Ilala: DC Sophia Mjema athibitisha wagonjwa wa COVID-19 hospitali ya Amana kuleta fujo na kutaka kuondoka wakajitibie nyumbani

Bila shaka mheshimiwa atasema wasibughuziwe, waachwe warudi nyumbani kujifukiza

Hospitalini hawapatiwi dawa kwasababu madaktari na manesi wanaogopa kuambukizwa kwani hawana vitendea kazi vya kujikinga na maambukizi [PPE]; mkuu wa nchi nae anakuja na kusema watu watumie dawa za kienyeji kama kujifukiza kunaponya covid-19!!! Matokeo yake ndio havo wagonjwa wanarudi nyumbani kujifukiza. Matamshi ya Magufuli hayasaidii nchi kupambana na huu ugonjwa bali yanaleta maafa zaidi kwa jamii.
 
This could be positive response of y' days' speech!. Yes, this was expected wanaenda kujivundika ndani kwenye moshi as they were advised.
 
Duuh

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu unataka kujiona na akili kuliko Mh.Rais. Yaani unakataa dawa zetu za kienyeji kusudi upate 10℅ ya madawa ya mabeberu. Umekwama aisee
 
Tungekua na Bunge lenye meno lingeilazimisha serikali kuchukua hatua. Bunge ni rubber stamp tu kwa sababu kwa nyakati hizi ilifaa wafanye vikao vya budget ya dharura.

Sent using Jamii Forums mobile app
Bunge letu ni imara sana..ata nchi zingine zinatuiga sisi.Tusitishane ndugu
 
Swali ambalo linahitajika na taarifa kadhaa Waziri wa afya aulizwe . Waginjwa wakitoka hospitali wakiwekwa karantini wanapata huduma gani, ikiwa corona Haina Dawa, Kuna nafasi ya kutosha ya kuhifadhi waginjwa kwa social distance,


Je vifaa tiba na nahitaji muhimu Kama barako , sanitizer, malazi Yana ubora kiasi gani na wanapatiwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Good!
 
Tatizo hapa ni jiwe.Hvi huyu rais hashauriki maana hajui aongee nini na wakati gani?Kutoroka kumehalalishwa na hotuba yake iliyokosa utulivu na utu yey analipuka tu.Siku zote tukiwa katika matatizo bora akae kimya maana ni confussor ,hajui kuiadress public ikiwa kwenye matatizo makubwa.Bila shaka takwimu zijazo zikawa fake ili kufurahisha nafsi yake,yey anatka wagonjwa waliipona wawe wengi
 

Sasa kama mtu amelazwa na amejitathmini akaona Haumwi tena na akagundua kua madaktari wanamwekea kauzibe asiondoke na yeye sio mfungwa ......
 
Wakuu naomba nielimishwe. Hawa walio amana si ndio wale waliopimwa na kuthibitishwa kuwa na tatizo au? Aliosema magu waachwe sio wale walio kule hosteli za magu wale ambao wamewekwa ila hawajapimwa[emoji56][emoji56][emoji56]??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu siku hizi una uwezo wa kubadilisha kichwa cha habari cha member bila shida badilisha tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuendelea kuwepo kwa JF ni jukumu letu sote. Si jukumu la Moderators pekee. Popote unapoona kuna tatizo linaloweza kuwatia msukosuko wasimamizi wa mtandao huu ni lazima(kama unaitakia mema JF) kuwasitua kwa kubonyeza kitufe cha report ama kuandika post kama nilivyofanya. Tuwe wamoja katika kuhakikisha JF inaendelea kuwepo bila matatizo. Karibu.
 
luck,
Kuna walikwepo pale wenye corona na ambao walikua wanasubiri majibu ila walikua na dalili zote za corona
 


Hizo ni figure za wiki kadhaa nyuma EU and US.

Kwa sababu awapimi na kutibu kila mtu confirmed cases (severe) ni wagonjwa wenye hali mbaya na ndio wanaopewa huduma hospitali. Hawa ndio wanatajwa kwenye takwimu wanazotoa kila siku za wagonjwa kwenye update zao.

Estimated cases ni (mild na moderate) wagonjwa ambao hawana vigezo vya kupokelewa hospitali kupunguza health services zisidiwe kwa ivyo wajitibu wenyewe majumbani na hawa wala hawapo kwenye takwimu zinazotolewa kila siku ndio tuelewe ukubwa wa tatizo lenyewe wakisema waangaike na kila mtu.

Hivi kama hao matajiri wameshindwa kutibu kila mtu mwenye Corona sisi tutaweza kweli kutaka kila mwenye dalili za Corona aende hospitali.

Maamuzi wanayochukua wenzetu sio kwa kupenda bali ni ya lazima; halafu eti kuna timu ziliundwa za kupambana na Corona.

The whole thing is shambolic na madhara yatazidi kuwa makubwa kama hawa jamaa awatabadilisha strategy.
 
Mgonjwa kuondoka haulizwi daktari au daktari muangalizi au nesi kwenye ward husika bali mlinzi wa geti la kuingilia au kutoka![emoji15][emoji15]

Tumefika hatua mbaya sasa!!
 
Siyo kama watu wahawati kukaa hospital sababu wanajiona hawaumwi sana...

Bila shaka huduma ni mbovu na huenda wagonjwa wapo wengi... Return Of Undertaker,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…