INASIKITISHA: Makaburi Kinondoni yanavunjwa makusudi ili ipatikane nafasi ya kuzikia

Buji makaburi ya hapo hayamalizi miaka kumi hasa yale ambayo ndugu zao hawayatembelei mara kwa mara... Linapandiwa dau watu wanaenda kujenga heshima bara

makazi ya watu yana jahaga lakini makaburi sijaona kujahaga
 
Nadhani marehemu wanapokuwa wanajigeuza wanagongagonga kuta za nyumba zao ndio maana zinabomoka
 
Kuna siku nilienda msibani, sa wakati wa kuzika tukiwa makaburini sheikh akatoa speech

Akiwataka wanaozika ndugu zao kwenye makaburi ya eneo hilo waache mara moja tabia ya kujenga makaburi kwa cement, concrete au tiles

Maana eneo hilo limekwisha jaa hivyo kufanya hivyo unakua unazuia wengine washindwe kuzika ndugu zao, utaratibu uliopendekezwa ni kuzika bila kujenga ili siku za mbeleni mwingine apate nafasi ya kuzika juu yako
 
Kudadadeki. Serikali inasemaje?
 
Kama mnapesa hivyo kwanini hamkusafirisha kijijini kwenu?
 

Kwahiyo hata huyu ulitaka asijengewe kisa ataabudiwa?
 
Mimi ninaomba nizikwe kwetu Mtae
Aisee. Unaweza kukuta wewe Ni Dada yangu.
Halafu kule kwetu udongo ni wa baridi, sio huku Kinondoni joto, changudoa wanafanya uppuuzi juu ya kaburi lako, vibaka wanavutia bangi juu halafu wahuni wanasambaratisha kaburi taratibu ili wamuuzie mtu aliyekua hatambelei kwao. Lkn pia Kinondoni unazikwa na watu usio na undugu nao. Kushoto mmakonde, kulia msukuma, kichwani Mluguru na miguuni mfipa. Mluguru akianza kuongea Hana kituo. Aka mie kwetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…