Inakuwaje mtu anatoa posa then anapangiwa mahali halafu anapotelea mitini? (Haoi)

Inakuwaje mtu anatoa posa then anapangiwa mahali halafu anapotelea mitini? (Haoi)

Ikiwezekana kipengele cha mahari kisiwepo kunusuru binti zao kuzurula mitaani, na kuzaa nje kama sio kuzalia nyumbani

Unapangiwa mahari ambayo ni ya kikatili, utadhani wewe ndio unae taka wakati ni matakwa ya wote yaani kijana na binti mwenyewe, ifike mahala mahari itakayo tajwa igawanywe kwa mbili!
 
Hii kauli huwa sitaki kabisa kuisikia.... Kuna binti mmoja nilionesha dalili za kumchumbia (umri atakuwa kagonga 28,,, maana ukimtizama waona kabisa gazeti jioni)
Ila kidume nikataka nijiweke hvyohvyo sababu vigezo vyangu baadhi anavyo halafu pia nikaona huyu hatutosumbuana kutokana na ukomavu wake...

Bwana bwana eeeh.... Si nikaamua kuweka mambo hadharani, na yeye akaanza nyodo (mara ninamtu wangu tena anadai kadum nae miaka 7,,, kimoyomoy nikasema Ni haki yake maana wanawake ndvyo walivyo)
Lakini cha ajabu akaendelea na sitaki na nataka .... Week iloisha nikamwambia dhamira yangu halafu mwisho nikamwambia ila kwasasa sitaki tena,,, pia nikamshauri siku nyingine akija mtu na mpango wa kuleta posa usimgusie swala la kunamtu kakukongoroa miaka 7, mwanaume atakimbia maana ataona wewe Ni mke wa mtu tayari!!!

Baada ya hayo nikamwambia mimi nimeshindwa aendelee na huyo anayejipanga kutafuta maisha mkoa jirani kwa mwaka wa7 Sasa, ili akiyapata ndo aje kujitambulisha kwao!!!
Nikainuka huyooo safari.... Huwezi amini baada ya hapo nikafuta namba nikajisemea mabinti wapo wengi tena wabichi kwanini nihangaike na limama... Toka hiyo week haishi kupiga simu, sms hazikauki na mimi nimekaza na msimamo wangu (yeye kauli aliyoishikilia Ni kwamba,,, sikumpenda Kama ningekuwa nimependa ningevumilia yote...... Pia Mimi namjibu kwa sauti ya upole kabisa
Kwamba "Mwanaume huwa haendeshwi na hisia... Sio lazima nikupende ili nikuoe, ukiwa na vigezo vya kuitwa mke hiyo inatosha... Kuhusu kukupenda ntajifunza kukupenda mbele kwa mbele🚶🚶
Ndo hvo mwanamke kafksha miaka karibia 30 lakini bado anadengua anapitwa na bahati ya kuolewa akiwa bado anamganda jamaa ambae hana hata mpango wa kuoa......pole sana mkuu utampata tu mwngne lakini umakini kiwe kipaumbele sana
 
Wanaume tuweni serious tusicheze na hisia za wachumba zetu, nashangaa kuona mtu anatoa mpaka posa anapangiwa mahali halafu anamkimbia bint hamuoi anaenda kuoa mwanamke mwingine, sijui tatizo huwa ni nini.
Kwani utaacha kizuri uchukue kibovu au utaacha kibovu uchukue kizuri?

Mbona wanawake wanawaacha wanaume mida mfupi kabla ya ndoa?
 
Kwani utaacha kizuri uchukue kibovu au utaacha kibovu uchukue kizuri?

Mbona wanawake wanawaacha wanaume mida mfupi kabla ya ndoa?
Ila kweli Kuna wanawake wanawakimbia waume zao hata mwaka haujaisha toka wafunge ndoa
 
Haikatazwi kubadilisha mawazo mkuu. Lakini kwann hadi afikie hatua kubwa kama hiyo afu aniache solemba[emoji848]. Aisee asinijaribu kabisa
Posa, mahari, uchumba, n.k, zote hizo ni taratibu za kusomana na kujirisha kwa unayetaka kuishi naye! Ukigudua mambo ndio sio, unasepa! Kwahiyo ni kawaida! Mfano, ugundue binti kwao ni wachawi, wana magonjwa ya ukichaa, wendawazimu, n.k. utakaaa? Unasepa mazima, ndukiii!
 
Wanaume tuweni serious tusicheze na hisia za wachumba zetu, nashangaa kuona mtu anatoa mpaka posa anapangiwa mahali halafu anamkimbia binti hamuoi anaenda kuoa mwanamke mwingine, sijui tatizo huwa ni nini.
Hilo suala nishawahi kulishuhudia zaidi ya mara mbili.

Lengo la kwanza huwa ni kukomoa na kudhalilisha, lengo la pili ni uhuni.

Nitaeleza visa hivi kifupi sana.

Kisa cha kwanza ni kama kukomoa: kuna msichana aliyejitunza vyema na akawa ni mfano kijijini kwao.

Kila kijana aliyemtaka kimapenzi alikataliwa na msimamo wa msichana ikawa kijana atakayemsikiliza ni yule mwenye malengo ya kuoa tu.

Mhuni mmoja akaigiza kumchumbia, taratibu za washenga na posa akatoa, ila kutangaza ndoa akawa anatoa visingizio kuvuta muda.

Kwa kuwa ameaminiwa na mchumba pamoja na wazazi, akawa anamchukua mchumba wake huyo mbele ya wazazi bila ya wasi wasi kwenda naye mjini kumnunulia vitu na huko msichana akalaghaiwa, jamaa akawa "anajisevia".

Na mwisho wa siku jamaa kaingia mitini huku lengo lake kalitimiza kauli mbiu yake ikiwa ni: ..."kwani pesa kitu gani kupoteza?"

Kisa cha pili mtiririko wa kuanzia unafanana na kisa cha kwanza, kuchumbia na kisha kufanya mapenzi kabla ya ndoa.

Sasa huyu alikuwa ni kivuruge hasa, ilikuwa afunge ndoa kanisani.

Aliiwatia hasara mpaka wazazi wake kwa kuandaa sherehe ya gharama kubwa na kisha akaingia mitini dakika za majeruhi, bibi harusi na wapambe kutelekezwa na shela lake kanisani bwana harusi asijitokeze na ikaishia hivyo.

Nilichojifunza kwa matukio haya mawili ni kwamba wasichana wenyewe kushindwa kusimamia misimamo yao mpaka mwisho.

Kuwaamini wachumba wao kupita kiasi, hasa mvulana akishamchumbia na kutoa mahari, huaminiwa sana kuwa hatua hiyo huwa si rahisi kubadili mawazo.

Nikija kwa upande wa wazazi: ni kusimamia kwa ufasaha maadili ya dini, mila, desturi na tamaduni juu ya malez bora ya mtoto wa kike.

Mtoto wa kike iwe ni mwiko "kusogeleana" na mchumba wake wa kiume mpaka siku watapofunga ndoa, ieleweke wazi kuwa thamani ya mwanamke hubakia ilivyo asipoguswa tu.

Na pressure ya muoaji ya "kubeba mzigo" hupanda akinyimwa na kuishia kula kwa macho, lakini akipewa ile muhu ya kuchakarika hushuka na mwisho wa siku ndiyo kuaibishana.

Watu hawajali thamani ya pesa zao za mahari na gharama zingine wanazozipata katika prosses hiyo.

Msilaghaiwe na utoaji wa mahari mkaanza kumruhusu mtoto wenu kutoka na mchumbake kabla ya ndoa, mambo yakibadilika aibu ni juu yenu wazazi.
 
Hilo suala nishawahi kulishuhudia zaidi ya mara mbili.

Lengo la kwanza huwa ni kukomoa na kudhalilisha, lengo la pili ni uhuni.

Nitaeleza visa hivi kifupi sana.

Kisa cha kwanza ni kama kukomoa: kuna msichana aliyejitunza vyema na akawa ni mfano kijijini kwao.

Kila kijana aliyemtaka kimapenzi alikataliwa na msimamo wa msichana ikawa kijana atakayemsikiliza ni yule mwenye malengo ya kuoa tu.

Mhuni mmoja akaigiza kumchumbia, taratibu za washenga na posa akatoa, ila kutangaza ndoa akawa anatoa visingizio kuvuta muda.

Kwa kuwa ameaminiwa na mchumba pamoja na wazazi, akawa anamchukua mchumba wake huyo mbele ya wazazi bila ya wasi wasi kwenda naye mjini kumnunulia vitu na huko msichana akalaghaiwa, jamaa akawa "anajisevia".

Na mwisho wa siku jamaa kaingia mitini huku lengo lake kalitimiza kauli mbiu yake ikiwa ni: ..."kwani pesa kitu gani?"

Kisa cha pili mtiririko wa kuanzia unafanana na kisa cha kwanza, kuchumbia na kisha kufanya mapenzi kabla ya ndoa.

Sasa huyu alikuwa ni kivuruge hasa, ilikuwa afunge ndoa kanisani.

Aliiwatia hasara mpaka wazazi wake kwa kuandaa sherehe ya gharama kubwa na kisha akaingia mitini dakika za majeruhi, bibi harusi na wapambe kutelekezwa na shela lake kanisani bwana harusi asijitokeze na ikaishia hivyo.

Nilichojifunza kwa matukio haya mawili ni kwamba wasichana wenyewe kushindwa kusimamia misimamo yao mpaka mwisho.

Kuwaamini wachumba wao kupita kiasi, hasa mvulana akishamchumbia na kutoa mahari, huaminiwa sana kuwa hatua hiyo huwa si rahisi kubadili mawazo.

Nikija kwa upande wa wazazi: ni kusimamia kwa ufasaha maadili ya dini, mila, desturi na tamaduni juu ya malez bora ya mtoto wa kike.

Mtoto wa kike iwe ni mwiko "kusogeleana" na mchumba wake wa kiume mpaka siku watapofunga ndoa, ieleweke wazi kuwa thamani ya mwanamke hubakia ilivyo asipoguswa tu.

Na pressure ya muoaji ya "kubeba mzigo" hupanda akinyimwa na kuishia kula kwa macho, lakini akipewa ile muhu ya kuchakarika hushuka na mwisho wa siku ndiyo kuaibishana, watu hawajali thamani ya pesa za mahari na gharama zingine wanazozipata katika prosses hiyo.

Msilaghaiwe na utoaji wa mahari mkaanza kumruhusu mtoto wenu kutoka na mchumbake, mambo yakibadilika aibu ni juu yenu wazazi.
Duh! kumkomoa mtu ni dhambi kubwa Sana ,
 
Huwa tunaoa familia hatuoi binti yao, sasa kama mzani umegoma kubalance kwenye tabia za familia ya binti hakika tunatimka mbio za Hussein Bolt, ile swaaaaa!!!! kama upepo 😂 😂

Sasa familia inaniuliza nafanya kazi gani na wapi, ni swali muhimu ila wamuulize binti yao. Na yeye kama hajui wamuulize tu anayaonaje maisha ya mwenza mume mtarajiwa, je ataweza kuhudumia familia watakayoianzisha?. Wakipewa majibu wamshauri binti yao sasa.

Siku wakionaan na muoaji ijadiliwe mahari na mambo ya jumla jumla tu lakini waangalie uongeaji wa wote waliokuja kuanzia muoaji hadi mshenga, amini tabia ya mshenga na muoaji huwa hazipishani sana, sasa mshenga kwakuwa hayupo kwenye nafasi ya kupoteza atawaonesha wao ni wakina nani hasa na wamekuja kufanya nini hapo kwao.
Eti tabia za mshenga na muoaji huwa hazipishani sana🤣🤣
 
Back
Top Bottom