In Fact: Kwa Kupendekeza Tanganyika Tume ya Warioba Imependekeza Majimbo!

In Fact: Kwa Kupendekeza Tanganyika Tume ya Warioba Imependekeza Majimbo!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Tume ya Warioba imebeza na kupuuzia kurudisha mfumo wa Majimbo ikidai itajenga ukanda na ubaguzi. Halafu "magenius wetu" hawa wakaamua kupendekeza kuundwa kwa Serikali ya Tanganyika na ya Zanzibar in fact wameunda majimbo mawili - moja kubwa sana litaitwa Tanganyika na jingine litaitwa Zanzibar. Je hakutakuwa na hisia ya ukanda (Sisi Watanganyika, na sisi Wazanzibari) au ubaguzi "Hawa siyo wenzetu"?

Hivyo madai kuwa wamekataa majimbo kiuhalisia si ya kweli kwani kwa kuunda nchi inayoundwa na "States" mbili kimsingi wametengeneza kile walichokikataa. Tatizo ni kuwa - kama nilivyosema hapo juu - Jimbo moja litakuwa kubwa sana kuliko jingine na matokeo yake litaendelea kujiona kuwa lina nguvu zaidi. Ni sawasawa na kuwa na California na Texas halafu ukazipair na Rhode Island!

Vinginevyo tusipoangalia miaka hamsini ya majaribio ya serikali tatu tutajikuta tunavutwa kurudi kwenye serikali moja!

Njia pekee kama wameamua kuja na majimbo ni kuigawa Tanganyika katika majimbo mengine ili angalau kutengeneza equilibrium ya utawala vinginevyo kama nilivyosema kwenye ile posti nyingine Tanganyika itakuwa na nguvu mno kiasi kwamba hakutakuwa na jinsi isipokuwa Zanzibar kujiondoa.

Upande mwingine kuunda serikali moja ya kitaifa - na siyo tatu au mbili ndio njia pekee ya kuimarisha Muungano.
 
Kimsingi Wazanzibar wamesema na wanasema wao hawakushirikishwa na Rais wao wa kwanza namna ya kuingia katika muungano! Ndo maana walitaka kuwepo kura ya kuamua either waendelee kuwapo ndani ya muungano or hapana! kwa kuwa kura hiyo haikuwepo basi kiu hii nayo haijawatoka zaidi ya kuja na serikali tatu! maanake ni kuwa muungano huu unapendwa na wabara ila wao ni mpaka tungepata majibu ya kura ya kuutaka au kuukataa muungano. Warioba na tume yake wamefanya shortcut badala ya kuanza na kura kwa wazanzibar.
 
Sera ya majimbo hata kama imekuwa na maana nzuri ni ya CHADEMA, kama ilivyokuwa sera ya katiba mpya.Sababu ya Tume kukataa mfumo wa majimbo naamini ni kuogopa kuongeza umaarufu wa CHADEMA na sidhani kama kuna sababu nyingine zaidi.
 
Tume ya Warioba imebeza na kupuuzia kurudisha mfumo wa Majimbo ikidai itajenga ukanda na ubaguzi. Halafu "magenius wetu" hawa wakaamua kupendekeza kuundwa kwa Serikali ya Tanganyika na ya Zanzibar in fact wameunda majimbo mawili - moja kubwa sana litaitwa Tanganyika na jingine litaitwa Zanzibar. Je hakutakuwa na hisia ya ukanda (Sisi Watanganyika, na sisi Wazanzibari) au ubaguzi "Hawa siyo wenzetu"?

Mimi nafikiri Warioba na Tume yake wameamua" kummaliza" Mwanakijiji kwa shinikizo la damu na vidonda vya tumbo.

Tokea juzi Mzee wetu hali vizuri,hajisikii vizuri.
Mzee Mwanakijiji, nisngependa kukubaliana na Nonda juu ya observation yako.
Naelewa kuwa CHADEMA na CUF are in total dis array baada ya kutolewa rasimu ya Katiba mpya.
Hivyo basi sioni analogy ya Tanganyika na Zanzibar kuwa "majimbo" kwa maana ya majimbo ya uchaguzi kwa jinsi tunavyoyajua.
They are more than that, halafu Zanzibar ni nchi atii!!!!
 
Mzee Mwanakijiji, nisngependa kukubaliana na Nonda juu ya observation yako.
Naelewa kuwa CHADEMA na CUF are in total dis array baada ya kutolewa rasimu ya Katiba mpya.
Hivyo basi sioni analogy ya Tanganyika na Zanzibar kuwa "majimbo" kwa maana ya majimbo ya uchaguzi kwa jinsi tunavyoyajua.
They are more than that, halafu Zanzibar ni nchi atii!!!!

Unaundaje federal government kukiwa na nchi mbili? MMK yuko sahihi kabisa, nadhani hawakuelewa (Tume) tafsri (logical) ya kile wanacho propose, unless otherwise useme tunavunja muungano na kuwa na kitu kama EU. Ukishakuwa na federal government basi tena hakuna nchi mbili kuna kuwa na nchi mmoja na constituent states (majimbo). Anacho suggest Warioba ni kuwa na nchi moja!!!

Na kwa mtazamo wa tume. mbovu kabisa kwamba unaweza kuwa na majimbo mawili tuuuuu !!!! halafu ukaunda federal government, for sure kama nilivyosema hapo mwanzo, ni njia SAHIHI YA KUUVUNJA muuungano. Tunataka muungano au hatuutaki? Ndio swali la kujiuliza!!!!
 
tatizo suala la katiba mpya na hiyo sera ya utawala wa majimbo ni za wapinzani hususan cdm so hata kama ni hoja ya kujenga hawa ccm na serkal yake wanaingiza uvyama...hata hilo la katiba wamekubali tu kwa kuwa no way...
 
Nakubaliana na dotto kuwa wazanzibar ndo wanahisi inferior, so they should decide whether to continue or to come out of Muungano but they should consider other social-economical factors like power generation, food production etc
 
Excellent, Very true.
CCM, Warioba na tume yake wamejaribu kukwepa au kuchelewesha mambo tu ili kukwepa aibu, lakini ukweli unabaki pale pale tu, mfumo wa serikali za majimbo ni jambo la muhimu na lisiloweza kuepukika hata kidogo.

Hoja ya kudai ni gharama sana kuendesha mfumo wa majimbo ni dhaifu sana, kwani mpaka sasa si tume wala serikali iliyofanya utafiti wa kujua ni gharama kiasi gani kuendesha mfumo huo lakini pia wameshindwa hata kuanisha ni vipi mfumo huo utakuwa una gharama kubwa kulinganisha na mfumo wa sasa wenye DC, RC, wakurugenzi wa halmashauri nk.

Suala la kudai kuwa litaigawa nchi kikabila nalo si kweli kwa sababu:

1/Kila jimbo litakuwa na makabila wenyeji zaidi ya moja.

2/Karibu maeneo yote hapa Tanzania yanakaliwa na watu kutoka makabila mbalimbali tena kutoka maeneo ya mbali na uasilia wao kikabila.

3/Mfumo wa kisheria na kimaisha hapa Tanzania unaruhusu mtu kwenda kuishi mahali popote pale hapa Tanzania.

*Jambo baya kuliko lote na la kushangaza ni kuwa Serikali ya CCM inapinga mfumo wa serikali za kimajimbo kwa hoja kuwa utaigawa nchi kikabila au kikanda, lakini serikali hiyo hiyo kila mara imekuwa ikigawa mikoa, wilaya, kata, vijiji, majimbo nk kwa kufuata asili ya wenyeji wa maeneo husika kikabila na Geografia ya maeneo na hata kiukoo!!
 
Upande mwingine kuunda serikali moja ya kitaifa - na siyo tatu au mbili ndio njia pekee ya kuimarisha Muungano

Hili haitakuwa kuimarisha Muungano tu itakuwa hatua moja Mbele na kwamba Ndoto ya Shirikisho la Afrika Mashariki itakuwa imeshika kasi na pia tuaondokana na Mipaka ya kikoloni .
Manufaa nyingine ukabila mfano wa kitusi na kihutu na Jaluo na Kikuyu unaweza kupunguzwa kwa kugawa upya maeneo hayo kwa kumega viji sehemu na kuunganisha na vingine kutengeneza Jimbo(States).
 
Binafsi ni mfuasi wa Serikali yenye muundo wa majimbo kama ilivyo kwa baadhi ya nchi zilizoendelea, kitu pekee ambacho tulipaswa kuwa makini ni namna ya mgawanyo wa nguvu au madaraka kwa Serikali hizo ndogo ndogo
 
Hivi nisaidieni... halmashauri zetu na hiyo sera ya majimbo what is the differences and similarities...
 
kwa hatua waliofikia zanazibar kwa sasa hakuna jinsi zaidi ya kuirudisha Tanganyika.
unachosuggest Mzee Mwanakijiji ni kama vile zanzibar ivunjwevunjwe na kutoa majimbo kadhaa let say mawili halafu na bara(Tanganyika) litoe majimbo kadhaa.
uhalisia wa mambo ni kuwa zanzibar isingekubali kuuacha 'u-inchi' na kuukubali majimbo.
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mwanakijiji, nisngependa kukubaliana na Nonda juu ya observation yako.
Naelewa kuwa CHADEMA na CUF are in total dis array baada ya kutolewa rasimu ya Katiba mpya.
Hivyo basi sioni analogy ya Tanganyika na Zanzibar kuwa "majimbo" kwa maana ya majimbo ya uchaguzi kwa jinsi tunavyoyajua.
They are more than that, halafu Zanzibar ni nchi atii!!!!
masopakyindi,

..kwanini unafikiri CUF na CCM r in total disarray baada ya rasimu hii kutoka?

..kubwa lililofanyika ni tume kukubali mapendekezo ya CDM na CUF kuwepo kwa mfumo wa serikali 3.

..hata tume huru ya uchaguzi ilikuwa ni moja ya mapendekezo ya CDM.
 
Last edited by a moderator:
Sera ya majimbo hata kama imekuwa na maana nzuri ni ya CHADEMA, kama ilivyokuwa sera ya katiba mpya.Sababu ya Tume kukataa mfumo wa majimbo naamini ni kuogopa kuongeza umaarufu wa CHADEMA na sidhani kama kuna sababu nyingine zaidi.

Amini usiami dhambi ya kuvunjika kwa Muungano haitawachaa Wazee wote(Tume ya Katiba).Kuja kwa Serikali ya Tanganyika kinachoitwa Muungano kwisha habari yake kama walidhani wanawakomoa Chadema watakuwa wamekosea hatua na Mkakati na hii ni suala la muda.

[h=5]TUNA SABABU KUBWA ZA KUYATOA MAMBO (4) KATIKA MUUNGANO[/h]
[h=5]Ukiona CCM wamefurahi kuna jambo!!!![/h]Daftari alisema miongoni mwa hofu inayomkabili ni kuhusu hatima ya wafanyabiashara Wazanzibar waliowekeza na kuweka makazi ya kudumu upande wa Bara, ikiwa zitaundwa serikali za Zanzibar na Tanganyika (Bara).

"Wazanzibar wanafanya biashara sana Bara, wamejazana kila sehemu ya nchi, sasa tukifikia kila upande kuwa na serikali yake, maana yake itabidi warudi Zanzibar ili serikali ya Bara iwatambue na kuwahudumiwa raia wake," alisema.

Na mengineyo mengi na haya niya Zanzibar bado ya Tanganyika.
 
Hivi nisaidieni... halmashauri zetu na hiyo sera ya majimbo what is the differences and similarities...

Despite the fact kwamba CCM kwa muda sasa wamejigamba kutekeleza sera ya Decentralization by Devolution(D by D) kwa kupeleka madaraka kwenye halmshauri na kuakisi sera ya majimbo UKWELI ni kwamba halmashauri hizi zinafanya kazi chini ya directives za wizara ya tamisemi na hazina mamlaka ya kupanga na kuamua juu ya mgawanyo wa rasilimali katika ngazi husika.

The only big difference kati ya mfumo wa majimbo na halmashauri ni juu ya mamlaka ya umiliki na uendeshaji wa rasilimali, maamuzi na utoaji wa huduma ndani ya maeneo husika.There is a big delay katika utoaji wa huduma coz mambo mengi yako centralized na hata Wakurugenzi katika mamlaka hizi wako dependent kifikra.
 
Mwanakijiji, sio majimbo 2 bali wameunda majimbo 25 Tanganyika n 10 Zanzibar, sasa hayo mawili makubwa tuyatafutie majina yake .

SIjui walikuwa wakimaanisha nini kuunda majimbo 25 ya Tanganyika kama wanasema ni ukanda na ukabila , sasa hao wabunge wa Muungano si ndio maseneta hao au ikoje , maana bado kutakuwa na Bunge la Tanganyika na lile la Znz .
 
Hata mimi nafikiri ingekuwa busara sana iitishwe kura ya maoni kuhusu muungano kama pande zote mbili zinataka kuendelea na muungano au la kama tutakubali kuwepo kwa muungano basi mjadala uendelee kuhusu aina ya muungano,.sijui ni kwa nini watawala wetu wanashinikiza kuwepo kwa muungano bila kuuliza kama wenye nchi wanautaka au la!!
 
Excellent, Very true.

Suala la kudai kuwa litaigawa nchi kikabila nalo si kweli kwa sababu:

1/Kila jimbo litakuwa na makabila wenyeji zaidi ya moja.

2/Karibu maeneo yote hapa Tanzania yanakaliwa na watu kutoka makabila mbalimbali tena kutoka maeneo ya mbali na uasilia wao kikabila.

3/Mfumo wa kisheria na kimaisha hapa Tanzania unaruhusu mtu kwenda kuishi mahali popote pale hapa Tanzania.

*Jambo baya kuliko lote na la kushangaza ni kuwa Serikali ya CCM inapinga mfumo wa serikali za kimajimbo kwa hoja kuwa utaigawa nchi kikabila au kikanda, lakini serikali hiyo hiyo kila mara imekuwa ikigawa mikoa, wilaya, kata, vijiji, majimbo nk kwa kufuata asili ya wenyeji wa maeneo husika kikabila na Geografia ya maeneo na hata kiukoo!!

Baada ya ukabila na ukanda tume imeongeza ujinsia kwa hoja dhaifu ya jimbo kuwa Wabunge wawili (Kike na Kiume). Sera ya majimbo inautunganisha sio kutugawa kimakabila.
 
Back
Top Bottom