Ilikuwaje watu wakaamini kwamba Tanzania inaweza kuendelea bila kushirikiana na dunia?

Ilikuwaje watu wakaamini kwamba Tanzania inaweza kuendelea bila kushirikiana na dunia?

Labda nikuulize swali. Marekani enzi za Trump ilijitenga na Africa. Vipi enzi za Joe Biden, imejitenga na Africa? Kwasababu hawa marais hawajawahi kuzuru Africa. He, Mama yetu amejitenga na Asia, Bara Arabu, India na China kwasababu hajaenda huko? Ukinijibu scholarly nikaelewa, nitakuheshimu.
Mkuu hata usiponiheshimu mimi sina shida yoyote ile, kwasababu mimi napenda kusimamia ukweli siku zote.
Haya turudi kwa Raisi Donald Trump, hivi unafahamu ni madhara gani ya muda mrefu ambayo ameyaleta kwa Marekani na dunia nzima ??? Sasa iko hivi:

Sehemu kubwa za kimkakati kwa taifa la Marekani ni hizi zifuatazo:
-The Western Hemisphere,
-Europe,
-The Persian Gulf,
-The Middle-East,
-The Pacific,

Afrika haijawahi kuwa ni sehemu ya kimkakati ya nchi ya Marekani japo ina umuhimu sana kwake. Marekani iliyojengwa na Franklin Delano Roosevelt na Harry S Truman ni nchi ambayo imekuwa na nguvu duniani kwasababu ya ushawishi iliyofanikiwa kuujenga kwenye hayo maeneo.

Nakuachia maswali sasa:
  • Kwanini leo hii Ursula Von Deleyen anapendekeza EU wake na jeshi lao ilhali wako ndani ya NATO ???
  • Kwanini mataifa kama UCHINA na URUSI yanafikiri kuacha kutumia dola katika biashara yao ???
  • Kwanini siasa za Mashariki ya kati zimekuwa hatari sana kuliko kipindi chochote kile ???

Majibu yake sasa ndiyo, The Trump Effect......
 
Tanzania ilipoteza dira baada ya Nyerere kufariki.

Awamu ya tatu na ya nne Tanzania lost its soul ikabakiza historia ya marehemu.

2015 hivi aliyeruhusu Magufuli awe rais alikuwa anawaza nini ?
Nyerere ndie aliyeanza kupoteza dira kwa kuacha mfumo sahihi wa kuleta maendeleo ulioasisiwa na wakoloni.Angechukua mazuri ya wakoloni akaenda nayo
 
Nyerere ndie aliyeanza kupoteza dira kwa kuacha mfumo sahihi wa kuleta maendeleo ulioasisiwa na wakoloni.Angechukua mazuri ya wakoloni akaenda nayo
Nafikiri hoja yako iko kwenye mada tofauti kidogo.
 
Inasikitisha kuwa watu kama mtoa uzi huu wapo wengi tu!! Akili yao haifanyi kazi!! Wanaamini kuwa bila msaada wa wengine hatuwezi chochote! watu waliofilisika kichwani hadi leo wanaabudu ubeberu!!! Pole yao!
Umewaza kijinga msome tena jamaa utamulewa
 
Naamini Tanzania inaweza kuendelea bila kutegemea misaada bali ikabaki tu kuheshimiana na kushirikiana kwenye maendeleo...

Wakubwa wa dunia wanaamini kwenye umafia kwa kuendelea kufanya wengine masikini kwa kutumia baadhibya tools zai kila mahala..Wakubwa wadunia wakigundua una mtazamo tofauti wakuwatoa watu kwenye utumwa wa kiuchumi basi hutumia tools zao na vibaraka waliopandikizwa kila mahala kukumaliza..... WaAfrica tujaribu kuwa real na Uafrica wetu tusishupaze shingo na kubabaika sana na hawa pua ndefu....
 
Mkuu hata usiponiheshimu mimi sina shida yoyote ile, kwasababu mimi napenda kusimamia ukweli siku zote.
Haya turudi kwa Raisi Donald Trump, hivi unafahamu ni madhara gani ya muda mrefu ambayo ameyaleta kwa Marekani na dunia nzima ??? Sasa iko hivi:

Sehemu kubwa za kimkakati kwa taifa la Marekani ni hizi zifuatazo:
-The Western Hemisphere,
-Europe,
-The Persian Gulf,
-The Middle-East,
-The Pacific,

Afrika haijawahi kuwa ni sehemu ya kimkakati ya bara la Marekani japo ina umuhimu sana kwake. Marekani iliyojengwa na Franklin Delano Roosevelt na Harry S Truman ni nchi ambayo imekuwa na nguvu duniani kwasababu ya ushawishi iliyofanikiwa kuujenga kwenye hayo maeneo.

Nakuachia maswali sasa:
  • Kwanini leo hii Ursula Von Deleyen anapendekeza EU wake na jeshi lao ilhali wako ndani ya NATO ???
  • Kwanini mataifa kama UCHINA na URUSI yanafikiri kuacha kutumia dola katika biashara yao ???
  • Kwanini siasa za Mashariki ya kati zimekuwa hatari sana kuliko kipindi chochote kile ???

Majibu yake sasa ndiyo, The Trump Effect......
Dah! Wewe kweli "AKILI KUBWA"!
 
Malcom Lumumba naamini wewe ni mtaalamu mzuri wa diplomasia

Na mwana diplomasia kama wewe ni lazima utakua unawafahamu wajuvi wenzako wa diplomasia ndani ya nchi hii

Swali langu...

Tuambieni watanzania, utaalamu wenu wa diplomasia ulitusaidiaje kama nchi kujikomboa na janga la umasikini?(before&after magu, maana kwa mujibu wako huyu ni sufuri kwenye diplomacy)
 
Ndo maana kuna nchi zinaitwa first world na sisi ni third world, get that fact right kwanza kabla ya yote!
Nchi tajiri zina templates kadhaa katika profile zao, wakiamua wanajitegemea, wakiamua wanaweza kututegemea masikini kwa faida zao , wakiamua wanasaidia masikini..kuna wakati nchi hizo zinafanya mamboyote hayo kwa wakati mmoja
hadi leo dawa za kifua kikuu , hiv, zinakuja kama misaada kutoka kwa beberu, meantime copper ya zambia hadi leo hii masoko yake yapo huko huko kwa beberu.
Mama anazunguka huko kwa sababu anajua beberu haipukiki kwa namna yoyote.
She will loose some and win some games katika rounds hizo
Sasa wewe utakuwa first world lini? Au umelizika kuwa third world?
 
Naamini Tanzania inaweza kuendelea bila kutegemea misaada bali ikabaki tu kuheshimiana na kushirikiana kwenye maendeleo...

Wakubwa wa dunia wanaamini kwenye umafia kwa kuendelea kufanya wengine masikini kwa kutumia baadhibya tools zai kila mahala..Wakubwa wadunia wakigundua una mtazamo tofauti wakuwatoa watu kwenye utumwa wa kiuchumi basi hutumia tools zao na vibaraka waliopandikizwa kila mahala kukumaliza..... WaAfrica tujaribu kuwa real na Uafrica wetu tusishupaze shingo na kubabaika sana na hawa pua ndefu....
Kwa watawala gani hawa wanaobambikia kesi wenzao kukwepa mijadala
 
Nakubaliana kabisa na wewe, lazima tulinde rasilimali zetu kwa WIVU MKUBWA, lakini siyo kutumia ile njia ambayo kipenzi chenu alikuwa anaitumia. Amevuruga mambo na itifikati katika kiwango kikubwa sana,.....
Kuna njia ipi mbadala ambazo nchi za Afrika zitatumia kulinda masilahi yake? Huoni aliyoyapa Gadaffi? Labda utasaidie hata kidogo, nchi kama Tanzania itawezaje kulinda rasilimali zake kwa njia ya urafiki na mabeberu?
 
Malcom Lumumba naamini wewe ni mtaalamu mzuri wa diplomasia

Na mwana diplomasia kama wewe ni lazima utakua unawafahamu wajuvi wenzako wa diplomasia ndani ya nchi hii

Swali langu...

Tuambieni watanzania, utaalamu wenu wa diplomasia ulitusaidiaje kama nchi kujikomboa na janga la umasikini?(before&after magu, maana kwa mujibu wako huyu ni sufuri kwenye diplomacy)
Nchi hii watu wenye akili hawapewi nafasi sababu hawana muda wakusifu ujinga
 
Nchi hii watu wenye akili hawapewi nafasi sababu hawana muda wakusifu ujinga
Yawezekana hujamwelewa Lumumba, yeye amejikita zaidi katika awamu ya tano...

Ndio maana naamini kabla na baada ya awamu ya tano, nyinyi wataalamu mlipewa nafasi na makafanya kazi

Swali langu, kabla na baada ya Magufuli mmeisaidiaje Tanzania katika vipengele alivyotaja Malcom?

Asante.
 
Hakuna ambae hakutaka kushirikiana na nchi nyingine ila kushirikiana kwa kutunyonya hilo ndo tulikataa awamu ya tano na inatakiwa iwe hivo kwa nchi zote za Africa gasa kusini mwa jangwa la sahara! Ile mikata ya kusaini mi nakuletea kandamili ww nipe Tanzanite hatuitaki

Sent using Jamii Forums mobile app
Ukitaja kujua tuliongukia mikono mwa matapeli washamba, msikilize Kabudi akielezea mirabaha kwenye madini, sijui tutapata 50/ 50 laki wakati huo huo tuna shares 16%. Halafu huo utapeli hawataki mtu ahoji bali ni ww kusifia tu, eti nchi mkononi kwa mzalendo! Ila Mungu amtuepusha na yule kiongozi muovu, acheni Mungu aitwe Mungu.
 
The truth hurts, but it only hurts the guilty - Honorable Elijah Muhammad.

Hivi kuna mtu ambaye ameenda shule na kusoma vizuri, mfuatiliaji mzuri wa mambo ya siasa, uchumi na historia atataka kweli nitoe maelezo ya nini maana ya neno DIPLOMASIA ??? Hili mbona linafahamika "It's common and generic knowledge". Wewe na wachangiaji wengine, mmethibitisha kile nilichikisema kwamba watanzania wengi huwa tunafanya mambo aidha kwa maksudi, kimaslahi au tumekosa uelewa lakini bado tunajifanya wajuaji.

Ndugu Mpinzire ambaye kapingana na mimi kama wewe unavyofanya hapa, kasema Demokrasia na Diplomasia ni dhana za kimagharibi ambazo zinasababisha rasilimali zetu kuibwa. Marehemu naye aliwahi kusikika akiwa kwenye vikao vya ndani na wanasheria wa nchi akisema hivyo hivyo: Ninyi wanasheria mnakuwa waoga waoga na hayo maneno yenu mengi. Yeye alidhani Diplomasia na Sheria za kimataifa ni maneno, maneno tu.

Hivyo basi, kama hatufahamu maana nzima ya neno Diplomasia, tutaweza kung'amua kweli wapi Marehemu alipatia au alikosea katika kuongoza nchi ???
Je USA anaheshimu diplomasia yz kimataifa? Nieleze kuhusu ushiriki wake katika mahakama ya ICC.
 
The truth hurts, but it only hurts the guilty - Honorable Elijah Muhammad.

Hivi kuna mtu ambaye ameenda shule na kusoma vizuri, mfuatiliaji mzuri wa mambo ya siasa, uchumi na historia atataka kweli nitoe maelezo ya nini maana ya neno DIPLOMASIA ??? Hili mbona linafahamika "It's common and generic knowledge". Wewe na wachangiaji wengine, mmethibitisha kile nilichikisema kwamba watanzania wengi huwa tunafanya mambo aidha kwa maksudi, kimaslahi au tumekosa uelewa lakini bado tunajifanya wajuaji.

Ndugu Mpinzire ambaye kapingana na mimi kama wewe unavyofanya hapa, kasema Demokrasia na Diplomasia ni dhana za kimagharibi ambazo zinasababisha rasilimali zetu kuibwa. Marehemu naye aliwahi kusikika akiwa kwenye vikao vya ndani na wanasheria wa nchi akisema hivyo hivyo: Ninyi wanasheria mnakuwa waoga waoga na hayo maneno yenu mengi. Yeye alidhani Diplomasia na Sheria za kimataifa ni maneno, maneno tu.

Hivyo basi, kama hatufahamu maana nzima ya neno Diplomasia, tutaweza kung'amua kweli wapi Marehemu alipatia au alikosea katika kuongoza nchi ???
Umeongea vizuri umemalza ayo mengine ndio ayo ayo ambayo chanzo cha sahihi kuwa apa akili,sasa mtu anakuulza swali et tanzania masikini unazan kutakua na maelewano apo ,akili za binadam zimetofautiana sana ila naona kwa Africa utofaut wetu na mkubwa zaidi ikiwemo tz umo umo ndio tunapata viongozi matokeo yake ndio aya
 
Huwa nawaza sana tulifikaje hapa tulipo leo,

Hivi ilikuwaje taifa lenye wasomi wazuri kabisa likaamua kufanya maamuzi ya kipumbavu ambayo hata Waroma wa kale walioishi miaka 2000 iliyopita wasingeyafanya. Hivi katika maksudi kabisa, taasisi nyeti za Tanzania ziliamini kabisa kwamba wao wangeweza kuifanya Tanzania nchi tajiri bila kushirikiana na dunia : Hivi ilikuwaje kabisa wataalamu wetu ambao wameenda shule, wanafahamu mifumo ya dunia ya kiuchumi, kiulinzi na kisiasa na wako kule USALAMA, BENKI KUU na MAMBO YA NJE wakakubaliana na huu upumbavu na kuanza kuutekeleza kabisa?

Mpangilio wa dunia yetu ya sasa uliwekewa msingi mwaka 1814 kule Vienna baada ya miaka 25 ya vita za mfalme Napoleon Bonaparte. Mwanamfalme Von Matternich alifahamu kabisa ili dunia isirudie kuingia kwenye songombingo la vita au kadhia yoyote ile, basi ni lazima watengeneze mfumo ambao uko kama utandu wa bui-bui: Kwamba maamuzi ya nchi moja yakifanyika lazima yaathiri nchi zote, hivyo nchi lazima zikubaliane kwenye baadhi ya mambo muhimu yanayowagusa wote. Ndiyo nadharia ya MZANI WA NGUVU (Balance of Power) ikazaliwa.

Mfumo wa dunia ya yetu hii tunayoishi leo hii umejengwa na matukio yaliyotokea miaka ya 1913, 1914, 1918, 1920, 1927, 1928, 1933, 1935, 1939, 1941, 1944, 1945, 1947, 1948, 1971 na 2001 . Kiufupi mlolongo wa matukio haya yafuatayo ndiyo yanatoa mwelekeo mzima wa mwenendo wa dunia yetu ya leo : Nashauri tufanya utafiti wa ndani kuhusu hili.

Formation of the Federal Reserve, World War I, Versailles Peace Treaty, Formation of League of Nations, Signing of Kellog-Briand Pact, The Great Depression, The Monte-Video Convention, America's Abolition of Gold Standard, World War II, The Bretton Wood Agreement, Formation of UNO, Signing of the GATT, Publication of the Universal Declaration of Human Rights, Nixon's Abandonment of the Gold Standard and China's Admission to the WTO n.k.

Mtaalamu yoyote yule wa Uchumi, Diplomasia, Ulinzi na Sheria ni lazima afahamu fika kuhusu haya ninayoyasema hapa. Kwamba dunia nzima tuko ndani ya utandu moja wa bui-bui. Huwezi kufanya jambo lolote lile ukiwa nje ya hapo. Ndani ya huu utandu wa bui-bui kuna kila aina ya watu: Wema na wabaya, Huru na watumwa, Masikini na tajiri, Wenye matumaini na wasio na matumaini, Wababe na dhaifu na Waamini Mungu na Maadui wa Mungu.

Huu ndiyo mfumo wa dunia (The World Order), huwezi kufanya maajabu yoyote yale ukiwa nje: Hata mataifa makubwa yenye nguvu duniani yanaheshimu huu mfumo kwasababu yanafahamu siku mfumo huu unaharibika basi ndiyo utakuwa mwisho wao. Hivyo kuna baadhi ya sheria hata yenyewe yatazifuata tu kwasababu zina manufaa kwao. Mwandishi George Orwell kwenye The ANIMAL FARM aliwahi kusema "All animals are equal, but some are more equal than others" hivyo hata kama tunataka usawa kuna wale waliotutangulia watakuwa mbele yetu kwenye baadhi ya mambo tu.

Sasa kinachoumiza wasomi wa Tanzania wenye PhD za sheria, uchumi na diplomasia. Huku wengine wakiwa na shahada kwenye masomo ya ulinzi, usalama na sayansi za vita wakiwa na akili timamu kabisa, wakaamua kuwa wapumbavu. Wakatundika elimu zao nyuma ya milango na kuanza kutekeleza jambo ambalo hata watu wa kale walioishi miaka 2000 hawakuwahi kuliwaza. Tanzania ina matatizo mengi, lakini ilikuwa inarekebishika vizuri tu kwasababu waliofikisha nchi yetu hapa wanafahamika na tunakula na kunywa nao kila siku.

Kuanza kulaumu mabeberu peke yake haisaidii kwasababu kuna wenzetu ambao wamefanikiwa kutumia mifumo hii-hii ya mabeberu kuwashinda mabeberu kiuchumi, kiulinzi na kisiasa. Ukweli ni kwamba huu mfumo umejengwa na mabeberu lakini hata walioujenga hawaundeshi wanavyotaka wao. Mataifa ya Magharibi ndiyo waanzilishi wa World Trade Organization (WTO) lakini leo hii, WTO imemnufaisha Uchina kuliko tangu alivyojiunga nao mwaka 2001 na mpaka sasa wanajutia kumkaribisha.

Nchi kama Singapore, India, Korea-Kusini na Brazil wamewezaje kucheza vizuri kwenye huu mfumo wa mabeberu hadi kufikia kuwango cha kuwashinda mabeberu kwenye baadhi ya mambo ??? Inahitaji akili ya ziada kutoka kwa Mungu ili kuweza kucheza kwenye huu mfumo. Raisi Donald Trump alijaribu kuitoa Marekani kwenye huu mfumo wa Vienna, lakini pamoja na maguvu yote ya Marekani alifanikiwa ???

Lakini leo hii kuna watu wako ndani ya IDARA ZA USALAMA ZA TANZANIA waliamini kabisa kwamba Tanzania inaweza kujitenga na dunia bila kupata madhara. Yaani waliamini kabisa na wengine bado wanaamini kabisa. Kuna wengine bado wanaamini kwamba mfumo wa Kileninisti na Kimaksisti (Marxist-Leninism) unaweza kutumika kuikomboa Tanzania. Sawa, lakini hata walioutuletea huu mfumo Warusi na Wachina, wamebadilisha sana baadhi ya hizi falsafa.

Dunia ya nchi moja kutawala wengine (Uni-Polar World) au nchi mbili kuamulia dunia nini kifanyike (Bi-Polar World) unakufa taratibu, ndiyo maana Marekani na Urusi wanapata shida kukubaliana na huu ukweli. Wao kama mataifa hawaanguki na bado wana nguvu, ila tu ni kwamba mataifa yale madogo na masikini kama Vietnam, Poland, Mexico yamekuwa makubwa yenye uchumi unaokua kwa kasi sana.

Tanzania tuliachiwa mtaji mkubwa sana kidiplomasia, ambao ulitujengea SOFT-POWER na INFLUENCE ambayo ilifanikisha ulinzi na usalama wa Tanzania kikanda na kidunia kwa kiwango kikubwa sana. Tuliingia sehemu ambazo hata nchi kubwa hazikuweza kuingia, tulipata taarifa nyeti kabla hata baadhi ya mataifa makubwa hayajazipata, tulipewa heshima ya kipekee (Special Treatment) ambayo mataifa mengine yenye uchumi mkubwa kuliko sisi barani Afrika hayakupewa.

Tuliogelea bwawa moja na mababeru, wakomunisti, wajahidina na wazayuni lakini tulitoka salama, kesho tena tukarudi kuogelea. We were a Shrimp among Whales, lakini bado tuliheshimika mno. Lakini leo hii hebu angalia, ile nguvu yote ambayo Mzee Nyerere na Raisi Mkapa walitutengenezea, imemomonyoka kisa kikundi cha watu wachache wasiokuwa na uelewa mpana wa mahitaji ya nchi yetu na nafasi yetu hapa ulimwenguni.

Binafsi naamini ili tuweze kutoka hapa tulipo ni lazima NYUMBA ISAFISHWE aidha mbele ya majirani au kisiri. Mambo ya UHAINI, KUHODHI MADARAKA, KUPANGA KUUA MARAISI WASTAAFU,KUSHIRIKIANA NA MAADUI WA TAIFA na KUWINDANA KWA KUTUMIA MAKUNDI NDANI YA TASISI ZA KIUSALAMA (Cloack and Dagger Diplomacy) tulikuwa tunayasikia nchi jirani tu: Kwetu sisi yalikuwa ni MWIKO KABISA. Vitendo vya kihaini tulishaachana navyo awamu ya kwanza. Lakini leo kuna kakundi kalifikiri kabisa kangeweza kutupangia sisi Watanzania nani awe Mkuu wa nchi kweli?

Halafu bado haka kakundi kanalelewa tu: Kuhakikisha kwamba nchi haiwezi kurudi tena kule ilipotoka there's one place these people belong : The Cemetery, A Noose or A Bullet in the head!!! A prison term is not enough for these ruthless and deranged fanatics (This is legal, legitimate, justified and righteous).

Mara nyingine huwa naumia sana kuhusu Tanzania, natamani hata nisingekuwa nayafahamu haya yanayondelea.....

Watu hawakuwa wanaamini ule utapeli, bali ilikuwa ni shuruti. Na ilikuwa ukionyesha kwenda kinyume na ule utapeli unatekwa, kuuwawa au kubambikiwa kesi. Yaani tulipata kiongozi muovu, hisia zake akawa anatulazimisha tuziamini!
 
Back
Top Bottom