Halafu hiyo hati original ni moja tuu? Zanzibar nao wana original yao? If so, wao huwa wanaihifadhi wapi?
Maana inadaiwa kuwa UN wala SMZ hawana Hati ya Mkataba wa Muungano | Zanzibar Daima Online
Mkuu Mwanakijiji usijidhalilishe kiasi hiki kati ya waliokuwepo wakati huo wamekana kuiona hiyo hati sasa na wewe unatuletea hadith za kusadikika eti Unalinganisha ndoa na suala la Huu muungano umetia aibu kuleta hoja mufilisi za CCM
Hiyo no fax no. Imetumwa tarehe 14 April 2013imetokea wapi hiyo?kwa nini ikulu inachanganya watu? Si wanasema walikuw wameitunza ilikuwa mahali sasa hiyo kutumwa kwa fax ilikuwa wapi
Tundu Lissu anahoja nzuri sana.Tatizo ni kusema kuwa HATI hiyo haipo...nahisi kuna namna ya utunzaji wa Vitu muhimu na kuna utaratibu wa kuvitoa...Siyo kila kitu kukiweka weka hovyo tu. Pili kama hiyo hati ni Original huoni kuwa Tundu Lissu na kundi lake watakuwa wameaibika? Kwa jinsi tulivyo mpa sifa leo halafu ije onekana tumetoa sifa kipumbavu aisee itaniuma sana.
Hii ni ipi? Bila shaka itakuwa ni ile ya kuchakachua yenye saini za kughushi!
Kama UN haipo, kama Zanzibar haipo na Bara ni ile ya kughushi. Ikulu wanataka kumdanganya nani????
This is too late for them. Tundu Lissu ana DATA ZOTE KUHUSU HATI YA MUUNGANO!Kama kuna ukweli wa hiyo HATI YA Muungano jana Wasingelizimia runinga Kamanda Lissu. Wapeleke upuuzi wao huko!!
Mkuu naunga mkono hoja yako kwa 100%... Kama kuishi na mwanamke kwa miaka 2 inatambulika kisheria kuwa ni ndoa halali iweje watu walioishi zaidi ya miaka 50 wamezaliana, wameendesha mambo yao pamoja, wamekabiliana na changamoto mbalimbali kwa umoja wao IWEJE leo tuseme eti Muungano ni batili kwakuwa eti cheti hakipo! Makubaliano au muungano ni zaidi karatasi yenye maandishi ya watu wawili! Muungano huu Unawakilisha Muungano wa Jamii ya watu wa Znz na Watu wa bara na umedumu kwa nusu karne mpaka sasa! Ukiangalia kwa undani utagundua kuwa pande zote mbili yaani CCM na UKAWA wote wako bias ile mbaya! Mifumo wanayopendekeza yanajikita kwenye political gain zaidi! CCM wajua kuwa ndani ya mfumo wa dola mbili wataendelea kutawala milele daima, UKAWA wanajua kuwa ndani ya dola tatu CCM itakosa nguvu na kuachia ngazi! Kama kweli wote wangekuwa na dhamira ya kweli ninauhakika leo hii Tanzania Ingekuwa Moja chini ya Serikali Moja yenye kuendeshwa kwa mfumo wa Majimbo kama zilivyo nchi za wenzetu..
Taarifa nilizozipata muda huu ni kuwa Waandishi wa habari wameitwa Ikulu na Katibu Mkuu Kiongozi lengo ni kuwaonyesha Hati Ya Muungano na kukata mzizi wa Fitina Kwa wajumbe wa bunge la Katiba. Tutawajulisha hapa hapa...
Hii ni sehemu ya Mkataba wa Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar...
Zitakuwa mbili, moja iko Tanganyika moja iko Zanzibar, ulitaka zote zikae Tanganyika?
it is too late to catch the plane at this juncture
Lissu na MBOWE ni Majembe.
Kwani kuna mgogoro kati ya Tanzania na Zanzibar mpaka kuelekea kudai hati hii kuoneshwa? Mh lisu acha kutuvuruga.
Hizo number za fax ni za city centre hapo Dar, kama ni hivyo ni sawa na mie niambiwe nilete cheti cha form wakati mie ni std 7 nachofanya ni kuchukua cheti cha mtu na kukitoa copy then nabandika jina langu alafu ninakituma kwa fax. (Nawaza kwa sauti tu)