Ikiwa tarehe 23 August ni mapumziko, je karani atazifikia kaya zote kwa siku hiyo?

Ikiwa tarehe 23 August ni mapumziko, je karani atazifikia kaya zote kwa siku hiyo?

Maanake ni kwamba hiyo siku karani atahesabu kaya kadhaa, kisha ataendelea kwa siku inayofuata. Je, mapumziko yataendelea kwa kaya amabazo hazikufikiwa???

Kwenye hili, ilikuwa rahisi zaidi kwa mwenyekiti au mtendaji wa mtaa/kijiji kwa kushirikiana na karani, kumtaarifu mhusika awepo nyumbani kwa siku husika. Uzuri ni kwamba wenyeviti wanawajua watu wao.

Sasa tija ya mapumziko ya siku moja ipo kweli? Karani atatembelea kaya zote kwa siku hiyo? Kwani 2012, ilikuwaje? Watu walipumzika?

Washauri wa rais wamsaidie kitaalam zaidi na si kwa mhemko! Kwa kifupi hayo mapumziko hayana tija!
Tija ipo sana, labda kwako wewe usiyejua, mapumziko yamelenga kwa wananchi wala sio makalani.
 
SERIKALI YETU NI SIKIVU, ISITAKE KUIGOMBANISHA NA WANANCHI.
Uamuzi umefanywa bila kifikiri kwa sababu viongozi wetu wanaendeshwa na wananchi. Sensa haiwezi kifanyika kwa siku moja itachukua wiki moja, sasa hayo mapumziko siku ya kwanza ni kwa ajili ya nini? Swali hili hata waziri mkuu hawezi kujibu.
Sensa huwa ni siku 1 duniani kote hata china yenye watu zaid ya 1bln, ila kukamilisha takwimu hata mwaka unaweza kuisha.
 
Nchi ya watu wavivu,mmepewa mpumzike siku 1 mnataka wiki.
Jesus
 
...

... zoezi linatakiwa lifanyike na kukamilika siku hiyo hiyo kama uchaguzi mkuu na ndio maana tarehe ni moja tu 23/8/2022; vingenvyo wangeweka interval labda kuanzia 23 hadi 31/8/2022; hawakufanya hivyo. Wao ni wataalamu wanajua wenyewe.
Mie siwezi hacha shuguli zangu ati kisa sensa, siku iyo japo nitakuwa mapumziko lkn nitaenda site hata kumwagilizia tu matofali, sitakaa kuwasubili na iwapo watakuja usiku sitafungua geti.


Overrr
 
Watanzania tunapenda sana kupumzika kila kitu mapumziko mpaka kuhesabiana mapumziko.


Sasa mpaka kuhesabiana tunahitaji public holiday.

Na kwakushindwa kuzalisha kwetu, tunaumizana kwa tozo.
 
Haishangazi kuona wenye makampuni kuajiri watendaji wakuu wahindi au wakenya wawaburuze wabongo. TZ tumejaa akili za kiuvivu na kutegea kila mahali.
Sioni tija ya hayo Maamuzi kwasababu zoezi sio la siku moja.
 
Wanapewa power bank then vishkwambi havihitaji network mkuu
 
Aliyelengwa kwa mapumziko ni nani? Watu wote wanafanya kazi, je ni mfanyakazi yupi?

1. Mfanyakazi serkalini na mashirika ya umma?
2. Je ni anayafanyakazi za biashara au kujiajiri?
3. Je mfanyakazi zq ndani?
4. Ni mfanyakazi za shamba?
Mimi kwa maoni yangu hii siku ya mapumziko haina maana kwa kuwa inalenga wenye ajira rasmi za kuajiriwa hususan serkalini lkn walioajiriwa hususan sekta zizizo rasmi haitawahusu au wao hawakuangaliwa bora isipowepo kabisa.

Nayaona maamuzi ya serkali yamejaa MIHEMUKO. Cha muhimu PUNGUZENI TOZO ambazo zinaongeza mzigo wa maisha. Sasa benki hatutaweka tena wala kwenye simu, tumerudi tena kufuata hela yako Morogoro kwa bus ni afadhali kuliko kukumbana na MAKATO labda mje tena ukisafiri ULIPE KODI.


Uzi hauhusiani lkn message sent



Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
 
Sensa huwa ni siku 1 duniani kote hata china yenye watu zaid ya 1bln, ila kukamilisha takwimu hata mwaka unaweza kuisha.
Usitufananishe sisi na nchi ambazo sensa huanzia siku unapozaliwa unaingizwa kwenye takwimu na hivyohivyo unapofariki cheti cha kifo hukutoa.
 
Mbona maswali hawajatupatia? Unaandaa majibu kwa maswali ya kujitungia au? Wasubiri kupokea madudu badala ya majibu sahihi. Mie nisisafiri kwa shughuli zangu kisa sensa? Acheni hizo!
Acha taarifa kukuhusu ikiwemo jina lako urmri, shughuli uzifanyazo, kipato na kadhalika kwa mdada wako wa kazi au hata mchepuko! Usitafute visingizio vya kutoshiriki sensa.
 
Acha taarifa kukuhusu ikiwemo jina lako urmri, shughuli uzifanyazo, kipato na kadhalika kwa mdada wako wa kazi au hata mchepuko! Usitafute visingizio vya kutoshiriki sensa.
Weweee! Yaani mdada wa kazi nimuachie taarifa zangu za kipato! Naona unataka kunichonganisha na mke wangu.
 
Pole sana.
Inaelekea huna uzoefu na hii kazi.
Na si watu wote utawakuta kwa siku na muda husika. Kurudi kwa mara nyingine hakuepukiki.

Yaani kwamba kwenye mtaa/ kijiji watu wote waache kwenda kutafuta riziki wakimsubiri msenseshaji/karani?
Labda kama ni quarters za watumishi wa umma na huyo karani aanzie hapo siku hiyo.

2012 tulihesabu watu na tulipata taarifa za wahusika kupitia watu wengine katika familia kwa ambao hawakuwepo. Na sio ndani ya siku moja.

Kuna mtu atakuwa safarini, huko aendako hakulala huko, maanake ni kwamba taarifa ataziacha kule anakopaswa kuhesabiwa.

Kuna kaya unaweza kukuta msiba au sherehe, karani itabidi uende wakati mwingine ili kupata taarifa.
Na ndio maana ya siku kuwa zaidi ya moja.
This country doesn't have enough great thinkers.

Na utakuja kusikia hoja hii ikipewa uzito subiri tu great thinkers wazinduke toka usingizini.

Umeenda mbali sana ndugu.

Hapa tulikuwa tunazungumzia kuqeka mapumziko siku moja.

Angalau utawapata watumishi ambao watakuwa mapumziko na hata wafanyabiashara wakisikia ni mapumziko wenye kujali watapumzika kusubiri kuhesabiwa, watanzania wengi ni waelewa sana.

Adha waise hayo uliyoyasema nayajua vizuri sana, sizungumzii changamoto atakazokutaka nazo huko kama misiba nk.
 
Pole sana.
Inaelekea huna uzoefu na hii kazi.
Na si watu wote utawakuta kwa siku na muda husika. Kurudi kwa mara nyingine hakuepukiki.

Yaani kwamba kwenye mtaa/ kijiji watu wote waache kwenda kutafuta riziki wakimsubiri msenseshaji/karani?
Labda kama ni quarters za watumishi wa umma na huyo karani aanzie hapo siku hiyo.

2012 tulihesabu watu na tulipata taarifa za wahusika kupitia watu wengine katika familia kwa ambao hawakuwepo. Na sio ndani ya siku moja.

Kuna mtu atakuwa safarini, huko aendako hakulala huko, maanake ni kwamba taarifa ataziacha kule anakopaswa kuhesabiwa.

Kuna kaya unaweza kukuta msiba au sherehe, karani itabidi uende wakati mwingine ili kupata taarifa.
Na ndio maana ya siku kuwa zaidi ya moja.
This country doesn't have enough great thinkers.

Na utakuja kusikia hoja hii ikipewa uzito subiri tu great thinkers wazinduke toka usingizini.
Halafu utakuwa umekosa kazi ya sensa safari hii, sio bure
 
Halafu utakuwa umekosa kazi ya sensa safari hii, sio bure
Hapana. Sikuhitaji kabisa.
Hiyo kazi si lelemama japo unapata kipato. Yaani jua lako, mvua yako. Unapandisha milima na mabonde. Unafika mahali unagonga hodi kwa nyumba ya watu, unasikia mbwa wanabweka getini. Unaanza kuuliza maswali hadi mate yanakauka. Aisee, hela tamu lakini kuipata kazi sana!

Halafu wakati huo nilikuwa under 30, sasa hivi umri ushaenda. Acha wadogo zetu wapige kazi. Tuwape tu ushirikiano hawa wazalendo wa nchi.
I wish hizi kazi zingefanyika kidigitali. Taarifa zingetumwa kwa njia ya mfumo maalum. Hii ya kuzunguka mtaani si kazi ndogo ujue!
 
Halafu utakuwa umekosa kazi ya sensa safari hii, sio bure
Ukweli ni kwamba, huwezi kuwa na kazi yako ya maana au biashara zako zinakupa kipato, ukaenda kubanana kwenye ajira za sensa tena ukarani!

Yaani kufight kwenye hizi ajira ni kiashiria cha wazi kabisa cha namna watanzania tulivyo na hali ngumu kiuchumi.
Just imagine umebeba begi lina vitendea kazi, umevaa laba miguuni (ukivaa viatu vya wazi jiandae kujaa vumbi au viatu kukatika) unazunguka nyumba moja baada ya nyingine, unaanza kuuliza maswali takribani 100+ then unajaza taarifa na kutuma mahali husika. Nikwambie tu, hii ni kazi ya kizalendo haihitaji ubrothermen au usister do! Ni kazi ya kikomavu!
 
Wewe nae unakomaza mfupa utafikiri umezaliwa mwaka 2013 na kuendelea, baada ya sensa zote zilizotangulia kuwa zimefanyika. Yaani utofauti wa sensa ya mwaka huu na zile zilizopita ni teknolojia tu labda na wasimamizi, kwamba kule ilikuwa paper work na hapa digital work.

Vingine vyooote vinafanana, kuanzia mapumziko na idadi ya siku za kuhesabu.

Sasa logic ya mapumziko iko wapi ikiwa kwa siku nyingine mhusika wa kaya hatakuwepo?

Hivi great thinkers wa nchi hii ndio kusema wote wameshatangulia mbele za haki???,[emoji848]
 
Vingine vyooote vinafanana, kuanzia mapumziko na idadi ya siku za kuhesabu.
2012 ilikuwa tarehe 26 August, siku ya jumapili. 2002 ilikuwa 25 Aug siku ya jumapili.
Mihula ya shule haikubalishwa. Shule hazikufungwa. Ya mwaka huu mabadiliko ni makubwa.
Kama ya tija kwa taifa ni jambo la heri.
 
Nisahihi sikuhiyo kuwa mapumziko maana tarehe 23 ratiba itasambazwa na karani ili kila mwenyekaya ajulishwe exactly karani atamfikia lini na midagani, pia watu wawe conscious na waache taarifa muhimu nyumbani ikiwama pia no. za nida, anuani za makazi(kama hazijabandikwa),mitanamba nk.
SENSA KWA MAENDELEO ........
 
zoezi la sensa huzingatia pia uzoefu wa sensa miaka ya nyuma. haya mapumziko ni kwa wale waajiriwa na watumishi wa umma a galau wawepo nyumbani siku hiyo. wataku baliana na balozi namna watakvyoweza kufikiwa zoezi linavyoendelea
 
Back
Top Bottom