Ina maana gani kuota unatembea uchi mbele ya watu?

Ina maana gani kuota unatembea uchi mbele ya watu?

Sio kweli lazima yatimie, Mungu kamuonyesha kitu kinachoweza kutokea hapo baadaye hivyo anatakiwa achukue hatua hivi sasa ili jambo h
asante kuna mrejesho nimesha uweka kausome utagundua upo sahihi 100
 
kuna tukio la kukuvua nguo linakuja. Hiyo ni signal umepewa.
Aza kuomba maombi ya kukataa kabisa hilo tukio au chochote cha namna hiyo, na utaepushwa, ukipuuza inakula kwako.

Sadaka napokea kwa cash. 😋
 
Mimi niliota Kuna watu walikuwa wameniibia viatu nikawa nawasaka nilifika sehemu naulizia wanasema hawajawaona,then nikaamua kurudi home,nje walikuwa wamekaa wanaume kadhaa wanapiga story,Wala hawakuniangalia wakaendelea na story zao .Nikaingia uani,nikakuta binti mmoja anauza duka na baadhi ya ndugu,mama yangu alikuwa amesimama pembeni,(ni marehemu sasa)nikawa nalalamika kuhusu kuibiwa viatu vyangu,wale ndugu wakanishangaa wakanambia mbona uko uchi,nikastuka nikajifunika sehemu za Siri na viganja,mama akawaambia wanipe shuka,wakanipatia shuka jekundu nikajitanda,akachukua maji kwenye kikombe akamwaga kwenye maji yalokuwa yamesimama yakionekana na uchafu,alipomwagia Yale maji toka kwenye kikombe ule uchafu kwenye maji Yale yalotuama ukatoweka/kuyayuka,mie nikatazamana na yule dada alokuwa auza duka tukatabasamu,hapo ndo fahamu zikanijia,kuona mama yangu yupo hapo,nikataka kumsalimia na kumjulia hali then nikazinduka toka usingizini,toka sikuile nawaza tafrsir ya hii ndoto,ila Sina majibu,naomba nifafanulie mkuu Kama una weza.


Huyo dada muuza duka ulikuwa unamjua au laa??
 
Kwanza kabisa nilikuwa juu ya jengo la ghorofa 4 nikiwa uchi kama nilivozaliwa, sasa wakati nashuka zile ngazi zilikuwa ni zile zinakaaga nje kwa pembeni, cha ajabu hizo ngazi hazikuwa za kawaida yaani ni nyembamba mno kiasi ya kwamba ili uzishuke lazima uwe umegeuzia tumbo ukutani na ushikilie ukuta.

Kwakweli nilijaribu tu kutembea ngazi moja nikashindwa sababu ya kuangalia macho chini, ila cha ajabu nilijikuta namalizia ngazi ya mwisho chini kushuka na nikashuka nikiwa hivo hivo uchi na kuanza kutembea kwenda jengo lingine lililokuwa pembeni yake.

Watu walikuwa tu wengi ila nilijipa ujasiri nikachukua mashine yangu na kuibana kwenye mapaja na kuanza kutembea, nikaenda bafuni na kuoga ila sikumbuki kabisa kama niliweza kuvaa nguo.
Aiseeh
 
Kuna siri nyingi zinazokuhusu zitakuwa wazi.Na zitawekwa wazi na mtu mwenye hadhi.Ila utazikabili na ukweli wote utajulikana.
 
Viatu ni nini? Viatu vinaubeba mwili wako wote. Viatu ni heshima, ndio maana watu wanakuangalia kuanzia chini (viatu). Viatu vinaonyesha hali yako, kama ulitembea kwa miguu mtu akikutazama viatu atajua huyu kapuyanga. Viatu vinaonyesha hali yako ya kipato. Hivyo basi ukiota viatu unakuwa unaota hatma yako (your destiny).

Mtu akichukua nyayo za miguu yako, dhamira yake ni kuharibu hatma yako, au ubaadaye wako au destiny yako.

Kwa ndoto hii ndoto ni kwamba hatma yako imeibiwa. Pia umesema walikuwepo wanaume kadhaa, wala hawakukujali. Hii ina maana upande wa baba yako hawana msaada, wala hawajihusishi na matatizo yako, hivyo ukipatwa na jambo lolote watakaa kimya kama hawakuoni.

Mama ni Mungu mdogo. Mama akakusitiri aibu yako, akakuvalisha shuka jekundu. Msaada wako utatoka kwa Mungu tu, kuvalishwa vazi jekundu ni kupewa mamlaka makubwa, ndio maana rais anapita kwenye red carpet na rais ndio huvaa tai nyekundu na rais ndio husain kwa wino mwekundu.

Kwa hiyo kifupi ni kwamba usiposali kwa juhudi na kumwomba Mungu uwe na kesho nzuri, utaishia kuabika (kuwa uchi) ila ukisali Mungu atashuka kukusitiri na ubaadaye wako utakuwa mkuu.
Dah Asante mkuu,nimepita kwenye misukosuko kazini na kwenye maisha kwa ujumla kwa miaka mitatu mfululizo,yani ilikuwa ni bandika bandua ya matatizo,mwaka Jana mwezi wa tisa nikaanza maombi rasmi na kujiunga na kikundi Cha maombezi,nikajitenga na maovu mengi nilikokuwa nimelowea🙏mwaka huu mwezi January nikaanza kuona mabadiliko kiasi hata kazini na maisha kwa ujumla,namshukuru Mungu at least sasa Niko sawa kiasi flani,na maombi nazidisha kwakwel manake nimepitishwa kwenye tanuru la Moto humu duniani bila kosa lolote,kweli mwanadamu mwone kama alivyo tu.
 
Dah Asante mkuu,nimepita kwenye misukosuko kazini na kwenye maisha kwa ujumla kwa miaka mitatu mfululizo,yani ilikuwa ni bandika bandua ya matatizo,mwaka Jana mwezi wa tisa nikaanza maombi rasmi na kujiunga na kikundi Cha maombezi,nikajitenga na maovu mengi nilikokuwa nimelowea🙏mwaka huu mwezi January nikaanza kuona mabadiliko kiasi hata kazini na maisha kwa ujumla,namshukuru Mungu at least sasa Niko sawa kiasi flani,na maombi nazidisha kwakwel manake nimepitishwa kwenye tanuru la Moto humu duniani bila kosa lolote,kweli mwanadamu mwone kama alivyo tu.
Hakika wewe ni kipepeo wa chuma
 
Hilo ni onyo kuwa unaweza kuliwa masega mda wowote, acha mazoea na yule mke wa meneja. Mungu kakufungulia kupitia ndoto.

Jiepushe sana na wake za watu utaumbuka soon. Hizo ngazi ni za hotel na wembamba wake unaashiria kuwa hutaweza kuepuka njemba zitakazokupaka Ray's kwenye masaburi!
 
Mbona tukiota tunaokota hela usiku asubuh tukiamka hatuzioni na mpaka leo hatujawa matajiri uongo tu waafrika ndio unatusumbua
 
Back
Top Bottom