Inawezekana kipindi cha Mkapa ndio ujambazi mkubwa ulitamalaki

Inawezekana kipindi cha Mkapa ndio ujambazi mkubwa ulitamalaki

Na alitangaza hadharani, majambazi wanyang'anywe silaha harakaharaka. Alitoa ile kauli kimzahamzaha ila kumbe alimaanisha.

Baada ya hapo stori zikawa ni mwndo wa majambazi yauawa wakati yakijaribu kupambana na polisi. Yani kama wewe ni jambazi unawekwa kwenye rada, unakamatwa unapelekwa milimani/maporini unapigwa shaba kisha asubuhi na mapema unakuwa kwa niuuuuz
Kuna moja polisi walisema mtuhumiwa alijirusha kwenye defender ikiwa kasi..😀
 
Chai.

Sababu ya watu wa mara kuwa jeshini kwa wingi ni ari na ujasiri wa kupigna vita wakati wa vita ya kagera. Wakati mikoa mingine wakiwa wamelegea na wengine kukimbia kwenda jeshini, mkoa wa Mara ulionekana kama vile nafasi zilizotoleww zilikuwa kidogo kulinganisha na wanaojiandikisha. Vijana wengine wakawa wanawahi kwenda mikoa ambayo vijana wanasitasita kujiandikisha. Mwisho wa usaili ikaonekana vijana wa Mara ni wengi sana. Kuna stori ambayo in uhakika kama ni kweli ila wanasema ilibidi hata serikali iangalie nafasi za mikoa ambayo hawakujiandikisha wa kutosha, zipelekwe mkoani Mara kwasababu kule vijana walikuwa wanapambana kujiandikisha.
mzee kuna secret agent tunajua mambo kibao nyuma ya pazia tuulize sisi.
 
Nadhani IGP alikuwa Omary Mahita aliyekuwa na kashfa nyingi za kushirikiana na na baadhi ya Majambazi

Kuna lile tukio la 2006 la uvamizi wa gari la NMB lililokuwa limebeba pesa.. Hili si la Mkapa lakini ni mabaki yake

Tukio lile la CRDB Nyerere road wale wandava waliingia saa mbili asubuhi na Range rover mbili nyeusi na kufanya yao.. Ilikuwa kama picha la shozniga.. Wakapora mabilioni wakasepa kusikojulikana.. Hatukuwahi kusikia kuna waliokamatwa

Likaja la Tegeta baada ya defender la polisi kuingia kwenye mfumo wa majambazi na kukutana na miziki minene ya AK47.. Katika kujihami askari wale na jibwa lao lenye mafunzo makali sana wakalala kwenye sakafu ya body la gari

Wale majambazi walikuwa na mafunzo ya ziada walipeleka moto wa risasi za rasharasha pembezoni mwa body na kuwamaliza askari wote pamoja na umbwa lao

Matukio ya uporaji mabenki at gun point yalikuwa mengi sana, mengine yalifanyka city center kabisa mapema asubuhi ama mchana kweupe

Matukio haya yakafuatiwa na uvamizi vituo vya polisi, kupora silaha, kujeruhi na hata kuua askari

Kwa wasiojua zamani kabla ya uvamizi wa vituo vya polisi raia walikuwa wanaingia muda wowote 24/7

Baada ya matukio ya uvamizi kushika kasi ndio ikaja sheria mpya ya askari kulinda vituo kuweka uzio na vizuizi na raia kutoruhusiwa kuingia na gari hasa nyakati za usiku.. Na baadhi ya vituo vikawa vinafungwa usiku

Matukio ya uvamizi, uporaji na mauaji havikuishia kwenye mabenki tu bali hata

Kwenye maduka makubwa na madogo
Sehemu za kubadili pesa za kigeni
Vibanda vya mawakala wa pesa
Vituo vya mafuta nknk

Kwenye matukio yote haya wahusika wa usalama wa raia na mali zao hakuna aliyejiuzulu hata mmoja

Kwenye matukio yote haya 'inside jobs' zilikuwa nyingi

Kwenye matukio yote haya kuna mamlaka za ulinzi na Usalama zilituhumiwa kushirikiana na majambazi

Nyakati za Jk kukawa na matukio mengi ya utapeli mkubwa kuliko ujambazi wa kutumia silaha

Kwenye utawala wa Magu todate majambazi yakafyekwa kisawasawa Ila kutekwa na kupotea kwa watu kukatamalaki kwa viwango vya kutisha
Alikuwa fala sana yule Mzee aliendekeza pombe na umalaya, Alikuwa na IGP Jambazi hovyo kabisa
 
Nadhani IGP alikuwa Omary Mahita aliyekuwa na kashfa nyingi za kushirikiana na na baadhi ya Majambazi

Kuna lile tukio la 2006 la uvamizi wa gari la NMB lililokuwa limebeba pesa.. Hili si la Mkapa lakini ni mabaki yake

Tukio lile la CRDB Nyerere road wale wandava waliingia saa mbili asubuhi na Range rover mbili nyeusi na kufanya yao.. Ilikuwa kama picha la shozniga.. Wakapora mabilioni wakasepa kusikojulikana.. Hatukuwahi kusikia kuna waliokamatwa

Likaja la Tegeta baada ya defender la polisi kuingia kwenye mfumo wa majambazi na kukutana na miziki minene ya AK47.. Katika kujihami askari wale na jibwa lao lenye mafunzo makali sana wakalala kwenye sakafu ya body la gari

Wale majambazi walikuwa na mafunzo ya ziada walipeleka moto wa risasi za rasharasha pembezoni mwa body na kuwamaliza askari wote pamoja na umbwa lao

Matukio ya uporaji mabenki at gun point yalikuwa mengi sana, mengine yalifanyka city center kabisa mapema asubuhi ama mchana kweupe

Matukio haya yakafuatiwa na uvamizi vituo vya polisi, kupora silaha, kujeruhi na hata kuua askari

Kwa wasiojua zamani kabla ya uvamizi wa vituo vya polisi raia walikuwa wanaingia muda wowote 24/7

Baada ya matukio ya uvamizi kushika kasi ndio ikaja sheria mpya ya askari kulinda vituo kuweka uzio na vizuizi na raia kutoruhusiwa kuingia na gari hasa nyakati za usiku.. Na baadhi ya vituo vikawa vinafungwa usiku

Matukio ya uvamizi, uporaji na mauaji havikuishia kwenye mabenki tu bali hata

Kwenye maduka makubwa na madogo
Sehemu za kubadili pesa za kigeni
Vibanda vya mawakala wa pesa
Vituo vya mafuta nknk

Kwenye matukio yote haya wahusika wa usalama wa raia na mali zao hakuna aliyejiuzulu hata mmoja

Kwenye matukio yote haya 'inside jobs' zilikuwa nyingi

Kwenye matukio yote haya kuna mamlaka za ulinzi na Usalama zilituhumiwa kushirikiana na majambazi

Nyakati za Jk kukawa na matukio mengi ya utapeli mkubwa kuliko ujambazi wa kutumia silaha

Kwenye utawala wa Magu todate majambazi yakafyekwa kisawasawa Ila kutekwa na kupotea kwa watu kukatamalaki kwa viwango vya kutisha

Inawezekana IGP kushiriki? Ingawa hizi story zimekuwepo. Na especially pale Moshi. Kulikuwa na RPC ambaye alikuwa anatizamwa kwa mashaka sana.
 
Ujambazi ulikuwepo ila mnaposema mpaka ilifikia hatua ya vituo vya Polisi kufungwa usiku sababu yao hapo mmeongeza chumvi.
Hapana fuatilia usiwe mwepesi wa kukanusha.. Ilifika mahali vituo vidogo vya police vilikuwa vinafungwa saa 12 jioni.. Tena vingine ni hapa Dar
 
Zamani kuipata pesa ya serikali ilikuwa ni ngumu sana ndo maana kukawa na magenge kutoka kwa viongozi sasa hivi watu pesa wanachota tu unakuta kijana mdogo ni tajiri mkubwa na ni mtoto wa kiongozi hizo pesa katoa wapi
 
nasikia watuhumiwa wengi walikua wanatoka mara serikali ikatumia njia ya kuwapa kipaumbele jeshini na upolisi sasa ivi hali ikawa shwari.

ukichunguza ni kama kweli 70% ya polisi na wanajeshi ni watu wenye vina saba vya mkoa wa mara
Kuna swali la kijinga watu huulizwa kuhusu umri wao ikitokea hoja.Nimelitoa kwenye kundi la kuitwa swali la kijinga.Kuulizwa ..."una umri gani"...?
 
Back
Top Bottom