Kikwete awaita Mbowe,Lipumba,Mbatia Ikulu
Ni Jumapili na Jumananne ijayo
Mbowe amtetea Lissu, ameonewa
Rais Jakaya Kikwete
Kasoro hizo ni kutoshirikishwa kwa Zanzibar, madaraka ya Rais ya kuteua wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba na kuvunjwa kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba baada ya kuwasilisha Rasimu badala ya kuendelea kuwapo hadi kura ya maoni.
Vyama hivyo licha ya wabunge wake kususia Bunge, pia vimeunda ushirikiano wa kupinga mchakato wa katiba kwa maelezo kuwa umehodhiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Tayari wenyeviti wake Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), Freeman Mbowe (Chadema) na James Mbatia (NCCR-Mageuzi) wameshafanya mikutano ya kadhara jijiji Dar es Salaam na Zanzibar na kesho kutwa vyama vyao vimeandaa maadamano ya nchi nzima na baadaye kufanya mikutano mingine katika mikoa yote kuwashawishi wananchi waukatae mchakato huo.
Aidha, vyama hivyo na makundi ya wanaharakati wanamtaka Rais Kikwete asiusaini muswada huo kwa maelezo kuwa utaleta katiba mbovu ambayo haina malahi kwa taifa.
Katika hatua nyingine, Ikulu imekanusha taarifa ambazo jana ziliingizwa katika mitandao ya kijamii na kusambazwa zikidai kuwa Rais Kikwete ametia saini muswada huo.
Ikulu ilisema Kwanza, Ofisi ya Rais haijapokea Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na kwamba inawezekana muswada huo umekwishakutumwa kutoka Bungeni, lakini haujamfikia Rais, hivyo, kama haujamfikia, hawezi akawa ameutia saini