Ikulu, Dar es Salaam: Rais Samia apokea taarifa ya Kikosi Kazi cha Kuratibu Maoni ya wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa

Ikulu, Dar es Salaam: Rais Samia apokea taarifa ya Kikosi Kazi cha Kuratibu Maoni ya wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa

Baraka Mina

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2020
Posts
586
Reaction score
590
Fuatilia matangazo ya moja kwa moja kutoka Ikulu jijini Dar Es Salaam ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndg. Samia Suluhu Hassan anapokea taarifa ya kikosi kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa leo tarehe 21 Machi 2022.

Pia soma > Kikosi Kazi: Tanzania ianze mchakato wa kupata Katiba Mpya baada ya Uchaguzi Mkuu 2025

Baadhi ya NUKUU za Rais Samia

Kikosi kazi mmejihalalishia kuwa na kazi karibu miaka 9 yote iliyobaki na mimi hapa, na huku ndio kunaitwa kujiajiri wenyewe. Lengo letu ni kuwa na siasa zenye tija

Vyama vya siasa na vyombo vya habari tuwe na uhusiano mzuri, nanyi vyombo vya habari msiwe na maslahi na upande wowote, mnatakiwa kuwa kati kati"

Nitaendelea kukutana na vyama vya siasa kuwasikiliza wanataka maboresho yapi, lengo wote twende kwenye reli moja katika kufanya siasa zenye tija kwa nchi yetu"

Katika suala la kanuni za mikutano ya hadhara, sio tu kwamba ziwepo ili mikutano ianze, lakini pia kanuni zianishe atakayekiuka atafanywaje

Watu wetu hawana uelewa wa mambo ya siasa, uzalendo wala elimu ya uraia, watu wangekuwa na elimu ya uraia, uzalendo na elimu ya dunia, mauaji tunayoyashuhudia hii leo yasingekuwepo. Yote hayo hawana, ndio maana wanajifanyia tu

Tukisema tutatoa ruzuku kwa kila chama cha siasa, fedha hizo tutazitoa wapi, lakini tukikubali hilo tutakuwa kama nchi fulani kwamba kila baada ya siku 3 chama kipya cha siasa kinaundwa

Tujiulize kwa hicho tunachokitaka kwamba Tume Huru, tujifunze kwa majirani zetu, je pamoja na kuwa na hizo zinazoitwa Tume Huru hakuna migogoro? Hawatangazi matokeo na kukimbia nchi? Maana halisi ya tume huru ni hasa

Wanawake tusililie tu nafasi za uongozi, lakini tujue pia wajibu wetu kama wanawake,lolote linalotokea katika nchi sisi ndio wa kwanza tunaoumia pamoja na watoto wetu. Kuingiza wanawake katika uongozi wa siasa ni muhimu kwa kuwa sisi tuna ajenda za kuzisimamia

Nitawapa mfano katika mkoa ninaotoka, kuna mwanamke mmoja alipambana akaingia katika nafasi za uongozi, alipoingia tu alisema afadhali na mimi nitapata kununua madhahabu nijipambe, ina maana analoendea huko hakuna. Hii ni historia ya kweli

Uadilifu unaweza kurudi kwa ukali kwamba unakuwa mkali, Ukifanya hivi nitakutoa, hiyo ni nidhamu ya uoga. Tunataka uadilifu ujengwe katika mioyo na sio nidhamu ya uoga, kwamba mimi nafanya hili nisipofanya kuna mtu atakwenda kunichongea

#KaziIendelee
#TunaImaniNaSamia

---
  1. "PCCB (TAKUKURU) hawafanyi kazi vizuri ni kweli; tusiposema hatujengi nyumba nzuri; tutakaposema tutarekebisha na tutajenga nyumba nzuri."
  2. "Unaposema kila chama cha siasa kitapewa ruzuku tutakuwa kama Lesotho, kila baada ya siku mbili chama cha siasa kimeundwa watu wanataka ruzuku...hiyo haitawezekana...Unapounda chama cha siasa, umejipimaje? Utajiendeshaje?"
  3. "Uadilifu umepungua ni kweli; tufanyaje sasa? Ni elimu ya uraia, uzalendo ili kila mmoja alipo ajue anafanya nini ndiyo uadilifu utarudi katika hatua yake."
  4. "Uadilifu unaweza ukarudi kwa ukali lakini tunasema ni nidhamu ya woga. Tunataka uadilifu ujengwe kwenye mioyo na sio nidhamu ya woga."
  5. “Maboresho ya sheria na kanuni za uchaguzi, sawa mtatuambia vipengele gani vinauma, tutajadili kwa pamoja tuone pengine inawezekana tukifanya maboresho huku na mengine yote yatakayofanywa huko pengine lile kelele la Katiba likaishia kwa sababu zile kiu za watu wanapotaka Katiba ibadilishwe zilishafanyiwa kazi huku.”
  6. “Suala la rushwa ni jukumu letu wote, twendeni tukalifanyieni kazi, chaguzi zetu ziende vizuri. Sijui kama tunaweza kufanya 100% lakini tukianza kupunguza ndio tunaelekea huko, vinginevyo wasio kitu hawataingia kwenye nafasi zozote zile.”
  7. "Kuingiza wanawake ndani ya vyama vya siasa ni muhimu sana kwa sababu sisi ndiyo tuna ajenda ya kusimamia."
  8. "Kuna kazi kubwa kweli kufanya wanawake wasimame vizuri kwenye vyama vya siasa. Tusililie tu nafasi za kuingia, tujue na wajibu wetu pia tunapoingia kama wanawake."
  9. "Tuna mambo mengi sana ya kuzungumza kwenye hili taifa kwa faida yetu (wanawake) na taifa letu kwa ujumla lakini kila siku mashaka yapo palepale."
  10. “Izo ‘codes of conduct’ za vyama vya siasa zisiwe za kukandamiza na vizuri mtakua wenyewe mnazitunga, zisikandamize, zisiue vyama vya siasa lakini zilete siasa zenye tija ndani ya nchi, isiwe kila siku tuko kwenye maBBC na CNN huko kila siku ukifungua BBC, CNN Tanzania imefanya hivi, sio ustaarabu kwa kweli, twende na siasa zenye tija.”
 
Sawa sawa maridhiano kwanza Halafu tunavuta muda Hadi 2025 ili tushinde uchaguzi Halafu katiba mpya ndio ipatikane 2025-2030!

!hapo nimemuelewa mama!!
 
Si walishawasilisha hiyo report akina Zitto na rafikize akina Jaji Mutungi...wamerudi tena, khee🥱
 
Sawa sawa maridhiano kwanza Halafu tunavuta muda Hadi 2025 ili tushinde uchaguzi Halafu katiba mpya ndio ipatikane 2025-2030!!hapo nimemuelewa mama!!
2030 watarusha tena hadi 2050

[emoji23][emoji23][emoji23]Chadomo watapata tabu sana

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
 
Hatuna umeme huku mtaani tutaangalia namna gani??

Simu zenyewe charge ipo 19.
 
Leo mama Samia amekisifia kikosi kazi kwa kujihalalishia kuwa na kazi kwa miaka 9 iliyobaki ya urais wake.

Sio kwa ubaya, Ina maana mama Samia ameshajihakikishia kushinda uchaguzi wa 2025??

Basi nitoe pongezi kwake kwa kushinda kabla ya uchaguzi.

Screenshot_20220321-124138_1.jpg
 
Anajisahau tu Mama yetu, hatakiwi kunyanyua mabega.

Binadamu tunapanga na Mungu anapanga na kupangua kadri anavyoamua.
 
Leo mama Samia amekisifia kikosi kazi kwa kujihalalishia kuwa na kazi kwa miaka 9 iliyobaki ya urais wake.

Sio kwa ubaya, Ina maana mama Samia ameshajihakikishia kushinda uchaguzi wa 2025??

Basi nitoe pongezi kwake kwa kushinda kabla ya uchaguzi.

View attachment 2159150
Wanajiajili wenyewe pesa wanalipwa za umma.

Wacha ninyamaze tu.
 
Hii kazi Warioba alishaimaliza siku nyingi, leta rasimu ya Warioba tupashe kiporo.

Kinachofanyika sasa ni ulaghai wa kisiasa tu, watu kama Mutungi na Zitto Kabwe watasimamia maslai ya Taifa tangu lini?
Ulaghai kwa kisiasa kwani dhalimu wako bado yupo?

Si mama anaupiga mwingi?

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
 
Leo mama Samia amekisifia kikosi kazi kwa kujihalalishia kuwa na kazi kwa miaka 9 iliyobaki ya urais wake.

Sio kwa ubaya, Ina maana mama Samia ameshajihakikishia kushinda uchaguzi wa 2025??

Basi nitoe pongezi kwake kwa kushinda kabla ya uchaguzi.

View attachment 2159150
Maana yake ameshajihakikishia hadi 2025 hana mpinzani!

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom