Influencer/brand ambassadors huwa wana ushawishi wa maana kwa watu kununua au kubadilisha bidhaa au huduma fulani?

Influencer/brand ambassadors huwa wana ushawishi wa maana kwa watu kununua au kubadilisha bidhaa au huduma fulani?

Hivi mtu kilaza kama Manara au Doto magari wanaweza kukushawishi wewe uache kutumia bidhaa flani na uhamie bidhaa flani?
Narudia tena, influencers wa Tanzania hawana impact kama ya influencers wa sehemu nyingine kama US.
Faida ya influencers wa Tanzania ni kuongeza kufahamika kwa brand husiku kitu ambacho mwisho wa siku kinaongeza mauzo.
Watu sio vichaa kuendeleza kuwatumia hao watu unaowaona ni vilaza.
 
Mkuu influencers Wana impact kubwa tu. Influencer wanaongeza visibility ya brand hasa kupitia kwenye digital platforms. Psychology ya manunuzi ilivo, ni rahisi mtu kununua kitu anachokifahamu au alichowahi kukisikia kuliko ambacho hajawahi kukiona au kukisikia kabisa.

Sasa issue sio personality ya influencer mmoja mmoja kwa mtu, watu wanachoangalia ni engagements zao kwenye digital platforms. Selling point ya influencers na brand ambassadors wengi bongo ni engagements zao DP.

In short, definition ya influencers wa bongo ni tofauti na influencers per SE kwa maana yake sehemu nyingine duniani.
Broo hapo umeongea kweli NI RAHISI MTU KUNUNUA BIDHAA ALOISIKIA AU KUIONA KULIKO BIDHAA AMBAYO HAIJUI 100%
 
Unaweza usielewe wala kuamini, lakini influencer wana mchango mkubwa sana kuuza bidhaa za makampuni. Ngoja nikupe shule ndogo kidogo;

1. Katika kufanya maamuzi, binadamu huongozwa na kitu kinaitwa Conscious (ufahamu huku ukijua) na Subconscious (ufahamu pasipo kujua), hao influencor kazi yao kubwa ni kuweka hints ya taarifa kwenye ubongo wako, na hiyo hubakia kama rejea (reference) itakayokuathiri wakati wa kuamua kununua kitu. wasipo kupata katika conscious basi wanaweza kukupata kupitia Subconscious. Hata kama hutanunua bidhaa wanayoitangaza (kwa sababu fulani mahususi uliyokwisha kuijenga) utajikuta wewe mwenyewe unanunua bidhaa nyingine lakini huku ukijua kabisa unaikwepa kimakusudi ile bidhaa iliyokuwa inatangazwa na influencer!

2. Katika sayansi ya biashara, huenda 90% ya wanunuzi huwa ni 'wajinga' wakati wa kununua, hununua bidhaa kwa kuaminishwa ni nzuri, bora au nafuu. Na imani hiyo huletwa kwa kusikia au kwa kuona watu wanaowaona au kuwasikiliza mara kwa mara. Mtu mwenye followers zaidi ya laki moja mtandaoni, maana yake ana watu laki moja wanaoweza kusilikiza chochote anachokileta, kuiga, kumuunga mkono nk. Ukikaa wewe mwenyewe binafsi halafu tafakari, utagundua kuna wakati maishani mwako uliwahi kununua kitu fulani kwa 'ujinga' tu, yaani kwa kuiga tu mtu au watu fulani, kuambiwa tu ni kizuri, bora au nafuu bila ya wewe mwenyewe kuchunguza kwa kina.
 
Inategemea ila mimi niko addicted na kitu chochote anachotumia Cristiano Ronaldo ata kondomu nitanunua because yeye
 
Bidhaa iliyo midomoni mwa watu ndiyo inayouzika mkuu.
Na ndicho makampuni mengi wanachofanya, kila muda we uwe unasikia neno pepsi pepsi, akilini mwako wakisema kinywaji basi basi chap utataja pepsi.

Ila nadhani wengi wanatumika kwakua wana folllowers wengi mitandao ya kijamii, so akitumia account yake kukutangizia bidhaa inawafikia watu wengi.
 
Doto Motokaa hawezi kukushawishi kununua gari kwa Ndugu Issa Tambuu?.
Hahaha kushawishika ni sawa na kutongozwa na ukakubali. Usifanye ujinga huo kabisa, nunua kitu kama unaweza au unakihitaji, usikubali kushawisiwa au kushawishika kwa namna yoyote ile.

Huyo Doto anakulipia hayo magari?
 
influencers Wana impact kubwa sana,
Hapa asilimia kubwa ya ambao wanapinga hilo hawajawahi hata kufanya biashara, wafanya biashara wanalijua hilo ndio maan kila leo utaona wanapewa hayo matangazo hao wakina baba levo wakina mwijaku kwasababu wale wanao walipa wanajua faida yake, ndio maana mtu haoni hasara kumpa kiredio M 2 afanye challenge bidhaa yake kwasababu anatarajia kurudi zaidi ya hiyo, halafa haya matangazo ya kulipia huko insta wewe unakutana nayo mangapi na unayapita bila kusoma wala kutizama? Huko YouTube Maadam Umewekewa Sekunde 30 Za lazima unakimbilia kukata sauti hutaki kusikia kabisa 😅
 
Back
Top Bottom