IKULU: Rais Magufuli amteua Dkt. Bashiru Ally Kakurwa kuwa Katibu Mkuu Kiongozi

IKULU: Rais Magufuli amteua Dkt. Bashiru Ally Kakurwa kuwa Katibu Mkuu Kiongozi

Kuna kipindi nilikuwa nafikiri Magufuli anaharibu mambo kwa ushamba tu, kwa ujinga, kwa kutojua, kwa ubishi, na kwa kutosikiliza watu.

Granted, hizo sifa nyingi kama si zote anazo.

Lakini kuna mambo mengi anafanya deliberately, kwa manipulation, Machievallian machinations, calculations etc.

Hapa naona kuna mkakati wa kukisimika chama deep kabisa kwenye civil service huko.

Mkuu mbona chama kimeshajikita muda ndani ya civil service. Kwani hujawahi kusikia swali civil servants wanaloulizwa kila mara na politicians la “Nani anakulipa mshahara?”
 
Kushinda uwezo wako unavyofahamu how unitary government system works.
Dogo bhana. Umeingia chuo kikuu umeanza kusikia hayo majina ya unitary government basi unajiona umejua sana mambo ya utawala na sheria
 
Kwenye sheria kuna msemo, justice must not only be done, it must also seem to be done.

Rais alikuwa na watu wengi sana wa kuwateua katika nafasi hii ya kiserikali isiyotakiwaa kuongozwa kisiasa, akachagua katibu mkuu wa chama chake ambaye ni mtu wa kisiasa.

Katibu Mku huyu ana historia tayari, historia mabayo hawezi kuikana na itamfuata tu huko kwenye civil servant.

Hivi Katibu Mkuu Kiongozi ambaye ashatoa matamko kibao ya kishabiki kwa kuishabikia CCM leo akiwaambia wafanyakazi wa serikali, watumishi wa umma, wasiendekeze siasa sehemu za kazi atachukuliwa serious?

Hivi, watu wakisema Magufuli ana mkakati wa kuingiza siasa za vyama kwenye civil service, atakuwa na point za kujitetea?

Hivi, hakuna watu wengine ambao hawana historia ya chama ambao wangefaa kuwa Katibu Mkuu Kiongozi?

Umeongelea Katiba. Ukweli kwamba kitu hakikatazwi kikatiba haumaanishi kwamba kukifanya ni busara na jambo zuri.

Magufuli kama last custodian of the land hakatazwi kikatiba kuiuza nchi nzima iwe shamba la Emir of Qatar.

Hakuna sehemu ambapo katiba inamkataza kufanya hivyo.

Lakini je, kufanya hivyo itakuwa haki? Itakuwa sawa? Itakuwa busara?
Naunga mkono hoja kwa 100%

Watumishi round hii kazi wanayo! Itakua CCM kila mahali hata ambapo kwenye masuala yasiyopaswa kuingia siasa
 
Nisome tena hapo chini...sheria yao ni moja lakini organized differently...wote wana jina la watumishi wa umma kiswahili kinaweka vizuri...wameajiriwa na umma katika madaraja yao including the president kwakua kwa katiba yetu Mh. Rais pia ni mtendaji na mwanasiasa so anachaguliwa na anaajiriwa na umma
Tofautisha umma (public) na serikali (civil)
 
Kwa hiyo anakuwa Katibu Mkuu wa Chama na Katibu Mkuu Kiongozi kwa wakati mmoja au anaacha kuwa katibu mkuu wa CCM?

Vipi kuhusu muongozo wa utumishi serikalini unaotenganisha mambo ya chama na utumishi wa umma serikalini?

Hata kama atajiuzulu Ukatibu Mkuu CCM, huu uteuzi unaonesha kwamba utumishi serikalini unaenda kupelekwa kichama chama zaidi.
Kwa sasa Dr Bashiru siyo wanasiasa. Ni mtumishi wa umma. Amepewa ajira kwanza ya umma kuanzia tarehe 26/02/2021 kuw balozi. Then akateuliwa kuwa katibu mkuu kiongozi. Maana hiyo nafasi ni post ya watumishi wa umma.
 
Nafikiri Dr Laurean Ndumbaro alikuwa anafaa kumrithi Dr. Kijazi
 
Rudi shule ukasome tena
Tatizo unatafsiri kiingereza kwenda kiswahili

Unafahamu maana ya neno Interchangable au similarities
Anayepaswa kwenda shule ni wewe unayekariri! Similarity haina maana kuwa vitu hivyo ni sawa bali vinafanana.
 
Katibu mkuu wa CCM ndo katibu mkuu Kiongozi.

Mwenyekiti wa CCM ndo amiri jeshi mkuu wa nchi.

Amini nakwambia, nchi hii ni ya vyama vingi
Kweli Nchi ni ya vyama vingi,lakini Chama kinachoshinda Uchaguzi Mkuu ndiyo kinashika Dola! Katiba inasema hivyo!!
 
Kanda ya ziwa tunateseka na digits tunazisoma kama walivo watanzania wengine. Jamaa anakula na masela zake
Hata wwe tukikuweka pale white house lazima utakula na Masela wako pia,tuwe wa kweli,Nani anapenda kula na maadui zake!?
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Back
Top Bottom