Ikiwa tarehe 23 August ni mapumziko, je karani atazifikia kaya zote kwa siku hiyo?

Ikiwa tarehe 23 August ni mapumziko, je karani atazifikia kaya zote kwa siku hiyo?

Lanlady

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2019
Posts
1,836
Reaction score
6,303
Kwa mtazamo wangu nadhani maamuzi mengine yanahitaji fikra yakinifu na si msukumo wa wadau.
Ikiwa wametangaza siku ya sensa kuwa siku ya mapumziko, na kwa nijuavyo si rahisi karani kuzifikia kaya zote kwa siku moja.

Labda kama mapumziko hayo yangekuwa ya wiki nzima. Ama sivyo, watumishi wangepewa siku moja maalum ya kupumzika kwa kuwasiliana na karani au mwenyekiti wa eneo lake kwa siku ambayo karani atafika kwenye kaya yake.

Maana lengo kuu ni kupata taarifa sahihi kutoka kwa wahusika. Sasa hili la siku moja ya mapumziko lina tija kweli?
Screenshot_20220818-120245_1.jpg
 
Hilo zoezi la sensa litaendelea kwa siku sita kulingana na nilivyosikia mwanzo, na kila siku hapo karani wa sensa atakuwa na majukumu tofauti, kuna kujua hesabu ya watu waliolala kwenye kaya husika, kujua idadi na wazee, vijana, wanawake, watoto, na wanaume, n.k

Naona kama wamelirefusha hilo zoezi makusudi ili angalau makarani wa sensa wawe busy, ili watakapokuja kulipwa, ionekane kweli walikuwa kazini.

Otherwise hilo zoezi naona lingeweza kuchukua hata siku moja likamilike, hii siku moja ya mapumziko kwangu ni kama siku ya kusherehekea kuanza kwa sensa Tanzania.
 
Ana siku 6 za kufanya kazi
Maanake ni kwamba hiyo siku karani atahesabu kaya kadhaa, kisha ataendelea kwa siku inayofuata. Je, mapumziko yataendelea kwa kaya amabazo hazikufikiwa???

Kwenye hili, ilikuwa rahisi zaidi kwa mwenyekiti au mtendaji wa mtaa/kijiji kwa kushirikiana na karani, kumtaarifu mhusika awepo nyumbani kwa siku husika. Uzuri ni kwamba wenyeviti wanawajua watu wao.

Sasa tija ya mapumziko ya siku moja ipo kweli? Karani atatembelea kaya zote kwa siku hiyo? Kwani 2012, ilikuwaje? Watu walipumzika?

Washauri wa rais wamsaidie kitaalam zaidi na si kwa mhemko! Kwa kifupi hayo mapumziko hayana tija!
 
Hilo zoezi la sensa litaendelea kwa siku sita kulingana na nilivyosikia mwanzo, na kila siku hapo karani wa sensa atakuwa na majukumu tofauti, kuna kujua hesabu ya watu waliolala kwenye kaya husika, kujua idadi na wazee, vijana, wanawake, watoto, na wanaume, n.k

Naona kama wamelirefusha hilo zoezi makusudi ili angalau makarani wa sensa wawe busy, ili watakapokuja kulipwa, ionekane kweli walikuwa kazini.

Otherwise hilo zoezi naona lingeweza kuchukua hata siku moja likamilike, hii siku moja ya mapumziko kwangu ni kama siku ya kusherehekea kuanza kwa sensa Tanzania.
Hata 2012 ilichukua siku 6 maximum.
Ila kuhesabu knategemea na eneo pamoja na idadi ya kaya.

Kumbuka kwa mfano nyumba moja ya kupanga inaweza kuwa na kaya hata 10, na kila taarifa zinajitegemea.
Kwahiyo sio rahisi kuzunguka eneo lote kwa siku moja au mbili.

Angalizo: watu watapumzika kwa siku hiyo, endapo karani hatawafikia, siku zile zinazofuata wataendelea na majukum yao.
 
Maanake ni kwamba hiyo siku karani atahesabu kaya kadhaa, kisha ataendelea kwa siku inayofuata. Je, mapumziko yataendelea kwa kaya amabazo hazikufikiwa???

Kwenye hili, ilikuwa rahisi zaidi kwa mwenyekiti au mtendaji wa mtaa/kijiji kwa kushirikiana na karani, kumtaarifu mhusika awepo nyumbani kwa siku husika. Uzuri ni kwamba wenyeviti wanawajua watu wao.

Sasa tija ya mapumziko ya siku moja ipo kweli? Karani atatembelea kaya zote kwa siku hiyo? Kwani 2012, ilikuwaje? Watu walipumzika?

Washauri wa rais wamsaidie kitaalam zaidi na si kwa mhemko! Kwa kifupi hayo mapumziko hayana tija!
Elewa basi na wewe siyo kukaza mfupa wa kichwa...

Umeambiwa tarehe 23 ndiyo mapumziko wewe unatuchanganyia habari za atakayehesabiwa tarehe 24...29

Ngoja nikupe mifano kadhaa hapa

Msimu wa sabasaba unaanzia tarehe mosi julai lakini mapumziko ni tarehe 7 julai (siku moja tu) mbona huulizi? Kadhalika nane8

Msimu wa maulid unakuwa ndani ya mwezi mzima (mfunguo sita wanaita) lakini serikali inatoa siku moja tu ya mapumziko kuadhimisha kitaifa mbona hukuwahi kuuliza?

Na mazoezi mengine mengi tu ya kitaifa!
 
...
Kwa mtazamo wangu nadhani maamuzi mengine yanahitaji fikra yakinifu na si msumumo wa wadau. Ikiwa wametangaza siku ya sensa kuwa siku ya mapumziko, na kwa nijuavyo si rahisi karani kuzifikia kaya zote kwa siku moja.

Labda kama mapumziko hayo yangekuwa ya wiki nzima. Ama sivyo, watumishi wangepewa siku moja maalum ya kupumzika kwa kuwasiliana na karani au mwenyekiti wa eneo lake kwa siku ambayo karani atafika kwenye kaya yake.

Maana lengo kuu ni kupata taarifa sahihi kutoka kwa wahusika. Sasa hili la siku moja ya mapumziko lina tija kweli?
View attachment 2327308
... zoezi linatakiwa lifanyike na kukamilika siku hiyo hiyo kama uchaguzi mkuu na ndio maana tarehe ni moja tu 23/8/2022; vingenvyo wangeweka interval labda kuanzia 23 hadi 31/8/2022; hawakufanya hivyo. Wao ni wataalamu wanajua wenyewe.
 
  • Thanks
Reactions: Cyn
Kwa mtazamo wangu nadhani maamuzi mengine yanahitaji fikra yakinifu na si msumumo wa wadau. Ikiwa wametangaza siku ya sensa kuwa siku ya mapumziko, na kwa nijuavyo si rahisi karani kuzifikia kaya zote kwa siku moja.

Labda kama mapumziko hayo yangekuwa ya wiki nzima. Ama sivyo, watumishi wangepewa siku moja maalum ya kupumzika kwa kuwasiliana na karani au mwenyekiti wa eneo lake kwa siku ambayo karani atafika kwenye kaya yake.

Maana lengo kuu ni kupata taarifa sahihi kutoka kwa wahusika. Sasa hili la siku moja ya mapumziko lina tija kweli?
View attachment 2327308
Itakuwa ni siku ya kuandaa majawabu sahihi na kuyaacha nyumbani ili hata makarani wakija kwa kuchelewa watayakuta. Usijipe stress za bureeeeee!
 
Hilo zoezi la sensa litaendelea kwa siku sita kulingana na nilivyosikia mwanzo, na kila siku hapo karani wa sensa atakuwa na majukumu tofauti, kuna kujua hesabu ya watu waliolala kwenye kaya husika, kujua idadi na wazee, vijana, wanawake, watoto, na wanaume, n.k

Naona kama wamelirefusha hilo zoezi makusudi ili angalau makarani wa sensa wawe busy, ili watakapokuja kulipwa, ionekane kweli walikuwa kazini.

Otherwise hilo zoezi naona lingeweza kuchukua hata siku moja likamilike, hii siku moja ya mapumziko kwangu ni kama siku ya kusherehekea kuanza kwa sensa Tanzania.
Ni kazi ngumu sana

Siku moja haitoshi kumaliza kupita kaya 150.
 
Kwa mtazamo wangu nadhani maamuzi mengine yanahitaji fikra yakinifu na si msumumo wa wadau. Ikiwa wametangaza siku ya sensa kuwa siku ya mapumziko, na kwa nijuavyo si rahisi karani kuzifikia kaya zote kwa siku moja.

Labda kama mapumziko hayo yangekuwa ya wiki nzima. Ama sivyo, watumishi wangepewa siku moja maalum ya kupumzika kwa kuwasiliana na karani au mwenyekiti wa eneo lake kwa siku ambayo karani atafika kwenye kaya yake.

Maana lengo kuu ni kupata taarifa sahihi kutoka kwa wahusika. Sasa hili la siku moja ya mapumziko lina tija kweli?
View attachment 2327308
Maza anataka watu wale bia j3
 
Sasa logic ya mapumziko iko wapi ikiwa kwa siku nyingine mhusika wa kaya hatakuwepo?

Hivi great thinkers wa nchi hii ndio kusema wote wameshatangulia mbele za haki???,🤔
Elewa basi na wewe siyo kukaza mfupa wa kichwa...

Umeambiwa tarehe 23 ndiyo mapumziko wewe unatuchanganyia habari za atakayehesabiwa tarehe 24...29

Ngoja nikupe mifano kadhaa hapa

Msimu wa sabasaba unaanzia tarehe mosi julai lakini mapumziko ni tarehe 7 julai (siku moja tu) mbona huulizi? Kadhalika nane8

Msimu wa maulid unakuwa ndani ya mwezi mzima (mfunguo sita wanaita) lakini serikali inatoa siku moja tu ya mapumziko kuadhimisha kitaifa mbona hukuwahi kuuliza?

Na mazoezi mengine mengi tu ya kitaifa!
 
Back
Top Bottom