipoijenga nyumba Waijengao wafanya kazi bure. Bwana asipoulinda mji Yeye aulindaye akesha bure."
Kwa neno hili maana yake sio vibaya kuweka walinzi, lakini lazima Mungu apewe nafasi yake na watu watambue yuko Mungu anayelinda kwa namna yake isiyoonekana kwa macho ya kibinadamu. Kama shetani angeruhusiwa au angepata nafasi ya kumdhuru mtu wa Mungu yanaweza kutokea kama yaliyomtokea Ayubu.

Ayubu1:9-10 "Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure? Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi.

Kwenye hayo maandiko shetani anamwambia Mungu kuwa ni kwa sababu ya ulinzi wake ndo maana Ayubu anamcha Mungu, la sivyo asingemcha. Kama ukisoma zaidi utaona Mungu alimruhusu shetani kumshambulia Ayubu kwa kuondoa ulinzi wake na kilichotokea nadhani wengi tunakifahamu.

Hivyo Mungu analinda watu wake lakini sio katika namna ambayo inaonekana kwa macho ya kibinadamu.
 
Back
Top Bottom