Inawezekanaje nchi ndogo ya Denmark kuipa misaada nchi kuubwa Tanzania?

Inawezekanaje nchi ndogo ya Denmark kuipa misaada nchi kuubwa Tanzania?

Kwa Tanzania Mzee Ruksa akaanza kuibomia misingi mibovu,mkapa akaendelea kuisambaratisha, Kikwete akaanza kuijenga upya, Magufuli akajitahidi kuirudisha baadhi ya misingi mibovu ya Nyerere na kuibomia misingi mizuri iliyosnza kujengwa na Kikwete, Mwenyezi Mungu akamstopisha.

Kwabuwezo wa Mwenyezi Mungu katuwekea Mama Samia kurekebisha palipoanza kubomolewa na bwana yule na kuendeleza kuijenga misingi thabiti iiyoanza kujengwa na Kikwete.

Heko mama Samia.
Comment yako hii kuna ujumbe zaidi ya ulichoandika, ingebeba maana kama ungekuwa neutral
 
Nikisema hoja yako ya kipuuzi, unaweza kusema nimekuonea, labda niseme kuwa huelewi chochote.

Ebu nipime uelewa wako kidogo:

Singapore, Malaysia, Thailand, hizi nchi zina umri gani? Unajua kuwa haya mataifa yote tulikuwa kwenye kiwango sawa cha umaskini 1961? Imekuwaje leo UNDP wanasema pale walipofikia Malaysia, wakabakia hapo hapo, wasuendelee zaidi, sisi kwa speed tunayoenda nayo itatuchukua miaka 250?

Vipi kuhusu mataifa kama Misri na India, yameendelea sana kwa sababu nibya zamani sana?

Fuatilia, kuna scientific study kubwa ilikwishafanyika ili kujua kwa nini baadhi ya mataifa ni maskini sana na mengine ni matajiri sana.
Asipoelewa hapa tena ndio basi tena hao ndio drawbacks zenyewe
 
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Mshahara wa mbunge uwe milioni Moja na watumie public transport!

Mkuu lakini na wewe! Hujui hata posho ya laki tatu kwa siku haitoshi?

Kumbuka malalamiko ya wajumbe wa bunge la katiba, walidai laki tatu ilikuwa haiwatoshi, wakapendekeza iongezwe ifike alau laki tano kwa siku.
 
Ubelgiji na mfalme Leopard II waliona zao la mpira wakawa wavuna na kupeleka Ulaya kama malighafi ya kutengeneza matairi.

Danlop ni moja ya viwanda maarufu duniani ambavyo malighafi yake ya mpira ilitokea Congo.

Pia Ubelgiji waongoza duniani kwa bidhaa zitokanazo na kakao ni wapenzi wa chocolate mtaelewa.

Mwisho, Antwerp ndipo yalipo makao makuu ya Amasi yote chafu (isiochakachuliwa) kutoka sehemu mbalimbali duniani hususan barani Afrika.

Ni kutumia akili zetu tu si uchawi, maana watanzania tulikuwa na kiwanda cha baiskeli cha Swala ambacho leo hii kipo tu kimetulia.

Hakuna matoleo mapya ya baiskeli wala matairi yake wala angalau baiskeli hata za watoto.
Mpaka sasa Tanzania inasifika kwa kuzalisha nini?
 
Chukulia mfano tu hata hapa Tz, mpaka leo msukuma/mnyakyusa wa huko ndanindani wala hajui kua hii nchi kuna kabila jingine zaidi yao. Hii inafanya kua na fikra mfu kabisa, huna changamoto yoyote utagunduaje vitu??
Mwaka 2020, nilikuwa sehemu fulani wilayani Misungwi mkoani Mwanza. Nilikutana na vijana watu wazima ambao ingawa kutoka hapo mpaka Mwanza Mjini nauli ilikuwa sh 5,000/=, lakini hawakuwa wameshafika Mwanza Mjini. Hata barabara ya lami hawakuwa wameshaiona.

Maghorofa waliyaonea kwenye video.

Tokea amezaliwa, amesoma hadi kuhitimu la saba, kaona na kuzaa, lakini barabara ya lami alikuwa akiisikia tu au kujiona kwenye video, japo Mwanza Mjini ulikuwa ni umbali wa nauli ya sh 5,000/= tu.
 
Nini chanzo cha huo utofauti?
Siunajua ukweli unauma, ila ngoja niseme, ni elimu yenye manufaa wa wote yaani hakuna ujinga nchi nzima, hata ukitengeneza sera unajiuliza hawa watu watazipokeaje maana uchambuzi wake hata kwenye mswada unakuwa wenye manufaa, mfano Sasa wengi wanaangalia taarifa ya habari kama tamthilia Sasa huko kila taarifa ya habari inahojiwa imeleta tija kweli au ni tamthilia, bunge linafanyiwa tathmini za kisomi kila wizara inaleta hoja zenye tija, na wabunge hivyo hivyo hawawezi kuweka watu juani na kutoa hoja za ndiyo Mzee bila kuulizwa hili litafanyika kweli au niusanii.
 
Mwaka 2020, nilikuwa sehemu fulani wilayani Misungwi mkoani Mwanza. Nilikutana na vijana watu wazima ambao ingawa kutoka hapo mpaka Mwanza Mjini nauli ilikuwa sh 5,000/=, lakini hawakuwa wameshafika Mwanza Mjini. Hata barabara ya lami hawakuwa wameshaiona.

Maghorofa waliyaonea kwenye video.

Tokea amezaliwa, amesoma hadi kuhitimu la saba, kaona na kuzaa, lakini barabara ya lami alikuwa akiisikia tu au kujiona kwenye video, japo Mwanza Mjini ulikuwa ni umbali wa nauli ya sh 5,000/= tu.
Ndio tatizo hilo sasa, mtu kama huyo hata lami haijui si ataona ni sawa tu kwa hiyo barabara aliyonayo.

Miaka ikienda wajukuu wakija kuiona lami wataanza kujiona ni hamnazo wakati huko kulikojengwa lami, wao waliona mahala wakaiga. Waliona tatizo la barabara wakatafuta soln
 
Hilo haliwezi kukataliwa, lakini adhari zake zisingepaswa kuwa za kudumu kwa miaka nenda rudi.

Tanzania haikuwa ya kwanza kukabiliana na vita. Kama vita ni sababu ya nchi kuwa dumavu kiuchumi, basi hata Japan na Ujerumani nazo zilipaswa kuwa chini.

Na Rwanda je? Pamoja na vita vya wenyewe kwa wenyewe ilivyokabiliana navyo mwaka 1994, lakini bado kuna vitu inatupita. Kumbuka Rwanda ni kadoogo kieneo, na rasilimali zake ni chache sana ukiilinganisha na Tanzania.

Fikiri tu, kwa mfano, TANZANITE, BANDARI YA DAR ES SALAAM na SERENGETI NATIONAL PARK zingekuwa kwa Kagame, Rwanda ingekuwa wapi kwa sasa?
Muda mwingine nadhani tupo trapped kwenye vicious cycle. Kwa maana ya kwamba mtu let's say hajaajiriwa halafu anaona walioko kwenye payroll Kwa maana ya waajiriwa iwe wanasiasa au watumishi wa kawaida wanavyotafuna pesa za serikali kifisadi , naye automatically ataamini kwamba kumbe mfumo ndio hivi wa kupiga pesa? Kwa hiyo ikitokea ameingia kwenye mfumo wa ajira tayari akiwa na hiyo mentality hata kama alikuwa ni mzalendo na hard working, mambo yanakuwa ni Yaleyale na tunakuwa stagnant kama nchi.
 
Muda mwingine nadhani tupo trapped kwenye vicious cycle. Kwa maana ya kwamba mtu let's say hajaajiriwa halafu anaona walioko kwenye payroll Kwa maana ya waajiriwa iwe wanasiasa au watumishi wa kawaida wanavyotafuna pesa za serikali kifisadi , naye automatically ataamini kwamba kumbe mfumo ndio hivi wa kupiga pesa? Kwa hiyo ikitokea ameingia kwenye mfumo wa ajira tayari akiwa na hiyo mentality hata kama alikuwa ni mzalendo na hard working, mambo yanakuwa ni Yaleyale na tunakuwa stagnant kama nchi.
Like the son, like the father.

Kunahitajika mapinduzi ya kifikra ili kutoka kwenye huo mzunguko.
 
Ukitaka kujua kuwa tatizo ni mtu mweusi, angalia nchi kama South Afrika na Zimbabwe. Kabla ya uongozi kuchukuliwa na watu weusi, nchi hizo zilikuwa zinakaribiana sana na baadhi ya mataifa ya Ulaya. Baada ya uongozi kuchukuliwa na watu weusi, mataifa hayo yanakwenda kwa kasi kuyafuata mataifa ya wenzao weusi.

Sasa hivi makaburu wa South Afrika, kila mwaka kwa mamia, wanaihama South Afrika, wengi wakihamia Australia.

Karne ijayo, South Afrika haitakuwa tofauti na mataifa mengine ya Afrika.
Hata sisi Nyerere alitakiwa awaache wakoloni kwa muda hadi tupate elimu ya kujisimamia
 
Hata sisi Nyerere alitakiwa awaache wakoloni kwa muda hadi tupate elimu ya kujisimamia
Wapigania Uhuru walikuwa na maono gani wakati walipokuwa wakiendesha harakati za uhuru? Ni nini walichokitarajia kukipata, ambacho wakoloni walikuwa hawawapatii?
 
Wapigania Uhuru walikuwa na maono gani wakati walipokuwa wakiendesha harakati za uhuru? Ni nini walichokitarajia kukipata, ambacho wakoloni walikuwa hawawapatii?
Wapigania uhuru wengi walijawa na chuki dhidi ya wakoloni, walitaka sana wapate madaraka
 
Back
Top Bottom