Ila kutapeliwa kunauma wakuu

Ila kutapeliwa kunauma wakuu

hakuna uchawi wala nini ni ujinga na tamaa tu ulijua utapata chochote ukifanikisha
 
Nimekuamini kooooote, ila pale ulipotoa pesa bila kuomba statement kama 1.5mil. imeingia, na kama haitoshi, ukaambiwa kabisa pesa hiyo hamna.., hapo nimegoma kuamini..
RUdia kusoma vizuri mkuu,. Ningejuaje kama niko na na laki6 na 15 bila kuambiwa na kupewa statement?,. Na nilirudia kujaza Bps upya

Anyways lishapita🙌🙌
 
U

Uchawi upo Ila hapa ametengenezwa akili yake kutokana na namna matapeli walivyojiweka kimwonekano wao, na yale mazingira waliyoyatengeneza ya kuaminika Kwa kuwa na gari. Pia ni lazima Kuna mtu ndani ya bank kauza majina kamili ya mtapeliwa. Halafu kuna kitu bidada ametuficha, huenda aliahidiwa Asante hii ndiyo ikawa chambo ya kumshawishi apoteze muda wake kufanya hilo zoezi lililomgharimu.
Bora hata ingekua wameniahidi chochote kitu😄😄🙌
 
Ndio maana Mimi Nina njia zangu za kufanya pindi tu nikikutana na watu nisiowaelewa basi kama wana Nia mbaya hawawezi kufanya kitu, sisi tuna nguvu ndani yetu.
Huwa unafanyaje mkuu,. Tujuze kwa faida ya wote basi mkuu
 
Hizo dawa nazijua, zishatumika sana kwangu hadi nikaona isiwe kesi acha nikajigange..😅😅😅

watu tunaofanya kazi za kukopesha huku mitaani tunatafuniwa sana hizo dawa

kwa kesi yako wewe, hao watu ni makonki.masta si mchezo, kuna Jini la utambuzi huwa wanalo so kabla ya kuongea na wewe unarushiwa kifurushi kwanza ndio unakaa sawa
Basi mimi hao watu wanaotumia hayo mambo walishanishindwa,

Mimi ipo hivi, Nkikutana na watu wa aina hiyo baada ya salamu fupi ( majibu yangu huwa ni mafupi kwa mtu ambae simfahamu )

Akileta hoja au jambo lake ( special case kama alichofanyiwa huyu mtoa mada ) huwa sijibu kitu kwanza, Nitakuangalia kwenye macho yako direct bila kukwepesha kwa zaidi hata sec 30, Baada ya hapo huwa wanatetemeka wenyewe na wanaondoka kwa aibu sanaa wengine hata kukimbia
 
Kutapeliwa huwa ni ujinga tu, na pia kinachonipa hasira zaidi ni watu kuamini kuwa ni uchawi.
Utapeli wa papo kwa papo kweli wajinga ndio utapeliwa ila Upo utapeli wa mikakati huo ndio mbaya zaidi, Hata wewe huwezi kuruka hata kidogo
Na unatapeliwa kisha kesho yake unakutana na huyo huyo tapeli na atakununulia vinywaji na kula nyama choma kwa wingi alafu anakutapeli kwa mara nyingine

Yani anahakikisha kakumaliza hela zote hata za kumfuatilia na mwisho unaweza kukaa hata ndani na muhanga ni wewe

Kiufupi mambo ni mengi sana hapa Duniani, aina hii ya utapeli ni mbaya sana

Mimi naishi kwenye maisha ya tahadhari na umakini mkubwa kama jasusi kwa sasa hivi.
 
Kuna mpuuzi mmoja eti alikuwa ananipa dili la biashara ya madini sasa nikimuangalia usoni kapauka balaa hala kachomekea nikiangalia viatu soli zimelika upande mmoja.Nilitaka kucheka ila nikamkaushia coz sisi wanaume utafutaji wetu ni jasho na damu.Mpuuzi mwingine eti aliniomba nimuazime simu eti amfahamishe mwenyeji wake amefika hakujua kwamba nna code zake tayari
 
Kuna mpuuzi mmoja eti alikuwa ananipa dili la biashara ya madini sasa nikimuangalia usoni kapauka balaa hala kachomekea nikiangalia viatu soli zimelika upande mmoja.Nilitaka kucheka ila nikamkaushia coz sisi wanaume utafutaji wetu ni jasho na damu.Mpuuzi mwingine eti aliniomba nimuazime simu eti amfahamishe mwenyeji wake amefika hakujua kwamba nna code zake tayari
Haha😂,. Kwamba anauza madini halafu mwenyewe kapauka
 
Huu mwaka umekua wa hovyo mapema mnoo aisee,

Habari zenu kwanza wakuu

Mwenzenu jana nimetapeliwa, na nikiri tu kuwaambia uchawi upo wakuu, Ilikua jana kuna hela nilipatiwa nikamlipie dogo Ada, Nimeenda bank( NMB)nimelipa, ile wakati natoka nikawa naelekea ile njia ya sokoni ili nikapite vile NBC then Mtaa wa zanzibar nichukue baadhi ya vitu halafu nirudi Nyumbani.. Asa wakati natembea mbele yangu kulikua na Gari Hillux ( sijui ndio hilohilo jina, ila ni haya wanatembeleaga sana wakandarasi sikufanikiwa kukariri plate number zake) Limeandikwa St. Joseph ila sikuweza kumalizia ni St Joseph nini maana kuna mtu alikua ameegemea pale kwenye Maandishi..

Napita akaniita kwa majina yangu matatu kabisa, Dada Lee habari?,, nikaitikia salama za kwako?, akanijibu tu safi za masiku nikamwambia salama nikawa nataka kuendelea kuondoka sikuwaza kwasabu nilijua huenda mteja niliwahi kumuhudumia kunijua majina yangu sio kesi,. Kabla sijafika mbali akaniita tena Akaniambia nashida mara moja naomba nisaidie nikamuuliza shida gani?,. Akasema yuko na sister mle ndani na kweli alishusha kioo ni mama mmoja hivi kavaa mavazi yale ya masista,.
Akaniambia mwanangu nina shida naomba nisaidie,. Nilikua natoa hela pale Atm bahati mbaya nimekosea pin mara3, Kadi Yangu imemezwa nasiwezi kwenda ndani kutoa sina kitambulisho,, sasa nataka uende kuna mtu nimeongea nae akahamishie hela kwenye account yako halafu utoe unipatie,,. ( Kwanza kwa maelezo kama hayo wakuu mtu mwenye akili timamu anaona kabisa hayana mashiko, kwanza kutoa hela kwenye Account yako na kitambulisho wapi na wapi?, alijuaje nina NMB account?, na kwanini asimtume yule kijana??,,. )

Basi dada enu ndo nlikua nisharogwa nahisi nikasema sawa,. Nipe namba ya huyo mtu akasema ukienda tu atakuona akachukua karatasi akaandika kiasi Tsh. 1.5m na akaomba nimtajie namba yangu ya Account nikamtajia basi nikaingia ndani, Mwenzenu nikiri tu sikua naelewa chochote mpaka wakati huo😥 ,. Nikaenda moja kwa moja nimejaza slip ya kutoa hizo hela na ni Account namba yangu niliandika,. Nimekaa foleni mpaka nimefika dirishani yule dada ananiambia mbona Acount yako haina hilo salio dada?,. Kiukweli sikua na hiyo hela ila akili yangu ilikua inaniambia kuna hela zinaingia so itakuwa ipo,. Nikamwambia yule dada basi tutoe kwanza hiyo iliyokuwepo nikarudi kujaza slip upya nikatoa laki6 na 15,. Nikarudi kule nje nikamwambia yule sista bado hawajaingiza ipo ileile yangu akaniambia nipe hiyo kwanza sisi tumwahi mgojwa wewe kaa dakika tano nenda tena watakua washahamishia hela kwako na sisi tunakuja mda sio mrefu,. Si nikakubali nimekaa weeee Pale nje sokoni kila nikienda ndani naambiwa hakuna salio..

Baadae sana ndio napata wazo hawa watakua washanitapeli maana hawakunipa hata namba yao, na Namba yao ya Account wala chochote ile karatasi waliandika tu kiasi na namba yangu ya account niliyowatajia ( Aisee jamani nimelia jana tena sanaaa),. Nikawafata wale walinzi nikawaambia nikawaelekeza na walikokua wamepark gari wanasema kule mbali sana Cctv camera haziwezi zinaonyesha kitu ( Ni kule karibu na mlango wa kuingilia soko kuu kwa mbele kidogo kama unataka Ukunje kona uende NBC),. Polisi nako ndio vilevile jana hamna hata cha maana nilijibiwa,. Na sijui ile gari ilikua ni ya St. Joseph University, St. Joseph Primary school, Hospital au ni nini??.

Nachoshukuru ni kwamba nilifanikiwa tu kulipa Ada ya dogo maana Bila hivyo walahi mzee angenikata kichwa au yeye afe kwa Pressure,.

Ila kuna watu ni wakatili sana, mlaaniwe nyie wakujiita watumishi wa Mungu halafu kumbe ni wezi,. For real wamenitia Umasikini maana ndio ilikua hela yangu ya mwisho. Mwaka ushakua wa Hovyo huu,. Tuwe makini jamani matapeli bado wapo na ninahisi wanatumia uchawi maana sio bure🤔😭
Dah!,pole mkuu,wale hata sijui inakuwaje mtu unajikuta unahisi hapa SI salama,ila Kuna roho inakuambia,angalia uone mwisho wao nishawahi tapeliwa kijinga buguruni pale,nilijicheka sana,wiki ilopita nimetapeliwa na kijana wa tigo ila jiji la dar bhana,matapeli Wana moto wao wa ziada wanaturudisha nyuma sana dah!.
 
Hizo dawa nazijua, zishatumika sana kwangu hadi nikaona isiwe kesi acha nikajigange..😅😅😅

watu tunaofanya kazi za kukopesha huku mitaani tunatafuniwa sana hizo dawa

kwa kesi yako wewe, hao watu ni makonki.masta si mchezo, kuna Jini la utambuzi huwa wanalo so kabla ya kuongea na wewe unarushiwa kifurushi kwanza ndio unakaa sawa
Mtu afanye nini ili hizo dawa za kutafuniwa zisimpumbaze hadi kutapeliwa?
 
Yan nimekumbuka maongezi yangu mimi na wewe hivi karibuni katika uzi fulani hivi,kwamba kuna mtu alikosea shilingi laki mbili akatuma katika namba yako kimakosa,halafu wewe ukahamishia katika namba yako ya halotel

Na ukasema siku hizi huna huruma kabisa kwakuwa ushatapeliwa sana,je huenda hela ya watu ndio imerudi na ziada juu?

Pole sana kpnz
 
Pole Sana.


Ulivyoona St Joseph na Sister .

Yawezekana huyo kavaa tu vazi Ila sio sister then mambo ya hela ni very sensitive kumruhusu mtu afanye alichofanya inafikirisha sana.

Pole Sana kwenye mambo ya hela unabidi kuwa makini Sana trust no body even ur self.
Sasa doktori umeongea point muhimu sana,sasa usipojiamini mwenyewe si ndo utatapeliwa kabisa
 
RUdia kusoma vizuri mkuu,. Ningejuaje kama niko na na laki6 na 15 bila kuambiwa na kupewa statement?,. Na nilirudia kujaza Bps upya

Anyways lishapita🙌🙌
Akaunti inakuwaje na laki 6 kama kuna 1.5mil. imeingia? Hiyo ndio point yangu iliyoganya nigome kukuamini
 
Back
Top Bottom