Uchaguzi 2020 Inawezekana vipi gari zote hizi tena aina tofauti ziwe na namba hii ya T 2020 JPM?

Hii nchi polisi wanajuaga sheria ikiwa ni upinzani tu, ukiwa CCM unaweza kufanya lolote. Huku Tabata yamejaa kuanzia la mgombea ubunge Segerea, madiwani na mashabiki.
Msijifanye vipofu wewe ungekuwa polisi ndio ungefanyaje?

Vaa viatu vyao
 
Achilia tu ajali, what if yanatumika kwa nia ovu na wazee wa malindi?
 
Utashindana na Rais wewe?
Mwambie asishindane nae kwa Nchi za Kiafrika Rais yupo juu kuliko hata Mungu si umeisikia ile video ya kimkakati mwanadada mwenzako alivyotamka ushindi wa CCM hauhitaji Mungu akipenda akipenda asipende ushind LAZIMA si ndio??
 
Kwahiyo likinigonga nisiende kuripoti?
We nenda tu karipoti lakini jiandae uwatajie chasis and engine number ya gari iliyokugonga, au engine na chasis number ya yale magari mengine 9 ambayo hayakuhusika ili hatimae wapate linalohusika!!

Haya mambo mbona simple tu Ndugu Wananchi!!!
 
Haziwezi zikawa special namba wakati ni magari zaidi ya matano hapo. Special namba inakua kwa gari moja
Sio kwa gari moja, kwa namna tofauti na ya kipekee
 
Utapoteza muda wako. Wewe umeyaona kama kumi hivi kwa hiyo yapo zaidi ya hayo. Utakapokuwa unatoa taarifa utalitofautishaje hilo na yale tisa mengine?
Nadhani level yako ya kuelewa iko chini. Huko kushindwa kutofautisha hayo magari yanayotumia hiyo namba ndiyo swali la aliyeleta hii mada. Swali lake kwa nini namba moja itumike kwa magari mengi, tutatofautishaje pale moja likileta shida?? Mrudie kumsoma na kisha soma ulichoandika.
 
Ni hivi, hizo ni private number na zinalipiwa TRA.
Hata wewe kama una gari 5 na zote unataka kuweka jina lako (Rrondo) ni pesa yako tu
Ukitaka kuweka jina lako, utasajili kwa COUNTRYWIDE 1, COUNTRYWIDE 2, COUNTRYWIDE 3 etc ili kuweka tofauti ya gari moja na nyingine. Huwezi kusajili magari yako kumi yote "COUNTRYWIDE"
 
CCM tuna rahaa tele kwa kuwa tupo juu ya sheria.Hata hii ya kwangu hii nimeweka hiyo namba
 
Mwaka 2015 Magufuli aliwaaminisha watu kuwa katika serikali yake kila mtu atafuata sheria hata awe wa CCM. Kumbe yeye ni bingwa wa kuvunja sheria na wale wafuasi wake kwenye hii nchi wameruhusiwa kufanya chochote. Yani mwaka 2015 tuliingia mkenge wa aina yake.
 
Kila siku tunapiga kelele kuhusu Serikali hii na CCM yake wanafanya mambo ya kipuuzi yaliyo kinyume cha Sheria lakini hakuna hatua inayochukuliwa. Imagine hayo magari yangekuwa yameandikwa Lissu au Rungwe unadhani yangeruhusiwa kupita Barabarani?
Kabla ya kufika huko, tra wangepata usajiri?
Maana angeambiwa kamishna nae angempigia Rais simu kutaka ushauri, angemwambia kama hutaki kazi sajiri
 
Ni hivi, hizo ni private number na zinalipiwa TRA.
Hata wewe kama una gari 5 na zote unataka kuweka jina lako (Rrondo) ni pesa yako tu
Zitakuwa something like RRONDO 1, RRONDO2, RRONDOX etc, na sio zooooooooote RRONDO!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…