Infosys IPS (T) LTD wakanusha kuhusika na LUGUMI katika kashfa ya ubadhirifu

JPM Magufuli alishinda kura ki halali, hakuna kura iliyoibiwa! Ni nyie wapumbavu na malofa ndiyo mnadanganywa na mnakubali upuuzi wa kutumiwa kama toilet paper na mbowe. Nikupe hinti kidogo. Mbowe na genge lake ili waendelee kuwa na wafuasi ktk chaguzi, njia mojawapo ni kuhakikisha wanapinga na kukataa matokeo ili wasiwakatishe tamaa waliowapigia kura, pia ili kutokuwapoteza waliowapigia kura (yaani wajinga kama wewe utakaa kuamini uliibiwa kura maana yake utaishi na hiyo hasira for 5 years) halafu ukija uchaguzi mwingine utakuwa kama mbuzi wa kafara utasema safari iliyopita niliibiwa basi safari hii lazima nipigie tena kwani tumehakikishiwa kuwa hatuwezi kuibiwa (maana hata mamvi naye kajibainisha tena kusema eti next election kura haziibiwi). Kwa kifupi mbowe ni mjaja ktk kucheza na akili za wapumbavu kama wewe, na kawaweza kweli kweli.
 
Kwa hiyo nani alitakiwa kufunga hizo fingerprint na wao Infosys walipewa tenda ipi na hiyo kampuni je waliifanya? Nashauri fika kwa Lugumi maana anatupa headache mitandaoni
 

Kwa maelezo yako na kwa maadili ya uongozi na utumishi wa umma kitendo cha Mh waziri kutajwa kwenye kashifa kama hivyo tayali ni lazima ake pembeni kupisha uchunguzi kwa manufaa ya umma sio ya Mh. Rais. Akithibitika hana hatia itatangazwa kumsafisha. Haya ya kampuni yenu kupewa kazi na kampuni ya marekani yatatumika katika kuchunguza kama ni kweli au la. Pia mnadai waziri si mmoja kati ya wakurugenzi wenu kwa sasa. Ni sashihi kwani hata uchunguzi ukifanyika si utaonyesha hivyo!!!! Kwa nini mnatoka jasho? Hata hivyo kumbukeni kuwa Tanzania ina watu Zaidi ya milioni 46, Kitwanga hata ikiwaje hawezi kubakia kuwa waziri wa mambo ya ndani milele. kwa mujibu wako, urafiki wa JPM na Kitwanga ndio umempa Kitwanga uwaziri wa mambo ya ndani. Kama sio tusi kwa JPM naamini mtaendelea kueneza utetezi kwa lugha hiyo ili asiteuliwe rafiki mwingine kuendeleza nepotism katika utawala wake. Tulieni ili sharia ifuate mkondo wake.
 


Hii ndio dalili ya kutojua siasa na kukosa uelewa wa namna ya kupeana mawazo kwa njia ya mjadala. Zaidi ya nusu ya andiko lako unatukana tu. Jazba unaitoa wapi katika kujadiliana mambo kama haya. Pesa za umma zimetumiwa ndivyo sivyo. Unajitahidi kudivert mjadala na kuwajadili watu as if wao pia ni sehemu ya ufujaji huo. Jikite kwenye hoja na mambo ya msingi katika thread. Huamini kuwa kulipwa 90% ya kazi kabla kazi haijafanyika ni kinyume na kanuni na sheria za manunuzi ya umma? Huamini kuwa kazi hiyo kutofanyika kwa muda uliopangwa bila maelezo ya kutosheleza ni ukiukwaji wa sheria zinazosimamia kandarasi katika miradi ya umma? Waache wenye hela zao wapige kelele ili wasikike. Maslahi yenu binafsi hayana nafasi safari hii.
 
Magumashi na figisufigisu zile zile............ hii nchi bana, natamani nihame niende hata sudan kusini
 
Huu ni uhuni. Lugumu ktk hili hakustahili hata kusign mkataba kwasababu si kampuni yake ambayo ilifanya kazi hiyo ya kuvileta na kuvifunga vifaa hivyo kutokana na maelezo ya huyu jamaa. LUGUMI ni DALALI. Na inatisha sana kazi za wizara ya mambo ya ndani ambazo zina husisha usalama wa Taifa na wananchi wake kumpa dalali. Lugumi kapewa fedha. Kaenda nunua kampuni yenye kuuza vifaa vya finger prints na n.k, Nayo hiyo kampuni ikanunua kampuni ingine ya kuvifunga vifaa hivyo. Huu ni uhuni na ufujaji wa pesa za Watanzania. Hapa Serikali imelipa kampuni 3, Kitu ambacho kama ingekuwa ni umakini tungebaki kuilipa kampuni moja ambayo ingefanya kazi zote kwa wakati mmoja. Na vile vile ingekuwa rahisi kuibana kampuni hiyo endapo kutatokea makosa katika undendaji wake. Leo hii ukianza kuzifuata kampuni zote hizo tatu hutofanikiwa kupata majibu ya maana. Kitakacho endelea hapa ni kupigana dana dana na siku zitaenda na " business will be as usual kama asemavyo Rais Magufuli". Magufuli unatakiwa kuwawajibisha walio saini na kuitoa tenda hiyo. Lugumi hahusiki katika hilo. Kupanga ni kuchagua. Hakuna aliye lazimishwa kutoa tenda kwa Lugumi. Wizara na walio husika kumpa Lugumi kazi wanatakiwa kushughulikiwa. Baada ya hapo wizara husika wamtafute Lugumi na wamufungulie mashtaka kwa kushindwa kukamilisha kazi waliyompatia.
 
hao infossy buz zao zimekaa kiujanja janja sana.
 
Ngoja bunge lianze maana hata escrow ilikua na mvutano hivihivi,ila jua likiwaka vizuri kivuli hujitenga na kuonekana vyema
 
Je unakumbuka Richmond Develpment Company LLC. ya Marekani au ulikuwa hujazaliwa?
 

Sijui kwa huzuiwi kuwa kwenye jukwaa mpaka sasa hivi, umetumia lugha ya matusi! Pumbavu na na lofa ni hawa wanaotumbuliwa majipu., na nguvu kubwa inatumika kusafisa hilo.... Ritz1 katundika kitu kule fb, ngoja tukifatilie, kinahusu malaria....... hapo kuna home shopping center, Jm, na ruge ,,,,,,, tunanafukunyua
JPM anajijua na anajua kwamba ni rais wa CCM na si wa wa Tz, rais wa wa Tz hata uwaamshe kesho kwenye kura halali na tume huru ya uchachuzi ni Ngoyayi.
Sasa hivi kama Ukawa tungechukuwa nchi kila kitu poa.......
 
Lukoma!nafikiri mtafiti yuko kazini kuja na majibu yote tata,lakini ninachojua polisi iliingia mkataba na Lugumi na Lugumi akatafuta Wamarekani wamarekani nao wakaona hawana haja ya kuja wao wakati kunawazawa wanaweza kuunganisha vifaa hivyo nakufanya installation kwa vituo 108,kunatatizo kubwa Polisi katika vituo vyote vingi vimesimam kwa ukosefu ama wa umeme ama uzembe mwingi,Tumeishi kwa mazoea sana nchi hii hata wenzetu waliopewa dhamana ilikuwa shida kubwa tumsubili mtafiti ashuke na full majibu maana haamini Udaku ama single source
 
Wao kama Infosys hawawezi kukiri kwamba wanauhusiano na Lugumi.Hata hivyo kama nia ya dhati ipo ya kusambaratisha ufisadi nchini na hakuna double standards kama ambavyo imeshadhihirika mpaka sasa,TISS wafanye uchunguzi wa kina kuhusu swala hilo.Ikidhihirika kwamba upo uhusiano wa mashaka,hatua stahiki zichukuliwe dhidi ya Infosys.
 
Wanaomchukia Rais Dr.JPM sio wapinzani ni wanachama wenzetu humu humu, kagusa maslahi ya wakubwa katika CCM. Mungu amlinde huyu Rais, nchi inyoke maana ilikuwa imepinda. Kumbuka alisema nchi ilikuwa inaongozwa hovyo hovyo. Kuirudisha kwenye mstari sahihi kuna hitajika ujasiri wake tu, wengine walishindwa. YEYE HATASHINDWA, HE IS ON THE RIGHT TRUCK NOW
 

Nchi hii iko hoi bin taaban kwa sababu ya utawala uliopita, kisiasa na na ki kimajipu ukimuhusisha JPM. Isitoshe yeye ni ni Rais aliyeokota dodo kwenye muarobaini.... naye
anajua ni ni akina nani wamemfanya awe rais
 
Hivi kuna haja ya kutafuta ushahidi mwiingi wakati tunaona kabisa huyo jamaa keshachafuka...

Kuna haja gani Magufuli kuendelea na huyo jamaa anayemtia doa wakati wapo wengi tu wanaoweza kuhudumu kwenye hiyo nafasi?

Tena nashangazwa sana na wanaohusisha mambo ya Kitwanga na serikali ya Magufuli... jamaa ahukumiwe kivyake...
 

Acheni kumhusisha Magufuli na madudu ya Kitwanga... Kama amechafuka ni yeye, sio Magufuli.
 

 
Jamii forums ambayo watu wanaochangia "wamejificha" ndio chanzo kikuu cha kupata habari kwa vyombo vingi..hawajui za kuambiwa changanya na zakwako
 
Jamii forums ambayo watu wanaochangia "wamejificha" ndio chanzo kikuu cha kupata habari kwa vyombo vingi..hawajui za kuambiwa changanya na zakwako
Yani leo wanaandika hiki, kesho wanakwapua info mitandaoni wanaandika kile, keshokutwa kingine.
Hili swala wala hawakuhitaji mlolongo mrefu, wangeaza kwa Lugumi, wakafuata na Biometrica, wakamaliza na Infosys. Ndio wakatuletea habari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…