Ikulu, Chamwino: Rais Magufuli ateua Baraza la Mawaziri lenye Wizara 23. Aunda Wizara mpya ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Ikulu, Chamwino: Rais Magufuli ateua Baraza la Mawaziri lenye Wizara 23. Aunda Wizara mpya ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Ndo Mana chadema wanatakiwa kuwa naye makini Sana huyu ni mtu wa ndani kabisa n apengine ana baraka zote kutoka huko jikoni
 
IMG_20201116_194028.jpg
niliamua kusave hii screenshot nione
 
Katika baraza hili lenye mawaziri 23 kwa haraka haraka
-Wanawake 4 (wanaume 19)
-?Waislamu 2 (?Wakristo 21)
-Mchaga 1 (Wasukuma 5+)
-Mzanzibar 0 (watanganyika 23)
 
Halafu nawe unawaza kuna siku utakabidhiwa Tanzania kama kiongozi, kwa fikira hii, hata "unywe gongo ya mapapai" huwezi kuwa!! Umejitakia mwenyewe laana hii. Hakuna namna.
Hivi mnawachukuliaje Waislam? Ingekuwa wameteuliwa Wakristu 3 na Waislam 19 mngenyamaza nyie manaswara? Au mngekuwa mnafundishana ubaguzi wa serikali kwenye vigango vyenu saa hii?
 
Otherwise alichofanya ni kubashiri tu kwa kuangalia trend ya Jiwe ya kufanya teuzi siku za mwisho wa week.
usichukulie kirahisi hivyo, hata ya covid 19 aliisema sana kuwa wanakwenda bungeni viti maalum...ikatokea. It is not a single event alizobashiri ; and coincidence can not fall on Kigogo at all times!
 
Matangazo ya moja kwa moja kutoka Ikulu, Chamwino mkoani Dodoma kuhusu Uteuzi uliyofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli leo tarehe 05 Desemba 2020



========
Rais Magufuli pia amewateua kuwa Wabunge Dkt. Doroth Gwajima(Alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya) na Dkt. Leonard Chamuliho (alikuwa Katibu Mkuu Uchukuzi).

Pia Rais Magufuli ameunda Wizara mpya ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.

Orodha ya Mawaziri kama ilivyotangazwa na Katibu Mkuu Kiongozi.

1. Wizara ya Maji - Juma Aweso

2. Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo - Innocent Bashungwa

3. Wizara ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Vijana na wenye ulemavu - Jenister Mhagama

4. Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto - Dkt. Doroth Gwajima

5. Wizara ya Uwekezaji ofisi ya Rais - Profesa Mkumbo Kitila

6. Wizara ya Katiba na Sheria - Dkt. Mwigulu Nchemba

7. Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia - Profesa Joyce Ndalichako

8. Wizara ya Mifugo na Uvuvi -Mashimba Mashauri Ndaki

9. Wizara ya Maliasili na Utalii - Dkt. Ndumbalo Damas

10. Ofisi ya Rais TAMISEMI -Suleiman Jaffo

11. Wizara ya Madini - Dotto Biteko

12. Wizara ya Nishati - Dkt. Medard Kalemani

13. Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi - Mhandisi Dkt Leonard Chamuliho

14. Wizara ya Kilimo - Profesa Adolph Mkenda.

15. Wizara Viwanda na Biashara - Mwambie Geofrey Idelphonce

16.Wizara ya Mambo ya Ndani - George Simbachawene

17. Wizara ya Muungano na Mazingira - Ummy Mwalimu

18. Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya habari - Dkt Faustine Ndugulile

19. Wizara ya Fedha na Mipango - Dkt. Philip Mpango

20.Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki - Profesa Paramagamba Kabudi

21. Wizara ya Ardhi na Makazi -William Lukuvi

22. Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa - Elias John Kwandikwa

23. Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora - Capt Mstaafu George Mkuchika

Kigwangala wajumbe hawakumuona au?
 
Katika baraza hili lenye mawaziri 23 kwa haraka haraka
-Wanawake 4 (wanaume 19)
-?Waislamu 2 (?Wakristo 21)
-Mchaga 1 (Wasukuma 5+)
-Mzanzibar 0 (watanganyika 23)
Mchagga ni yupi hapo?

Nimejaribu kucheki surname sioni
 
Ndo Mana chadema wanatakiwa kuwa naye makini Sana huyu ni mtu wa ndani kabisa n apengine ana baraka zote kutoka huko jikoni
mimi siwezi kumdharau, akisema kitu nitachukua tahadhali
 
Duu Baraza la Mawaziri la Tanzania mbona halina Wazanzibar? halafu halija balance kwa misingi ya imani!

Msifikiri naangalia kwa ubaguzi lakini ukweli lazima tuuseme haya ni maoni yangu!
 
Juma Aweso, Ummy Mwalimu, Suleman Jaffo hao ni wakristu pia? Katika wabunge wote angalia ratio ya wakristu na Waislamu utapata jibu.

Waislamu Kuna kitu huwa hamtaki kukubali kuwa swala la elimu dunia hamkulipa kipaumbele toka zamani, wenzenu wakristu walienda sambamba elimu ya dini na elimu ya dunia. Kwa Sasa Waislamu ndo mmekuwa na mwamko wa elimu ya dunia wakati wakristu tayari wamepiga hatua kubwa. Kwa hiyo itachukua muda mrefu kuziba hilo pengo na kuwa na uwiano sawa wa wasomi.

Kwa hiyo kwa Sasa usitegemee kuwe na uwiano sawa katika uongozi ilihali hakuna uwiano sawa wa wasomi Kati ya Waislamu na wakristu.
Kama umeweza kuwaza kidini na ukahitimisha kuwa wakristo wanastahili zaidi kwa sababu wamesoma na kuelimika zaidi, sasa Waza pia kikabila halafu chambua hivyo hivyo, na tumia sampuli ya makabila ya wachaga(Northen zone) vs wasukuma (Lake zone) kwenye teuzi hizi za leo au hapo kabla.

Nasubiri uchambuzi wako hapa.
 
Back
Top Bottom