Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
RUdia kusoma vizuri mkuu,. Ningejuaje kama niko na na laki6 na 15 bila kuambiwa na kupewa statement?,. Na nilirudia kujaza Bps upyaNimekuamini kooooote, ila pale ulipotoa pesa bila kuomba statement kama 1.5mil. imeingia, na kama haitoshi, ukaambiwa kabisa pesa hiyo hamna.., hapo nimegoma kuamini..
Bora hata ingekua wameniahidi chochote kitu😄😄🙌U
Uchawi upo Ila hapa ametengenezwa akili yake kutokana na namna matapeli walivyojiweka kimwonekano wao, na yale mazingira waliyoyatengeneza ya kuaminika Kwa kuwa na gari. Pia ni lazima Kuna mtu ndani ya bank kauza majina kamili ya mtapeliwa. Halafu kuna kitu bidada ametuficha, huenda aliahidiwa Asante hii ndiyo ikawa chambo ya kumshawishi apoteze muda wake kufanya hilo zoezi lililomgharimu.
Basi mimi hao watu wanaotumia hayo mambo walishanishindwa,Hizo dawa nazijua, zishatumika sana kwangu hadi nikaona isiwe kesi acha nikajigange..😅😅😅
watu tunaofanya kazi za kukopesha huku mitaani tunatafuniwa sana hizo dawa
kwa kesi yako wewe, hao watu ni makonki.masta si mchezo, kuna Jini la utambuzi huwa wanalo so kabla ya kuongea na wewe unarushiwa kifurushi kwanza ndio unakaa sawa
Utapeli wa papo kwa papo kweli wajinga ndio utapeliwa ila Upo utapeli wa mikakati huo ndio mbaya zaidi, Hata wewe huwezi kuruka hata kidogoKutapeliwa huwa ni ujinga tu, na pia kinachonipa hasira zaidi ni watu kuamini kuwa ni uchawi.
Kuna mpuuzi mmoja eti alikuwa ananipa dili la biashara ya madini sasa nikimuangalia usoni kapauka balaa hala kachomekea nikiangalia viatu soli zimelika upande mmoja.Nilitaka kucheka ila nikamkaushia coz sisi wanaume utafutaji wetu ni jasho na damu.Mpuuzi mwingine eti aliniomba nimuazime simu eti amfahamishe mwenyeji wake amefika hakujua kwamba nna code zake tayariAisee
Haha😂,. Kwamba anauza madini halafu mwenyewe kapaukaKuna mpuuzi mmoja eti alikuwa ananipa dili la biashara ya madini sasa nikimuangalia usoni kapauka balaa hala kachomekea nikiangalia viatu soli zimelika upande mmoja.Nilitaka kucheka ila nikamkaushia coz sisi wanaume utafutaji wetu ni jasho na damu.Mpuuzi mwingine eti aliniomba nimuazime simu eti amfahamishe mwenyeji wake amefika hakujua kwamba nna code zake tayari
Ujue kuna vitu vingine vinachekesha sana just imagine viatu soli zimelika upande mmoja,sura imepauka kama fuso lililotoka shamba kubeba mazao katikati ya msimu wa mvua.Haha😂,. Kwamba anauza madini halafu mwenyewe kapauka
Dah!,pole mkuu,wale hata sijui inakuwaje mtu unajikuta unahisi hapa SI salama,ila Kuna roho inakuambia,angalia uone mwisho wao nishawahi tapeliwa kijinga buguruni pale,nilijicheka sana,wiki ilopita nimetapeliwa na kijana wa tigo ila jiji la dar bhana,matapeli Wana moto wao wa ziada wanaturudisha nyuma sana dah!.Huu mwaka umekua wa hovyo mapema mnoo aisee,
Habari zenu kwanza wakuu
Mwenzenu jana nimetapeliwa, na nikiri tu kuwaambia uchawi upo wakuu, Ilikua jana kuna hela nilipatiwa nikamlipie dogo Ada, Nimeenda bank( NMB)nimelipa, ile wakati natoka nikawa naelekea ile njia ya sokoni ili nikapite vile NBC then Mtaa wa zanzibar nichukue baadhi ya vitu halafu nirudi Nyumbani.. Asa wakati natembea mbele yangu kulikua na Gari Hillux ( sijui ndio hilohilo jina, ila ni haya wanatembeleaga sana wakandarasi sikufanikiwa kukariri plate number zake) Limeandikwa St. Joseph ila sikuweza kumalizia ni St Joseph nini maana kuna mtu alikua ameegemea pale kwenye Maandishi..
Napita akaniita kwa majina yangu matatu kabisa, Dada Lee habari?,, nikaitikia salama za kwako?, akanijibu tu safi za masiku nikamwambia salama nikawa nataka kuendelea kuondoka sikuwaza kwasabu nilijua huenda mteja niliwahi kumuhudumia kunijua majina yangu sio kesi,. Kabla sijafika mbali akaniita tena Akaniambia nashida mara moja naomba nisaidie nikamuuliza shida gani?,. Akasema yuko na sister mle ndani na kweli alishusha kioo ni mama mmoja hivi kavaa mavazi yale ya masista,.
Akaniambia mwanangu nina shida naomba nisaidie,. Nilikua natoa hela pale Atm bahati mbaya nimekosea pin mara3, Kadi Yangu imemezwa nasiwezi kwenda ndani kutoa sina kitambulisho,, sasa nataka uende kuna mtu nimeongea nae akahamishie hela kwenye account yako halafu utoe unipatie,,. ( Kwanza kwa maelezo kama hayo wakuu mtu mwenye akili timamu anaona kabisa hayana mashiko, kwanza kutoa hela kwenye Account yako na kitambulisho wapi na wapi?, alijuaje nina NMB account?, na kwanini asimtume yule kijana??,,. )
Basi dada enu ndo nlikua nisharogwa nahisi nikasema sawa,. Nipe namba ya huyo mtu akasema ukienda tu atakuona akachukua karatasi akaandika kiasi Tsh. 1.5m na akaomba nimtajie namba yangu ya Account nikamtajia basi nikaingia ndani, Mwenzenu nikiri tu sikua naelewa chochote mpaka wakati huo😥 ,. Nikaenda moja kwa moja nimejaza slip ya kutoa hizo hela na ni Account namba yangu niliandika,. Nimekaa foleni mpaka nimefika dirishani yule dada ananiambia mbona Acount yako haina hilo salio dada?,. Kiukweli sikua na hiyo hela ila akili yangu ilikua inaniambia kuna hela zinaingia so itakuwa ipo,. Nikamwambia yule dada basi tutoe kwanza hiyo iliyokuwepo nikarudi kujaza slip upya nikatoa laki6 na 15,. Nikarudi kule nje nikamwambia yule sista bado hawajaingiza ipo ileile yangu akaniambia nipe hiyo kwanza sisi tumwahi mgojwa wewe kaa dakika tano nenda tena watakua washahamishia hela kwako na sisi tunakuja mda sio mrefu,. Si nikakubali nimekaa weeee Pale nje sokoni kila nikienda ndani naambiwa hakuna salio..
Baadae sana ndio napata wazo hawa watakua washanitapeli maana hawakunipa hata namba yao, na Namba yao ya Account wala chochote ile karatasi waliandika tu kiasi na namba yangu ya account niliyowatajia ( Aisee jamani nimelia jana tena sanaaa),. Nikawafata wale walinzi nikawaambia nikawaelekeza na walikokua wamepark gari wanasema kule mbali sana Cctv camera haziwezi zinaonyesha kitu ( Ni kule karibu na mlango wa kuingilia soko kuu kwa mbele kidogo kama unataka Ukunje kona uende NBC),. Polisi nako ndio vilevile jana hamna hata cha maana nilijibiwa,. Na sijui ile gari ilikua ni ya St. Joseph University, St. Joseph Primary school, Hospital au ni nini??.
Nachoshukuru ni kwamba nilifanikiwa tu kulipa Ada ya dogo maana Bila hivyo walahi mzee angenikata kichwa au yeye afe kwa Pressure,.
Ila kuna watu ni wakatili sana, mlaaniwe nyie wakujiita watumishi wa Mungu halafu kumbe ni wezi,. For real wamenitia Umasikini maana ndio ilikua hela yangu ya mwisho. Mwaka ushakua wa Hovyo huu,. Tuwe makini jamani matapeli bado wapo na ninahisi wanatumia uchawi maana sio bure🤔😭
Jiji la dar linafundisha kutokuamini watu,na hasa wanaoomba msaada wowote ule,ukisikiliza tu bhas unalizwa.Pole Sana, uzuri kutapeliwa ni mara moja Tu. Hutatapeliwa tena
Angalau maana kuna uongo ambao kidogo unakaribiana na ukweli,lakini uongo wake na ukweli ulikua mbingu na ardhiHaha😄,. Angekuwa smart kidogo ungeshawishika lakini
Mtu afanye nini ili hizo dawa za kutafuniwa zisimpumbaze hadi kutapeliwa?Hizo dawa nazijua, zishatumika sana kwangu hadi nikaona isiwe kesi acha nikajigange..😅😅😅
watu tunaofanya kazi za kukopesha huku mitaani tunatafuniwa sana hizo dawa
kwa kesi yako wewe, hao watu ni makonki.masta si mchezo, kuna Jini la utambuzi huwa wanalo so kabla ya kuongea na wewe unarushiwa kifurushi kwanza ndio unakaa sawa
Sasa doktori umeongea point muhimu sana,sasa usipojiamini mwenyewe si ndo utatapeliwa kabisaPole Sana.
Ulivyoona St Joseph na Sister .
Yawezekana huyo kavaa tu vazi Ila sio sister then mambo ya hela ni very sensitive kumruhusu mtu afanye alichofanya inafikirisha sana.
Pole Sana kwenye mambo ya hela unabidi kuwa makini Sana trust no body even ur self.
Akaunti inakuwaje na laki 6 kama kuna 1.5mil. imeingia? Hiyo ndio point yangu iliyoganya nigome kukuaminiRUdia kusoma vizuri mkuu,. Ningejuaje kama niko na na laki6 na 15 bila kuambiwa na kupewa statement?,. Na nilirudia kujaza Bps upya
Anyways lishapita🙌🙌