Inakuwaje sarafu za milioni 200 zinafichwa mamlaka zisishtuke mapema?

Inakuwaje sarafu za milioni 200 zinafichwa mamlaka zisishtuke mapema?

Mkuu tatizo hapo sio kukusanya izo coins. Tatizo ni kuwa wanakwepa kodi hawa jamaa. Unakuta mtu amechukua kibali cha kuchezesha kmali cha mashine 100 tu. Kumbe amesambaza mashine 200. Na ukiwa na mashine nyingi ni lazima uwe na coins nying za kusambaza.

Kitu kingine kunakiwango maalumu cha pesa mtu anatakiwa awe nacho kama cash. Kikizidi ni makosa.

Sasa uyo mchina kosa linaweza kuwa ni kuwa na kiwango kikubwa cha pesa in cash.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mil 200 Ni pesa nyingi za kukamatwa?
 
Hayo 9 wangekuja huku Temeke Dar .
Kwa siku mchina anaondoka na mamilioni ya bodaboda, wachoma chips, na vijana waokota makopo .

Bila shaka Wachina wanatumia uchawi, maana si kwa kula kule. Wanacheza vijana 30 anabahatika mmoja kula elfu 10 huku 29 wote wameliwa jumla ya laki na ushehe.
Kila kona huku wameweka dubwi
 
Hayo 9 wangekuja huku Temeke Dar .
Kwa siku mchina anaondoka na mamilioni ya bodaboda, wachoma chips, na vijana waokota makopo .
Bila shaka Wachina wanatumia uchawi, maana si kwa kula kule. Wanacheza vijana 30 anabahatika mmoja kula elfu 10 huku 29 wote wameliwa jumla ya laki na ushehe.
Kila kona huku wameweka dubwi
Tatizo Ni Nini? Hao vijana wanashikiwa visit kucheza?
 
Kwanza Bodi ya bahati nasibu sidhani kama wana wataalamu wa kutosha wa kuchezea hizi mashine za kichina kujua ni fake au la.

Mchina mjanja ana kirimoti kidogo anaseti anawapiga weeeee then anawaachia kidogo.

Kuna majamaa wanajua kuzcheza na zile machines, Wakija wanamzuga mwagalizi huku wanayachokonoa. Then kila wakiweza mia mbili zinamiminika pesa.

Sijui wako wapi wale jamaa, mchina hawapendi.
 
Sioni tatizo hapo kwani wabongo wenyewe ndo wanawapelekea hizo sarafu kwenye zile mashine za bonanza sasa shida iko wapi??

Wao wameona fursa ya wabongo kupenda kamari na fedha za mdebwedo na wakaamua kutumia fursa. Hizo sarafu ndo commodity kwenye biashara yao,kuwakamata wakati ww ndo umewapa leseni ya biashara sio busara. Mara mia wawafungie tu hizo mashine zao za bonanza
Mkuu, una elimu gani, tuanzie hapa kwanza..

1. Unafaham madhara ya kiuchumi kwa baadhi ya watu ku hold pesa bila kuziingiza kwenye mzunguko!??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hizo sarafu ndio kama commodity zao, ni kama wewe uwe na duka na bidhaa za kuuza. Kwao bidhaa ni hizo sarafu. Na sehemu kama Morogoro wanakua wameweka vituo vingi sana hadi vijijini na huwa hawaajiri mtu mweusi ashike hela zao so utakuta sarafu zote kwenye hivyo vituo zinakusanywa sehemu moja na zitasambazwa tena baadae zikihitajika.

Naamini wakiwakagua hata mikoa mingine kama Dar na mwanza watakuza hata zaidi ya mil 400 za sarafu
Leo niko na wewe...

Kwa sheria za bank kwa nchi yetu, Je, unajua ni chombo gani chenye mamlaka ya kutoa change!???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tukitaka ukweli na haki hizo sarafu hazikufichwa.

Hao wachina wana leseni na wanalipa kodi kwa ajili ya biashara yao ya kamali ambayo ipo mkoa mzima wa Morogoro kuanzia Morogoro mjini hadi wilayani hadi Dodoma

Mashine zao za kamali haziingii noti zinaingia sarafu sasa mlitaka wahifadhi noti kwa ajili ya kusupply mashine zao?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hiyo biashara ni halali...Mimi nashangaa kuweka ndani Kiasi kikubwa cha Fedha ...Mimi kwa uelewa wangu Fedha ni Mali ya Serikali, sisi tunamiliki thamani ya fedha,!

Ndio maana ukifanya kazi unalipwa kwa kuthaminisha na Fedha... Sasa ukizitoa kwenye mzunguko huoni kuwa Ni hatari!
Hata ule mchezo wa Dar kuuziana change' Nafikiri kiuchumi SIO SAWA!
Wanamashine zaidi ya 500 ulitaka wasupply noti kwenye hizo mashine

je hawalipi kodi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
TUKITAKA UKWELI NA HAKI HIZO SARAFU HAZIKUFICHWA
HAO WACHINA WANA LESENI NA WANALIPA KODI KWA AJILI YA BIASHARA YAO YA KAMALI AMBAYO IPO MKOA MZIMA WA MOROGORO KUANZIA MOROGORO MJINI HADI WILAYANI HADI DODOMA

MASHINE ZAO ZA KAMALI HAZIINGII NOTI ZINAINGIA SARAFU SASA MLITAKA WAHIFADHI NOTI KWA AJILI YA KUSUPPLY MASHINE ZAO?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu, unadhani wametumia mda gani kukusanya hizo pesa!??

Bank ina kazi gani mkuu!??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nadhani huo ni uonevu tu wa mamlaka.

Hao wachina wana mashone zao za kuchezesha kamari na wameruhusiwa na mamlaka.
Na wanalipa kodi.

Sasa Mamlaka ilipowaruhusu waweke makorokoro mitaani walijua kuwa yanaweka ili yagawe maziwa?
Bro haya mambo yapo Tz tu..sasa unampa mtu kibali afanye biashara na mtaji wake ni coins alafu zikiwa nyingi unamkamta ili iweje wanataka wachezeshe hizo kamali kwa kutumia uterine fibroids au...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu, una elimu gani, tuanzie hapa kwanza..

1. Unafaham madhara ya kiuchumi kwa baadhi ya watu ku hold pesa bila kuziingiza kwenye mzunguko!??

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwani ni lazma ziwe kwenye mzunguko wakat hyo ndo flowing capital kulingana na mashine zao???huwezi kuweka justification kwamba wazipeleke kwenye mzunguko wakat ndo capital alafu hiyo biashara ita run na nini mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naam, kama hawakuiba hakuna shida. Mbona watu wameweka dola za US hapa lakini Marekani hailalamiki?
Ninavyoelewa Mimi hayo makokoro yanautumia coins 200 na 500. Na mashine moja inaweza kuweka mpaka coin 1000.

Sasa kila siku lazima wapitie mashine zote kuongeza pesa ama kuchukua pesa.

Sasa lazima wawe na float (working capital).

Ukiangalia 200million gawanya kwa Mia mbili unapata coin 1,000,000 za Tsh 200 ama 500,000 za Tsh500.

Kama Wana mashine 200 maana yake kila mashine imekuwa allocated 5000 coins za Tsh 200 au 2500 za Tsh 500.

Hivyo kuwa na hizo coin Wala sioni Kama ni shida.

Mbona Kuna watu ulienda nyumbani kwao watakuwa na zaidi ya billion 3 ndani kwao.

Tujipange na mambo ya maana.

Covid inaua, stay safe stay home
 
Mimi nachezesha game ps2, 3 na 4 mara nyingi hujikuta nina hadi laki 1 ya sarafu za shilingi hamsini, mia, mia mbili na mia tano.

Je na mimi siku yangu yaja?
 
Sio kwamba wanazificha, hao wanafanya biashara ya kamari ambazo zinatumia coins(200) ili kuchezesha ambapo utakuta mashine moja lazima iwe na mtaji wa hizo coins wa laki mbili ndani yake, ili mtu akila ziweze kutoka kama zawadi ya ushindi huo.

Sasa kama mkoa mzima wa Morogoro wana mashine unategemea nini, lazima wawe na pesa hizo, za kwenda kuongeza pindi mashine inapoishiwa/pungukiwa mtaji, na sio kama ni kweli kuwa hizo 200 lazima ziwe zimekusanywa kutoka Morogoro tu, inawezekana hata kwenye mabank, dar pia wanachukua.

Kosa ambalo serikali ilifanya ni kuruhusu pesa za nchi hasa hizo coins(200/100) kutumika kwenye mashine za michezo ya kubahatisha, na pool table,badala ya TOKEN!! leo ndio wanakuja kusema kuwa ni kosa kutumia pesa badala ya token, baada ya kuwakamata hao wachina!!! Wakati ni miaka mingi tu coins ndio zinatumika!!!!
 
Back
Top Bottom