Melki Wamatukio
JF-Expert Member
- May 3, 2022
- 6,156
- 10,974
Naomba nimtumie rafiki yangu kama kidubwasha cha mfano.
Aliuza kiwanja cha urithi kule Nanjilinji, akauza na nyumba aliyopewa pale Mburahati. Akanunua mzigo wa friji na Tv za Sumsung za kutosha, pesa iliyobaki akakodi fremu Sinza, akaajiri kadadaa kamsaidia kuingiza maokoto
Baada ya miezi mitatu kupita, alikafukuza, kisha akamtaka mkewe asimamie maokoto. Mwezi mmoja tena, nilishangaa sana kumkuta yeye mwenyewe golini. Wiki mbili tena nikawa napita mchana namkuta yeye akiwa ameuchapa tu huku udenda ukimmwagika mchana kweupe, siku si nyingi mbeleni nikawa nawakuta yeye na mkewe wameuchapa huku wanakoroma fofofo
Biashara kubwa kubwa zinahitaji connections, social media sponsoring, location nzuri ya fremu, ukarimu wa muuzaji, uhitaji wa bidhaa na mtazamo juu ya hadhi ya watu unaokwenda kuwauzia. Inafikia hatua mpaka msosi wa mchana hupigi ilihali una friji la Boss la 2mil dukani, inachekesha sana. Wateja hawaonekani dukani, basi achukue hata mafuta ya manabii, wapii, au amtafute mshana jr wapande kilingeni, wapi! Inasikitisha sana
Mara mia angewaza hata kufungua duka la nafaka kwa kweli. Ni hayo tu
Aliuza kiwanja cha urithi kule Nanjilinji, akauza na nyumba aliyopewa pale Mburahati. Akanunua mzigo wa friji na Tv za Sumsung za kutosha, pesa iliyobaki akakodi fremu Sinza, akaajiri kadadaa kamsaidia kuingiza maokoto
Baada ya miezi mitatu kupita, alikafukuza, kisha akamtaka mkewe asimamie maokoto. Mwezi mmoja tena, nilishangaa sana kumkuta yeye mwenyewe golini. Wiki mbili tena nikawa napita mchana namkuta yeye akiwa ameuchapa tu huku udenda ukimmwagika mchana kweupe, siku si nyingi mbeleni nikawa nawakuta yeye na mkewe wameuchapa huku wanakoroma fofofo
Biashara kubwa kubwa zinahitaji connections, social media sponsoring, location nzuri ya fremu, ukarimu wa muuzaji, uhitaji wa bidhaa na mtazamo juu ya hadhi ya watu unaokwenda kuwauzia. Inafikia hatua mpaka msosi wa mchana hupigi ilihali una friji la Boss la 2mil dukani, inachekesha sana. Wateja hawaonekani dukani, basi achukue hata mafuta ya manabii, wapii, au amtafute mshana jr wapande kilingeni, wapi! Inasikitisha sana
Mara mia angewaza hata kufungua duka la nafaka kwa kweli. Ni hayo tu