Inawezekanaje nchi ndogo ya Denmark kuipa misaada nchi kuubwa Tanzania?

Inawezekanaje nchi ndogo ya Denmark kuipa misaada nchi kuubwa Tanzania?

Tatizo letu ni misingi mibovu iliwekwa toka tulipopata uhuru.
Sidhani ni tangu tulipopata uhuru, sema tangu tulipozaliwa.

Maana kama ni misingi mibaya baada ya uhuru, mpaka leo ni miaka mingapi? Hiyo misingi mibaya kwa nini haibadilishwi? Mbona mataifa mengine yaliyopata uhuru baadaye, kama Botswana na Namibia, wao angalao wanapiga hatua kwa kasi?
 
Magufuli alipotaka kuigeuza Tanzania iwe sawa na nchi za Ulaya mlimfanyaje? Mnataka maendeleo lakini hamtaki namna ya kuyafikia hayo maendeleo. Maendeleo ni malengo, nidhamu, kujitoa mhanga (self sacrifice), bidii ya kazi, uadilifu na kutambua vipaji na ubunifu na kuvitumia ipasavyo. Ulaya wameweza kuviunganisha hivyo vyote kufikia hapo walipo. Sisi hapa bado tunajitafta na akija mwenye mawazo kama hayo bado hatumwelewi. Tutachelewa sana.
 
Miaka ya nyuma, wakurugenzi wa Halmashauri walikuwa na kawaida ya kukusanya mafungu ya kuwapelekea wabunge ili mambo yawawaendee sawa wakati wa bajeti, hivi huo ujinga ulishaishaisha?
Sisi tunaangushwa na viongozi wetu, kupitishatu bajeti mpaka wabunge wahongwe. Yaani Africa tumelogwa na nani?
 
Mnaonaje katiba ijayo tuwe na kipengele Cha kusajili viongozi, Kama mawaziri, wakuu wa wilaya, Kama ifanywavo kwenye football.

Tuna mchukua mtu kwenye Kariba ya kiduku😀 tunamkabithi wizara kiroho Safi, tuna achana na hawa wanaoiba huku, kesho wahamishiwa Kule wakaibe Tena.

Rais pekee ndio tunampigia kura
 
Denmark inatarajia kuufunga ubalozi wake nchini Tanzania ifikapo 2024. Ni kati ya nchi ambazo zimekuwa zikiipa Tanzania misaada, tokea ikiitwa Tanganyika hadi sasa ikiwa inajulikana kwa jina adhimu, Tanzania.

Lakini Denmark ni nchi ya namna gani?

Ukifanya ulinganisho, Tanzania imeizidi kwa mambo mengi isipokuwa ujinga na umaskini. Ina rasilimali nyingi sana kuizidi, na hata idadi ya watu tumeipita mbali sana.

Denmark, ni kanchi kadoogo, kenye ukubwa wa kilomita za mraba 42,920 lakini inaizidi kiuchumi Tanzania, nchi Kuubwa kieneo, yenye kilomita za mraba 945,087.

Denmark, ni kanchi kadoogo kenye watu milioni tano lakini inaipa misaada nchi kuubwa, Tanzania, yenye watu milioni sitini na moja.

Ni nini siri ya kanchi kadogo kuizidi nchi kubwa kama Tanzania? Imekuwa ikiisadia Tanzania tokea 1963, enzi hizo ikiitwa Tanganyika, lakini hakuna taarifa ya Tanzania ambayo ni nchi kubwa kuisaidia Denmark kanchi kadogo.

Imewezekanaje kwao lakini kwetu ikashindikana?

Mwingine anaweza kusema ni kwa sababu ya ukoloni, lakini hilo halina mashiko. Hata Korea Kusini ilishawahi kuwa koloni la Japan, lakini kwa sasa wanatukimbiza kiuchumi.

Ni nini walichogundua hao watu weupe ambao weusi wa Tanganyika na Zanzibar hawajagundua?

Angalia, hata eneo la Korea Kusini ni dogo sana ukililinganisha na ukubwa wa Tanzania. Ina kilomita za mraba 100,210 na watu milioni hamsini na moja.

Inawezekanaje kanchi kadoogo, Denmark, kuipa misaada nchi kuubwa, Tanzania?
Denmark wanaweza kugeuza mchanga/udongo kuwa mashine, Tanzania hatuwezi kugeuza mchanga/udongo kuwax mashine.

Sababu ya pili utawala bora.

Tatu wasomi wao hawalink tumbo na akili katika kudadavua hoja huku kwetu tumbo ndio linaaamua upi uwe ukweli na upi usiwe ukweli sio brain.

Mwisho, huku kwetu wizi ndio primary factor katika kuamua kipi kifanyike na kifanyike n.amna gani, wao determinant ni wap kuna manufaa makubwa zaidi kuliko kwingine wanapotaka kuchagua wafanye kipi.
 
Siyo Denmark pekee. Vinchi vyote vidogo huko Ulaya, na baadhi huko Asia, ukilinganisha na Tanzania ni aibu tupu:

Denmark
Norway
Finland
Sweden
Singapore
Switzerland

Utajiri mkubwa hapa Ulimwenguni ni akili, wala siyo idadi kubwa ya fisi na pundamilia, siyo dhahabu na gas, ardhi nzuri ya kilimo, maziwa, bahari au hali nzuri ya hewa.

Hata upewe vyote, ukinyimwa akili, vyote vinakuwa havina maana. Lakini ukibahatika ukapata akili,ni mwanzo wa mafanikio yote. Kwanza utajua ni nini kilicho muhimu, utakuwa na mifumo mizuri ya kuvuna rasilimali, utakuwa na tekinolojia, utakuwa na mifumo mizuri ya utawala, na mifumo mizuri ya kusimamia uchumi kwa ujumla.

Sisi tuna vitu vingi, lakini asilimia kubwa sana ya watu wetu wamenyimwa akili, utashi na maarifa. Ndiyo maana wachache wenye akili, maarifa na utashi, ama wanakuwa frustrated na kukata tamaa au kuishia kwenda kufanya kazi mataifa ya nje kwa sababu nchini mwao ni giza nene.
Mkuu, vipi ukilinganisha Tanzania na kanchi kadoogo, Rwanda?

Ni ndogo kieneo, na rasilimali zake ni chache mno ukilinganisha na Tanzania, lakini unaionaje?

Imeshapitia misukosuko migumu mno, lakini...

Nakubaliana nawe, utajiri mkubwa ni AKILI!!!
 
Mifumo ya Europe na kwetu ni tofauti kabisa.Uwajibikaji uko juu sana.kwa pande zote kwa serikali na kwa wananchi

Huko Ulaya wanachi wanaogopwa sana na wanasiasa huku kwetu wanasiasa wanaogopwa sana na wananchi.

Yaani Serikali unaiweka madarakani mwenyewe halafu ikishaingia inaanza kukukupa vitisho ukiihoji

Tanzania ni nchi ya matamko,vitisho na upigaji kwa ngazi zote
 
Kuna mwamba alisema Afrika hasa kusini mwa jangwa la sahara tukihamishiwa nchi za Ulaya nao wakaletwa kuishi hapa Afrika... Kwamba baada ya miaka 5 tutakuja kuomba msaada nilicheka sana... Ila ni kama. Kuna ukweli ndani yake

By the way... Kwanini wanafunga ubalozi wao!??
 
Siyo Denmark pekee. Vinchi vyote vidogo huko Ulaya, na baadhi huko Asia, ukilinganisha na Tanzania ni aibu tupu:

Denmark
Norway
Finland
Sweden
Singapore
Switzerland

Utajiri mkubwa hapa Ulimwenguni ni akili, wala siyo idadi kubwa ya fisi na pundamilia, siyo dhahabu na gas, ardhi nzuri ya kilimo, maziwa, bahari au hali nzuri ya hewa.

Hata upewe vyote, ukinyimwa akili, vyote vinakuwa havina maana. Lakini ukibahatika ukapata akili,ni mwanzo wa mafanikio yote. Kwanza utajua ni nini kilicho muhimu, utakuwa na mifumo mizuri ya kuvuna rasilimali, utakuwa na tekinolojia, utakuwa na mifumo mizuri ya utawala, na mifumo mizuri ya kusimamia uchumi kwa ujumla.

Sisi tuna vitu vingi, lakini asilimia kubwa sana ya watu wetu wamenyimwa akili, utashi na maarifa. Ndiyo maana wachache wenye akili, maarifa na utashi, ama wanakuwa frustrated na kukata tamaa au kuishia kwenda kufanya kazi mataifa ya nje kwa sababu nchini mwao ni giza nene.
Kumbe sote bas hatuna akili[emoji848][emoji848] maana sijui whats wrong with Africa... Au ndivo tulivo na tusijaribu kujilinganisha nao
May be sisi tumeumbwa tuwe nyuma
 
Mnaonaje katiba ijayo tuwe na kipengele Cha kusajili viongozi, Kama mawaziri, wakuu wa wilaya, Kama ifanywavo kwenye football.
Tuna mchukua mtu kwenye Kariba ya kiduku😀 tunamkabithi wizara kiroho Safi, tuna achana na hawa wanaoiba huku, kesho wahamishiwa Kule wakaibe Tena.

rais pekee ndo tunampigia kura
Naunga mkono hoja.
 
Kwa ufupi mtu mweupe kabarikiwa. Na zaidi sisi mijitu mieusi tunateswa na ubinfsi. Angali kiongozi wetu ananunua goli million 20 nchi gani taifa gani raisi ananunua goli la timu ya klabu kama sio ufisadi nini
Just imagine... Unanunua tiketi kwa ajili ya watu ambao wangeweza kujinunulia tiketi... What a wastage of resourses any way yani Muumba aje tu atutwae wote[emoji34][emoji34][emoji34]
 
Siyo Denmark pekee. Vinchi vyote vidogo huko Ulaya, na baadhi huko Asia, ukilinganisha na Tanzania ni aibu tupu:

Denmark
Norway
Finland
Sweden
Singapore
Switzerland

Utajiri mkubwa hapa Ulimwenguni ni akili, wala siyo idadi kubwa ya fisi na pundamilia, siyo dhahabu na gas, ardhi nzuri ya kilimo, maziwa, bahari au hali nzuri ya hewa.

Hata upewe vyote, ukinyimwa akili, vyote vinakuwa havina maana. Lakini ukibahatika ukapata akili,ni mwanzo wa mafanikio yote. Kwanza utajua ni nini kilicho muhimu, utakuwa na mifumo mizuri ya kuvuna rasilimali, utakuwa na tekinolojia, utakuwa na mifumo mizuri ya utawala, na mifumo mizuri ya kusimamia uchumi kwa ujumla.

Sisi tuna vitu vingi, lakini asilimia kubwa sana ya watu wetu wamenyimwa akili, utashi na maarifa. Ndiyo maana wachache wenye akili, maarifa na utashi, ama wanakuwa frustrated na kukata tamaa au kuishia kwenda kufanya kazi mataifa ya nje kwa sababu nchini mwao ni giza nene.
Umemaliza kila kitu hapa
Utajiri na rasilimali muhimu ni watu watu wenye akili ya kuchanganua mambo na kutatua changamoto zinazowazunguka
 
Back
Top Bottom