Ilikuwaje Nyerere akamshinda Sykes?

Ilikuwaje Nyerere akamshinda Sykes?

Unapotosha Sana. Unataka kuniambia waingereza ndio walimchagua Nyerere pale Anatoglou?. Kuhusu Wickens yule alikuwa Katibu Mukhtasi na Wala hakuwa na mamlaka yoyote. Kumbuka baada tu ya kupata uhuru wasomi walikuwa wachache hivyo tulikopa waingereza watusaidie.
Hilo la Arnatoglo wewe umelisoma wapi?

Hilo la Wicken mimi nakupa kitu kipya kabisa.

Ulishamuona katibu mukhtasi gani mwengine Tanzania hii au duniani akikutana na head of states, hususan Malkia?
 
Kulingana na mahojiano ya Tundu Lissu na mtangazaji wa ITV , Lissu alidai mara ya Mwisho CCM kufanya uchaguzi wa Mwenyekiti kwa ushindani ilikuwa mwaka 1954 kati ya Julius Nyerere na Abdulwahid Sykes. Ambapo Nyerere alimbwaga Abdulwahid Sykes. Uchaguzi huo ulifanyika kwenye ukumbi wa Anatoglou.

Swali la msingi ilikuwa ni kwamba ilikuwaje Nyerere amshinde Sykes ambaye alikuwa ni mtoto wa hapa Dar na baba yake alikuwa kiongozi wa TAA hapo kabla. Yani Nyerere kutoka Musoma aliwezaje kuwashawishi wajumbe wamchague yeye wamuache Sykes wa Dar.

Tusaidiane mbinu alizotumia Nyerere kushinda uchaguzi huo maana haikuwa rahisi.
Economist,
Nyerere hakufanya chochote.

Katika mazungumzo yaliyofanyika nyumbani kwa Hamza Mwapachu Nansio Ukerewe kati ya Mwapachu Abdul Sykes na Ali Mwinyi Tambwe walikubaliana kuwa Nyerere achaguliwe kuwa President na mwaka unaofuatia 1954 TANU iundwe kwa nia ya kudai uhuru na Julius Nyerere aongoze harakati hizo.

Kwa nini walikwenda kwa Hamza Mwapachu?

Sababu yeye ndiye alikuwa kiongozi wa harakati hizi za kuwaleta vijana wasomi ndani ya TAA kwa nia ya kukibadili chama kiwe chama cha siasa kamili wadai uhuru.

Hamza Mwapachu akamwambia Abdul Sykes amsaidie Nyerere achaguliwe ili mkakati huu wao ufanikiwe.

Aliporudi Dar es Salaam Abdul alifanya kama walivyokubaliana Nansio na Nyerere akapita uchaguzi ule lakini kwa kura chache sana.

Angalia video:


View: https://youtu.be/QKV-whFBnWY?si=ZtnHJjhUW1QvNWbB
 
Si wewe weka ukweli kuupanguwa upotoshaji wake. KInakushinda nini?

Umekazana "anapotosha" wakati hicho unachokiandika umekisoma kwake. Au unacho mbadala chenye ukweli?
Majanga.

Hapana Mimi sichukui chochote Kwa huyo Mzee. Jana historia imewekwa wazi.
 
Kulingana na mahojiano ya Tundu Lissu na mtangazaji wa ITV , Lissu alidai mara ya Mwisho CCM kufanya uchaguzi wa Mwenyekiti kwa ushindani ilikuwa mwaka 1954 kati ya Julius Nyerere na Abdulwahid Sykes. Ambapo Nyerere alimbwaga Abdulwahid Sykes. Uchaguzi huo ulifanyika kwenye ukumbi wa Anatoglou.

Swali la msingi ilikuwa ni kwamba ilikuwaje Nyerere amshinde Sykes ambaye alikuwa ni mtoto wa hapa Dar na baba yake alikuwa kiongozi wa TAA hapo kabla. Yani Nyerere kutoka Musoma aliwezaje kuwashawishi wajumbe wamchague yeye wamuache Sykes wa Dar.

Tusaidiane mbinu alizotumia Nyerere kushinda uchaguzi huo maana haikuwa rahisi.
Kama kasema hivyo, kadanganya, CCM haikuwepo wala haikujulikana kama itakuwepo mwaka huo.
 
Picha inaongea maneno 1,000 hiyo.

Ulishamuona katibu mukhtasi yupi duniani akakutana na malkia? Hata wa kwao Uingereza hutomuona. Protokali haziruhusu, itakuwa dharau kwa Malkia.

Lakini hapo? Unajionea mwenyewe.

Hiyo pîcha imepigwa Mwaka gàni?
Ulikuwa ni Muda WA Kazi?

Kuongea Jambo Kwa kujitungia NI uongo.
Uislam umekufundisha kujitungia mambo?
 
Na mimi nataka kujua , kwani huo uchaguzi ulikuwa na wa DSM tu? Au Tanganyika nzima?

Kama ni Dar pekee , basi ngoja wajuzi wa mambo waje,

Na kama ni Tanganyika yote , basi jibu ni kwamba , Nyerer alikuwa ni msomi na ana nguvu ya HOJA na USHAWISHI. Full stop
Mwaka 1954 ulitaka watu wabebe maboksi ya kura hadi Tandahimba mkuu?
Hapo Dar si kulikuwa na mchanganyiko wa wakazi kutoka sehemu mbalimbali, Nyerere mwenyewe si ni mzaliwa wa Mara.
 
Hilo la Arnatoglo wewe umelisoma wapi?

Hilo la Wicken mimi nakupa kitu kipya kabisa.

Ulishamuona katibu mukhtasi gani mwengine Tanzania hii au duniani akikutana na head of states, hususan Malkia?

Wewe unakataa kwamba Nyerere hakuchaguliwa , lakini unanilazimisha nikubali kwamba Secretary wake ndio alikuwa Rais wa Nchi. Unafurahisha Sana.
 
Picha inaongea maneno 1,000 hiyo.

Ulishamuona katibu mukhtasi yupi duniani akakutana na malkia? Hata wa kwao Uingereza hutomuona. Protokali haziruhusu, itakuwa dharau kwa Malkia.

Lakini hapo? Unajionea mwenyewe.

Hapo walikuwa kwenye tafrija wanaongelea. Sio kwamba malkia alifungwa official visit kuja kuonana na hiyo secretary wa Nyerere.
 
Back
Top Bottom