Ikulu, Chamwino: Rais Magufuli ateua Baraza la Mawaziri lenye Wizara 23. Aunda Wizara mpya ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Ikulu, Chamwino: Rais Magufuli ateua Baraza la Mawaziri lenye Wizara 23. Aunda Wizara mpya ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Kwani hilo ni baraza la dini au wanaangalia vigezo ?????????
Vigezooooooo!!!!
Unamaanisha Tanzania nzima kuna waislamu watatu tu Ndio wanakidhi Vigezo vya kua mawaziri???
Anyway I feel sorry kwa waswahili wenzangu waliokuwa wanamshadadia mtu anaeonyesha chuki za dhahiri kwetu
 
Naam umeona mbali sana. 👍🏽
Mimi nilishaula tokea sijazaliwa.Ila Baraza lile acha kabisa......pale Mwugulu sasa anaandaa mswaada wa kuondoa ukomo wa madaraka kwa rais.
 
Tunasema katika baraza la watu 23 waislamu ni watatu haijawahi kutokea tangu Uhuru
 
Vigezooooooo!!!!
Unamaanisha Tanzania nzima kuna waislamu watatu tu Ndio wanakidhi Vigezo vya kua mawaziri???
Anyway I feel sorry kwa waswahili wenzangu waliokuwa wanamshadadia mtu anaeonyesha chuki za dhahiri kwetu
Mmehama kwenye HOJA za kura feki sasa mnarejea katika hisia KONGWE za UDINI ee?!!

Yaani ninyi ni KUHAMISHA MAGOLI TU...

Wangekuwa wako 20 ndipo hapo ROHO YAKO ingekuwa KWATUUU?!!si ndiyo?
 
Matangazo ya moja kwa moja kutoka Ikulu, Chamwino mkoani Dodoma kuhusu Uteuzi uliyofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli leo tarehe 05 Desemba 2020



========
Rais Magufuli pia amewateua kuwa Wabunge Dkt. Doroth Gwajima(Alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya) na Dkt. Leonard Chamuliho (alikuwa Katibu Mkuu Uchukuzi).

Pia Rais Magufuli ameunda Wizara mpya ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.

Orodha ya Mawaziri kama ilivyotangazwa na Katibu Mkuu Kiongozi.

1.Wizara ya Maji - Juma Aweso

2.Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo - Innocent Bashungwa

3.Wizara ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Vijana na wenye ulemavu - Jenister Mhagama

4.Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto - Dkt. Doroth Gwajima

5.Wizara ya Uwekezaji ofisi ya Rais - Profesa Mkumbo Kitila

6.Wizara ya Katiba na Sheria - Dkt. Mwigulu Nchemba

7.Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia - Profesa Joyce Ndalichako

8.Wizara ya Mifugo na Uvuvi -Mashimba Mashauri Ndaki

9.Wizara ya Maliasili na Utalii - Dkt. Ndumbalo Damas

10. Ofisi ya Rais TAMISEMI -Suleiman Jaffo

11. Wizara ya Madini - Dotto Biteko

12. Wizara ya Nishati - Dkt. Medard Kalemani

13. Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi - Mhandisi Dkt Leonard Chamuliho

14. Wizara ya Kilimo - Profesa Adolph Mkenda.

15. Wizara Viwanda na Biashara - Mwambie Geofrey Idelphonce

16.Wizara ya Mambo ya Ndani - George Simbachawene

17. Wizara ya Muungano na Mazingira - Ummy Mwalimu

18. Wizara mpya ya Mawasiliano na Teknolojia ya habari Dkt Faustine Ndugulile
19.Fedha Dkt Philip Mpango
20.Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof Paramagamba Kabudi
21 Ardhi-William Lukuvi
22.Ulinzi na JKT Elias John Kuandikwa
23.Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Capt Mstaafu George Mkuchika.

Nasikitika jinsia haikuzingatiwa kabisa
 
Wakiristo watupu!
Juma Aweso, Ummy Mwalimu, Suleman Jaffo hao ni wakristu pia? Katika wabunge wote angalia ratio ya wakristu na Waislamu utapata jibu.

Waislamu Kuna kitu huwa hamtaki kukubali kuwa swala la elimu dunia hamkulipa kipaumbele toka zamani, wenzenu wakristu walienda sambamba elimu ya dini na elimu ya dunia. Kwa Sasa Waislamu ndo mmekuwa na mwamko wa elimu ya dunia wakati wakristu tayari wamepiga hatua kubwa. Kwa hiyo itachukua muda mrefu kuziba hilo pengo na kuwa na uwiano sawa wa wasomi.

Kwa hiyo kwa Sasa usitegemee kuwe na uwiano sawa katika uongozi ilihali hakuna uwiano sawa wa wasomi Kati ya Waislamu na wakristu.
 
Nini mantiki ya kuundwa wizara mpya ya Teknologia ya Habari, wakati huo huo kuna wizara nyingine ya Habari na wizara nyingine ya Technologia?
Unawezaje ukatenganisha technologia, habari na teknologia ya habari ?
 
Ilikuwepo wakati wa JK
Nini mantiki ya kuundwa wizara mpya ya Teknologia ya Habari, wakati huo huo kuna wizara nyingine ya Habari na wizara nyingine ya Technologia?
Unawezaje ukatenganisha technologia, habari na teknologia ya habari ?
 
Back
Top Bottom