Ila biashara nyingine Sinza zinachekesha sana

Ila biashara nyingine Sinza zinachekesha sana

Melki Wamatukio

JF-Expert Member
Joined
May 3, 2022
Posts
6,156
Reaction score
10,974
Naomba nimtumie rafiki yangu kama kidubwasha cha mfano.

Aliuza kiwanja cha urithi kule Nanjilinji, akauza na nyumba aliyopewa pale Mburahati. Akanunua mzigo wa friji na Tv za Sumsung za kutosha, pesa iliyobaki akakodi fremu Sinza, akaajiri kadadaa kamsaidia kuingiza maokoto

Baada ya miezi mitatu kupita, alikafukuza, kisha akamtaka mkewe asimamie maokoto. Mwezi mmoja tena, nilishangaa sana kumkuta yeye mwenyewe golini. Wiki mbili tena nikawa napita mchana namkuta yeye akiwa ameuchapa tu huku udenda ukimmwagika mchana kweupe, siku si nyingi mbeleni nikawa nawakuta yeye na mkewe wameuchapa huku wanakoroma fofofo

Biashara kubwa kubwa zinahitaji connections, social media sponsoring, location nzuri ya fremu, ukarimu wa muuzaji, uhitaji wa bidhaa na mtazamo juu ya hadhi ya watu unaokwenda kuwauzia. Inafikia hatua mpaka msosi wa mchana hupigi ilihali una friji la Boss la 2mil dukani, inachekesha sana. Wateja hawaonekani dukani, basi achukue hata mafuta ya manabii, wapii, au amtafute mshana jr wapande kilingeni, wapi! Inasikitisha sana

Mara mia angewaza hata kufungua duka la nafaka kwa kweli. Ni hayo tu
 
Hizo pesa Si angepeleka utt aims ....
anae waza utajiri hawz weka hela uko asubli aslimia 7

kitendo chakuweka utt aims means huna matumiz ya hizo ela sasa wew ni mzee had ukose chakufanya? au woga wa kupotza ela?
sio kila uwekezaji unakufa kijana au wew unaona sawa ueke 30Mil afu uwe unapewa 250k-300k kila mwenzi kweli?

yani hapo umempa mtu 30mil akazungushe aje kukupa gawio ambalo hata akulipe mwaka huwez even nunua plot
 
anae waza utajiri hawz weka hela uko asubli aslimia 7

kitendo chakuweka utt aims means huna matumiz ya hizo ela sasa wew ni mzee had ukose chakufanya? au woga wa kupotza ela?
sio kila uwekezaji unakufa kijana au wew unaona sawa ueke 30Mil afu uwe unapewa 250k-300k kila mwenzi kweli?

yani hapo umempa mtu 30mil akazungushe aje kukupa gawio ambalo hata akulipe mwaka huwez even nunua plot
Kuliko kukurupuka kufanya biashara kwa kuiga bora uweke benki kwenye usalama. Siku zote ukipata fedha za mkupuo, ni vizuri ukazituliza kwanza sehemu kama benki wakati ukifikiri cha kufanya. Na siku ukiamua kufanya biashara ni vizuri uanze na mtaji kidogo sana ili upate uzoefu kwanza.
 
Back
Top Bottom