Ikiwa Tundu Lissu ameridhia kununuliwa gari ya kifahari na wananchi. Akiwa Rais atafuta manunuzi ya V8?

Muonye mwenye BUSARA atasikia,

Lissu ni kiongozi mkubwa baadaye, ni muhimu kumuonya na kumkumbusha matakwa ya wananchi Ili aliingia mamlakani asijevimbiwa kama Hawa waliopo.
 
Halafu hakuna mahala nimemlaani Lissu.

Lissu ni Mbarikiwa hawezi kulaaniwa,

Tunampenda ndio maana tunamwambia kile wananchi maskini wangependa kukiona Toka kwake.

Don't take it personal.
 
Rais gani tena jamani? si tulishakubaliana serikali inaundwa na CCM wengine waendelee kula ruzuku jamani?
Hawezi kuwa Rais toa mfano wa Cheo kingine tafadhali
 
Rais gani tena jamani? si tulishakubaliana serikali inaundwa na CCM wengine waendelee kula ruzuku jamani?
Hawezi kuwa Rais toa mfano wa Cheo kingine tafadhali
Mungu na wananchi wakiamua awe Rais, hayupo wa kupinga .
 
Salaam, Shalom!!

Naomba majibu yawe mafupi na yaliyoshiba HOJA, vyama tuweke pembeni.

NB: Swali gumu linahitaji jibu gumu! Swali jepesi lijibiwe pia kiuwepesi!

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Karibuni 🙏.
Kwenye hiyo unategemea atakuwa rais
 
Halafu hakuna mahala nimemlaani Lissu.

Lissu ni Mbarikiwa hawezi kulaaniwa,

Tunampenda ndio maana tunamwambia kile wananchi maskini wangependa kukiona Toka kwake.

Don't take it personal.
Kipi hicho unapenda kukiona toka kwake Mchungaji zaidi ya hivi anavyofanya sasa..?

Je, furaha yako ni akatae gari atakayopewa na wananchi (Landcruiser Prado V8) ili awe na uhakika wa safari zake na kuizingukia Tanganyika nzima kuamusha watu waliolala ktk usingizi wa ujinga wa kutojua wajibu na haki zao za kisiasa..?
 
Uongozi ni vitendo.

Wananchi hatupendi viongozi wetu kutumia magari ya kifahari, watumie gari himilivu, nzuri lakini Bei nafuu kama land cruiser Mkonga.

Pesa ingine iende kuondoa shd ya wananchi.

Akikataa na kuapa kufuta V8 ,HAKIKA ataungwa mkono na wananchi.

Aliendelea hivyo,

Urais ataisikia tu redioni.

Opinion is not a fact. Ni maoni tu.
 

..Chadema walinunua Ford Ranger kwa ajili ya shughuli za chama. Kwa hiyo tunaweza kusema tunao mfano wa jinsi wanavyotumia fedha za umma ktk masuala ya vitendea kazi vya usafiri.

..V8 ambazo zimeshanunuliwa na serikali ya Ccm zitatumiwa na serikali itakayoingia madarakani, bila kujali ni ya Nccr, Cuf, Act. Jambo la msingi ni serikali mpya kukomesha ununuzi wa ma-V8, na magari mengine ya kifahari, kwa ajili ya watumishi wa umma.

..Kwa upande mwingine, Lissu, au kiongozi mwingine, akinunua gari BINAFSI la fahari, hayo ni maamuzi yake. Kitu ambacho wananchi tunaweza kuhoji ni kama manunuzi hayo yanalingana na KIPATO halali cha mhusika.
 
HOJA IPO kwake sababu pesa hizo ni michango ya wananchi wa kawaida.

Hili jambo linahitaji mjadala mpana.

Kuna namna viongozi hawaelewi wananchi wanataka nn iwe CCM au upinzani🤔
 
HOJA IPO kwake sababu pesa hizo ni michango ya wananchi wa kawaida.

Hili jambo linahitaji mjadala mpana.

Kuna namna viongozi hawaelewi wananchi wanataka nn iwe CCM au upinzani🤔
..lakini Chadema gari zao si Ford Ranger? Kwanini unawalaumu kuhusu V-8 wakati chama magari hayo?
 
..lakini Chadema gari zao si Ford Ranger? Kwanini unawalaumu kuhusu V-8 wakati chama magari hayo?
Kwani Ford ranger walinunua Kwa kuchangiwa na wanachama au ni msaada Toka wafadhili?

Pia ipi tofauti ya Bei kati ya ford na V8?
 
Kwani Ford ranger walinunua Kwa kuchangiwa na wanachama au ni msaada Toka wafadhili?

Pia ipi tofauti ya Bei kati ya ford na V8?

..Chadema kama chama hawana V8 hata moja.

..ford ranger bei yake inaelekeana na toyota hilux / double cabin.

..kwanini unawapakazia kwa matumizi ambayo chama chao hakijayafanya?
 
..Chadema kama chama hawana V8 hata moja.

..ford ranger bei yake inaelekeana na toyota hilux / double cabin.

..kwanini unawapakazia kwa matumizi ambayo chama chao hakijayafanya?
Hapo hujaona Question mark?
 
Salaam, Shalom!!

Naomba majibu yawe mafupi na yaliyoshiba HOJA, vyama tuweke pembeni.

NB: Swali gumu linahitaji jibu gumu! Swali jepesi lijibiwe pia kiuwepesi!

Mungu ibariki Nchi yangu nzuri niipendayo TANZANIA 🇹🇿

Karibuni 🙏.
Ningekuwa na uwezo Tundu Lissu ningemnunulia Rolls Royce wacha hilo la kuchangiwa. Heshimu sana sana na sana mtu aliyekataa hongo ya mtoto wa Samia. Ni watu wachache sana wenye uwezo huo. Badala ya kumpa moyo mtu kama huyu nyie mnakuja na mada za kipumbavu kabisa.
 
Tunaongelea way forward,Kwamba Leo Lissu ni Rais,

Je atafuta matumizi ya madc kwenye misafara, DCs na RCS?

Au atakuwa kama Hawa CCM?

HOJA imejikita hapo!
 
Nasi tungependa kujua msimamo wa Lissu kama kiongozi,

Auonyeshe umma kuwa anaucgungu na pesa za watz, anunue gari nzuri isizidi huo 150ml.

Na aape kufuta manunuzi ya V8 endapo atakuwa Urais.

Watz Si wajinga.
Lisu hana tamaa ndiyo maana hana kashifa ya ufisadi naye kama binadamu atakuwa na madhaifu yake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…