Inaumiza sana mtu ana masters degree ila hawezi hata kujilipia kodi ya chumba kimoja. Elimu ya juu imesababisha wategemezi wengi wenye umri mkubwa

Inaumiza sana mtu ana masters degree ila hawezi hata kujilipia kodi ya chumba kimoja. Elimu ya juu imesababisha wategemezi wengi wenye umri mkubwa

Education system inatugharimu San nchi nyingi za Africa,,
Elimu imekaa katika mifumo ya kuajiriwa siyo kujiajiri
Kwani huko ulaya mifumo yao ya elimu ndio imekaa kimfumo wa kujiajiri..?
Cha msingi serikali ifanye wajibu wake wa kuhakikisha kunakuwa na fursa nyingi za ajira na kujiajiri kwa vijana na sio siasa au propaganda kila sehemu.

Hawa European na USA au China na japan sio wajinga wanakuwa na data za kila mwezi kuhusu hali ya ajira ya wananchi wao..

Haiwezekani wanatoka vijana wenzetu hapa hawana ajira wanafika ulaya na america wanapata ajira on spot na wanaanza kuwekeza huku kwa nn sisi tunashindwa tunashida mahali ise.
 
INAUMIZA SANA KWA KWELI UNAPOONA WASOMI WAZURI ILA WANA HALI NGUMU KIUCHUMI.
Naomba posts kama hizi kabla hujafika mbali muwe mnatuambia na nyie mlianzaje maisha ,,, mfano elimu ya awali Diploma
Kabla ya kuajiliwa :niliuza sana maji na makopo kiasi sikutamani kuajiliwa ,alafu ndio unaingia kuwalaumu wenzio Sasa,


Japo mshangao wako una tija,ila ni vizuri kujitathimini wewe, elimu yetu na kinachotokea kwa hao vijana, unaweza mlaumu mtu kumbe tatizo ni elimu tunayopewa
 
Kwani huko ulaya mifumo yao ya elimu ndio imekaa kimfumo wa kujiajiri..?
Cha msingi serikali ifanye wajibu wake wa kuhakikisha kunakuwa na fursa nyingi za ajira na kujiajiri kwa vijana na sio siasa au propaganda kila sehemu.

Hawa European na USA au China na japan sio wajinga wanakuwa na data za kila mwezi kuhusu hali ya ajira ya wananchi wao..

Haiwezekani wanatoka vijana wenzetu hapa hawana ajira wanafika ulaya na america wanapata ajira on spot na wanaanza kuwekeza huku kwa nn sisi tunashindwa tunashida mahali ise.
Ukiwaambia ,wanakwambia graduates wavivu .


Stupid
 
Kwahio wote wakasome marketing n.k. Madktari, Ma-engineer n.k. vyote havina maana
Moja:
kama ndivyo unavyosema kwanini haya masomo mengine yasifutwe ?

Mbili:
Enterpreneurship sio kwenda shule na kusoma theory ni attitude ya mtu na discipline...

Tatu: Mmekuwa brainwashed kiasi kwamba mnafanya kazi ya watunga Sera iwe rahisi kama ya mganga wa kienyeji - Ukishindwa ni makosa yako na haujafuata masharti sio kwamba makosa ni yao....

Nne:
 
Kwa ss ivi mtoto wako n kumsimamia vitu vya kusoma ili akitoka huko unampa sapoti kwa kile alichosomea kama kasomea ufugaji unamuwezesha huko kama n uvuvi unamuwezesha huko kama n veta unamuwezesha huko kama pharmacy unamuwezesha huko sio unamsomesha mtoto mavitu hayana connection yyte kwenye jamii na ww huna connection yyte mfano unamsomesha HR ww huna hata kampuni halaf badae unamsapoti vp huyo kijana wako
 
INAUMIZA SANA KWA KWELI UNAPOONA WASOMI WAZURI ILA WANA HALI NGUMU KIUCHUMI.

Wazazi tuchukue tahadhari, Tusomeshe watoto sambamba na kuwaandaa waweze kujiajiri ama kufanya biashara, degree/masters zinawaaibisha watu mitaani​


Wazazi tunapaswa tubadilike sana kwenye kuwekeza kwa ajili ya watoto wetu. tuwekeze kwenye mali zaidi kuliko kuwalipia ada mamilioni mwisho wa siku wanarudi nyumbani wakiwa hawawezi hata kujitegemea
Mimi nilishaacha huu ujinga.

Kama una uwezo sawa ila kama hela ni za kuunga unga fanya yanayowezekana.
Badala ya kulipa Milioni 40 kwa ajili ya form four tu bora anunua mashamba awezekeze hata kilimo cha Nguruwe.

Tuna tatizo la kuiga mifumo ya maisha.

Mwenzako ni Afisa kwenye taasisi ya serikali ana michongo ya pesa kibao na ndio wamejaa Huko Feza schools,marian na st thomas.

Wewe unauza Duka la Mchaga unakazana fuvu
 
Hayo ndo mapambano yenyewe mkuu. Usishangae hadi huku vijijini kwetu sasa vijana wasomi wapo na kazi inaendelea boda, kilimo, ufugaji, mikopo/ujasiriamali, saidia fundi, migahawa etc. (Hoja ya kiwango cha elimu wameiweka pembeni kwanza - wanapiga kazi).
Cha msingi ni wajipatie riziki kiHalali na wasikalie kazi ya kulalamika kutwa nzima as if kuna mtu amezuia au amehodhi nafasi za ajira kiasi kwamba ndo imesababisha wao wasipate au wakose ajira.
Ule ujiko wa kusoma kama huna hela hauna maana tena.

Cha msingi kila mtu mkono uende kinywani.

Hakuna kitu kibaya kama kuwa Broke hadi mla unakuwa wa taabu.
 
Mkuu kila mtu ana namna yake ya malezi. Wapo wanaojenga nyumba hadi za wajukuu na wapo ambao hawawapeleki shule kusoma degree. Kuna mzee mtoto akimaliza form four anakuwa utingo wa mafuso yao ya nyumbani akizoea anapewa fuso lake aanze mapambano. Na wote wapo vizuri.
Ni kweli mkuu, lakini inakuwa kwanza mtoto au mjukuu yeye mwenyewe aoneshe kwamba anaihitaji hiyo nyumba ila anashindwa uwezo. Mtoto kuwa utingo wa mafuso yao nyumbani (kama mtihani kwake) ni sawa ili ajifunze, apate uzoefu na mwisho kama akionesha kweli anamudu shughuli hiyo na ameipenda, akipewa fuso lake ili sasa yeye ndo awe mmiliki wa mali hiyo au ni dereva au msimamizi, mfuatiliaji na mkusanayaji mapato ambayo ni mali yake, hiyo ni sawa. Vinginevyo tofauti na hapo, hilo fuso linaweza kuwa ndo mwisho wa maisha yake. Ukimjengea nyumba anaweza kuitelekeza hapo na akaishia kusikojulikana.
 
Ni kweli mkuu, lakini inakuwa kwanza mtoto au mjukuu yeye mwenyewe aoneshe kwamba anaihitaji hiyo nyumba ila anashindwa uwezo.
Mkuu kama unaweza, mali kwa uzao wako ni lazima si suala la uhitaji wa mtoto. Hata kama kasoma, kumpatia kiwanja, nyumba akiwa anaanza maisha ni sahihi. Ile inarahisisha mambo mengi na kuondoa vizazi vyako katika umasikini. Kama inawezekana lakini ila kama huwezi unafanya lile linalowezekana ila hakikisha mwanao hapitii yale uliyopitia, njia yake iwe na unafuu.

Unajua kwanini wapo wanasiasa hawashibi na wanajua hawaishi milele? Wanataka kuacha urithi hadi wa vitukuu.
 
Mkuu kama unaweza, mali kwa uzao wako ni lazima si suala la uhitaji wa mtoto. Hata kama kasoma, kumpatia kiwanja, nyumba akiwa anaanza maisha ni sahihi. Ile inarahisisha mambo mengi na kuondoa vizazi vyako katika umasikini. Kama inawezekana lakini ila kama huwezi unafanya lile linalowezekana ila hakikisha mwanao hapitii yale uliyopitia, njia yake iwe na unafuu.

Unajua kwanini wapo wanasiasa hawashibi na wanajua hawaishi milele? Wanataka kuacha urithi hadi wa vitukuu.
Yataka moyo na mtu ajipange vizuri tokea wanawe wakingali wadogo. Ipo mifano mingi (nadhani unaijua hata ww) ya matajiri waliojaribu hivyo lakini mara tu baada ya kifo chao, kulianza mtifuano ndani ya familia wakigombea mali alizoacha marehemu hata kama aliandika wosia. Wengine wamediriki hata kuuana katika ugomvi huo.
 
Yataka moyo na mtu ajipange vizuri tokea wanawe wakingali wadogo. Ipo mifano mingi (nadhani unaijua hata ww) ya matajiri waliojaribu hivyo lakini mara tu baada ya kifo chao, kulianza mtifuano ndani ya familia wakigombea mali alizoacha marehemu hata kama aliandika wosia. Wengine wamediriki hata kuuana katika ugomvi huo.
Huu mfumo haufai kutumika kama una watoto wa mama tofauti tofauti unless ulitumia nafasi yako kama baba kuwaleta pamoja wakawa kitu kimoja, yaani watoto wapendane bila kujali mama zao wanawaambia nini.

Pia huu mfumo unafanya kazi vizuri pale ambapo watoto tangu wadogo wanakua wakiwa wanashirikishwa katika shughuli za familia. Sio wameenda kusoma huko wamerudi ni watu wazima ujaribu kuwaingiza kwa nguvu.

Mfano, mnajenga nyumba watoto wakiwa na 10 years wanaenda sight kupanda miti, kila mmoja kapewa mti wake wa kuutunza wakija kuwa na 25 years maamuzi ya kuuza hiyo nyumba yatakuwa magumu mno sababu ya memories na bond zilizosimikwa na eneo husika.

Tatizo letu wazazi wa kitanzana matukio ya kuwafanya watoto wawe na bond hatuna kabisa.
 
Back
Top Bottom