Inafikirisha sana kuona viatu vinakupwaya lakini unajipa matumaini ya kuendelea na safari ya uongozi kwa Watanzania

SSH ndio Raisi,hadi 2025,sijui kama atagombea au hapana,bali kwa sasa kazi ya kuongoza nchi tumewaachia akina mama.Miaka tuliongoza wanaume 27 ya Nyerere, 10 ya Mzee Ruksa,10 ya Mkapa, 10 ya Kikwete, 6 ya Magu jumla ni 63.
Na katikati 63 ya uongozi wa maraisi wanaume hatukuondoa umaskini.
 
Narudia tena mtumishi wa Mungu, marehemu ameshalala.

Anayefuatwa na maswali ya waliko kina Ben Azory Lijenje au waliowadhulumu kina Lissu Mawazo na wale wa kwenye viroba ni mtumishi wa Mungu yupi?



Imeandikwa - wapo miungu wengi tu!
 

Mmewaachia kina Mama au mwenyewe kawashurutisha na anakomaa kuachiwa hadi angalau 2030?

Kesha onja asali huyo!

Ikija 2030 akitaka tena zaidi nani wa kumzuia? Kwani jiwe alikuwa ataachia 2025?
 
Mpaka nimecheka eti, yaani maswali yako, naona tunakoelekea utaniuliza Kama Yesu alioga au hakuoga? Utaniuliza hizo nguo alizovaa zilikuwa zinafuliwa na Nan? Jaman walimu kumbe wanakaz sanaaaaaaa

Mkuu nashauri ukipata nafasi anzisha huzi seperate, kwenye jukwaa maalum. Hapa tuko ndan ya huzi wa mtu naona hatuko sahihi kuwa na hoja mbili tofauti.....Ila elewa maswali yako Yana majibu.

Na majibu hayo huwezi kuyajuwa mpaka uwe unaelewa theology vizuri, kwa mfano kuna lugha zimetumiwa kwenye biblia bila wewe kujua hz ni Figurative language, utapata shida.......

Swala la Yesu kupaa mbinguni na viatu na nguo, huwezi kuelewa kabisaa mpaka ujue kwenye theology kitu wanaita "the Incarnation of Jesus"

Ujuwe kwenye theology maana ya Perfectly divine and perfectly human. Vyote vinamuhusu Yesu, having two complete distinct nature's at once......

Anzisha huzi kwenye jukwaa husika wasomi wa Biblia watafungaka Kama wote...
Kwani Yesu alipopaa physically alipaa kutoka wapi na kuelekea wapi??, alikuwa kavaa nguo au hakuwa na nguo, hizo nguo bado anazo au hana??, huko alipokuwepo anakula nini??---- je maswali hayo yanahitaji Biblical interpretation ??

Kwani Yesu alipopaa physically alipaa kutoka wapi na kuelekea wapi??, alikuwa kavaa nguo au hakuwa na nguo, hizo nguo bado anazo au hana??, huko alipokuwepo anakula nini??---- je maswali hayo yanahitaji Biblical interpretation ??
 
Umeandika riwaya ndeefu afu ujinga tuu.Nyerere alivyokufa kila mtu alisema hivyo viatu vinapwaya hakuna wa kuziba pengo nk nk ..

Je uliona pengo halijazibika? Je baada ya kupwaya umeona viatu vimevulika?

Binafsi niwe tuu mkweli sijawahi mkubali Mwendazake hata siku moja,namaanisha na Wale wapigania uhuru wa zamani waliokuwa wanatumia mihemko na propaganda kuhadaa watu afu wakaishia kufa na kushindwa eg Edward Sokoine, Thomas Sankara,Patrice Lumumba, Robert Mugabe na wengine wa dizaini hiyo..

Mashujaa wa kweli waliotumia akili kama Nelson Mandela na J.K Nyerere walistahimili hadi kufariki vifo vya asili.

Huwezi tumia watu kama hao kuwa reference maana ni wanyapara waliofeli ila walifaulu kwenye propaganda zaidi.
 


Kwahiyo kwa mujibu wa Theolojia na sio kwa mujibu wa Biblia unataka kusema Yesu alipaa mbinguni figuratively na sio physically (in literally sense)??
 
Kwahiyo kwa mujibu wa Theolojia na sio kwa mujibu wa Biblia unataka kusema Yesu alipaa mbinguni figuratively na sio physically (in literally sense)??
Unaposema kwa mujibu wa theologia siyo kwa mujibu wa Biblia.. tayari hapa nimeisha ona kuna tatizo.... Pata kaawa kwanza mambo yakae vizur
 
Mama kama Ana nia dhabiti ya Kuendelea na Muhula wa 2025 - 2030 Basi huu ndio wakati wa Kuweka mizizi ya Loyalist wake ambao hata hawakuwepo Kwenye Regime ya JPM kitendo cha kuacha Cabinet ya Mawaziri vile vile ilikuwa sio Good move, Asafishe bado mapema haya Makapi mengi aliyonayo yatapiga Uturn Kubwa sana kuanzia 2024, Na siasa Za Nchi hii tunazijua haswa ifikapo kipindi Cha nani Awe Rais, Yote yote kwa Mama ni Rais Bora sana Sana Na Mimi Binafsi namtakia kila laheri katika Kutekeleza Majukumu ya Kujenga Taifa letu
 
Hata Mzee Mwinyi alisema hivyo hivyo kuwa yeye nikichuguu tu kwa Nyerere kumbuka hao ni watu pwan.Unaweza ona anakusifia kumbe anakunanga

Sent from my Infinix PR652B using JamiiForums mobile app
 
Kuanzia lini magufuli alikua kielelezo cha uongozi bora?

Imembidi azungumze hivo kutokana na kelele nyingi za kumfaninisha kwa heshima kuliko kusema wako tofauti au hakikubaliana na style take ya uongozi akaona atumie lugha ile.

Hata kama hatukubaliani nae sio kukosoa kihovyo hivi
 
Mleta mada mbali ya kuwa na chuki na Rais Samia, lakini pia uwezo wako wa kufikiri ni mdogo sana!

Nyie ndo mlimdanganya Rais Magufuli mpaka akadhani yeye ni Mungu,akajaa kiburi, akafokea viongozi wa dini hadi madhabauni!

Kwa hasira Mwenyezi Mungu akamchukua!
Sasa sijui huko aliko huyo "Mungu" wenu Magufuli ana hali gani!

Rais Magufuli pamoja na mazuri yake kiasi lakini alikuwa kiongozi mropokaji aliyefikia hadi kuomba kuwaongoza Malaika!!?

Julius Nyerere mtu aliyekuwa na akili kubwa kupata kutokea hapa Tanzania na mcha Mungu wa kweli,mnyenyekevu hakuwahi kufokea watu madhabauni!

Rejea mapokezi ya Kadinari Polcarp Pengo aliporudi toka Roma uone jinsi Mwalimu Julius Nyerere alivyoenda pale Airport kujipanga na raia wenzake kumpokea!

Huyo "Mungu" wenu Magufuli alitaka Maaskofu wamwabudu yeye! Askofu Niwemugizi wa Rulenge alimpinga wazi kabisa!

Rais Magufuli alikuwa Kiongozi Mkatili, mjivuni na mchoyo sana japo kuna mazuri pia ameliachia Taifa!

Hivyo nafasi aliyopata huyu Mama Samia ni mpango wa Mwenyezi Mungu!

Katika akili yake ya kibinadamu Magufuli amekufa bila kujua Mungu alikusudia Mama Samia ndo awe Rais wa Taifa letu.

Na Mwenyezi Mungu alivyo muweza na wa ajabu akamweka Magufuli kumwandaa huyu Mama Samia kuwa Rais bila yeye kujua!

Magufuli hakuwa mjuzi wa lugha yoyote ya kigeni hivyo hafla zote kubwa, mikutano mikubwa ya kimataifa yote alimtanguliza huyu Mama!

Mwenyezi Mungu kama alivyomuinua Yusufu mwana wa Yakobo ,akamuinua Samia binti wa Hassan!
Mwenyezi Mungu apewe sifa zake muda wote!

Kuhusu CCM, wewe na wenzako akina Polepole nimeshawambia hamkijui CCM, kama huyu Mama atagombea 2025, Katibu Mkuu atatengeneza fomu moja tu!

Kama mna akili badala ya kuanzisha SHULE ZA UONGOZI , anzisheni CHAMA chenu na siyo CCM!

Kwa ukatili aliokuwa nao Magufuli kuna mtu angethubutu kuua raia hapa Nchini bila yeye kujua! Haya mtuambie Magufuli aliongea nini kuhusu kifo cha aibu cha Leopold Lwajabe , mtumishi mwandamizi wa Serikali?!
Magufuli aliongea nini kupotea kwa Ben Saa nane, Azory Gwanda n.k?!

Wale wauaji wasiojulikana leo wameenda wapi?! Nao walikufa pamoja na Magufuli?!

Mwenyezi Mungu amemleta huyu Mama Samia kutibu maumivu ya Watanzania wengi wenye akili na si " Misukule" kama huyu mleta mada!

Na msijidanganye kwamba Rais Samia hachaguliki! Nani hadi leo anaamini Magufuli alipata kura asilimia 86% dhidi ya Tundu Lissu?!

Hivyo kaa ukijua Mama akigombea atashinda kwa KISHINDO, ya nini kuwaficha?!!

Rais Samia ni kama ile dawa Salimia ya kuchua maumivu!
Kwa uongozi wa chuki, njaa, mauaji na hofu chini ya Magufuli hatutajali hata kama Rais Samia atatuongoza kwa muda mrefu sana!

Hata tena Rais akitoka Zanzibar baada ya Rais Samia itakuwa vizuri sana, kwani hatutaki tena viongozi wabinafsi na Makatili hapa Tanzania.
 
Unaposema kwa mujibu wa theologia siyo kwa mujibu wa Biblia.. tayari hapa nimeisha ona kuna tatizo.... Pata kaawa kwanza mambo yakae vizur


Hivi; kila anayesoma Biblia ni lazima awe anajuaTheology kuhusu Biblia?? Kama ni kweli nani kasema hivyo??.

Hakuna tatizo mkuu, ila tatizo lipo kwako!!🤣
 
We mzee una akili ndogo kama kisoda viatu kutokumtosha siyo maana kwamba hana uwezo ni hivi mfano mdogo tu.Kama mwendazake alikuwa anavaa namba size 7 na yeye size namba 5 obviously hivyo viatu vya mwendazake haviwezi kumtosha hata kama ni vya kampuni moja.Kwa mfano huo mdogo nafikiri utakuwa umeelewa hiyo kauli ya viatu kumpwaya.
 
Sawa. Wasalimie Denmark.
 


Ni hivi, viatu vya Mwendazake vilikuwa vidogo na huyu miguu yake ni mikubwa ndio maana akasema havimtoshi kwakuwa ni vidogo Kwake, kama angesema viatu vya mwendazake ni VIKUBWA hapo ndio ingekuwa hoja.
 
Mkuu mbona unahangaika sana??? Hata huyo unayemsifia alipata kusema "alikuwa anabeep tu ikaita!!" akafikia kusema "...usiku kucha haulali ni kusoma mafaili tu!!" "kumbe kina mzee Mkapa na mzee Kikwete walikuwa na kazi ngumu hivi!!" je nini na yeye kilimkatisha tamaa kwenye urais wake??
Mwalimu alisema "Ikulu si mahali pa kukimbilia.." waliopakimbilia matokeo yameonekana na huyu aliyekuja kwa bahati anakiona kilichoko ndani ndio maana akavisema hivyo viatu...
Katiba mpya ndio ufumbuzi kuliko maneno mengi
 
Ili nisionekane nahangaika ulitaka nifanye niandike kitu gani? Hivi uliisikiliza hotuba ya huyo mgombea pekee mtarajiwa? Yeye anakiri hana uwezo wa kumfikia Marehemu Maguguli halafu wewe unasema Ni kauli tu ya kisiasa? Kwa hiyo, ili tuweze kumuelewa mama tuwe tunakuuliza wewe kwa kauli hii au ile alimaanisha nini?
 
Mwinyi alikuwa kichuguu na Nyerere mlima lakini Mwinyi alimaliza safari. Kazi iendelee.
 
Kwa hiyo,kwa kauli Yake kuwa Viatu vya Magufuli Ni vikubwa anamaanisha Magufuli alikuwa na uwezo Mdogo kulinganisha na yeye mama?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…