Infosys IPS (T) LTD wakanusha kuhusika na LUGUMI katika kashfa ya ubadhirifu

Infosys IPS (T) LTD wakanusha kuhusika na LUGUMI katika kashfa ya ubadhirifu

Haya sasa ukweli umewekwa wazi kumbe ni juhudi za kumpiga vita Waziri Kitwanga na kutaka kuichafua serikali ya Magufuli.

Wapiga dili tafuteni kiki nyingine ukweli ndio huu.
Ukweli upi ? Hapo hakuna ukweli wowote bali Uchakachuaji na Rushwa ndivyo vimetawala , hata mje na utetezi gani Safari hii Huyo boss wako lazima ajue kuwa Watanzania wa Sasa si wajinga kiasi hicho.
 
Kitwanga akae tu pembeni regardless of whatever... hizi tuhuma hazitapotea ng'o.
 
1. Wewe ni waziri tena wa wizara ambayo kampuni uliyoianzisha wewe wana mahusiano ya kibiashara. Je huoni kwamba kuna mgongano wa kimaslahi?

2. Ikiwa wizara yako imetangaza tenda kampuni yangu ikatenda na Infosys uliyoianzisha wewe ikatenda, naweza kupewa mimi? Hata nikikosa kwa haki na ikapata Infosys nitaridhika?

3. Hivi ni sahihi kampuni zenye mahusiano na mawaziri kufanya kazi na serikali wanayoitumikia?

4. Kampuni yako imekanusha kuijua wala kushirikiana na Lugumi. Wewe binafsi unaijua Lugumi na wamiliki wake? Kama unaijua inawezekanaje watu wa kampuni uliyoianzisha hawaijui?

5. Kelele kubwa zinaendelea kuhusu wizara unayoiongoza, kimya chako kinasababishwa na nini? Mbona hujatoka hadharani kuzungumza lolote kuhusu kinachoendelae ofisini mwako?

6. Unasubiri kutimuliwa? kwa nini usimwombe bwana mkubwa akuweke pembeni ili uchunguzi uendelee vizuri ofisini kwako?

7. Ni kweli kwamba una uhusiano/rafiki wa karibu na bwana mkubwa?

8. Uhusiano huo kama upo ni wa kawaida au wa kibiashara?

9. Kama ni wa kibisahara anahusika kwenye Infosys?

10. Kama mna uhusiano kama inavyosemekana huoni kwamba unampa mtihani mkubwa sana rafiki yako?

Kaswali kangu kadogo ni "Hao biometrica waliwajuaje na kuwapatia dili hawa Infosys?" Hili niswali linalojibika na linaweza kutuweka huru.
 
Kampuni ya INFOSYS IPS (T) LTD imekanusha taarifa zinazoenezwa katika mitandao ya kijamii kwamba kampuni hiyo inahusika na inashirikirikiana na Lugumi Enterprises katika kashfa ya ubadhilifu.

Katika habari zilizosambazwana watu wasiojulikana zinasema kwamba kampuni ya infosys ilipokea mabilioni ya shilingi kutoka katika kampuni ya Lugumi, jambo ambalo siyo la kweli na nilakupuuzwa na umma.

'Hatujawahi kufanya biashara na kampuni ya Lugumi Enterprises' Amesisitiza Bwana Sweki Donald Naibu Meneja Mkuu Infosys ips (T) LTD.
 

Attachments

  • IMG_4129.jpg
    IMG_4129.jpg
    85.7 KB · Views: 35
Hii nimeipenda. Kumbe Jeshi la Police ndo iliwapa kazi Bio-Metrica LLC, na siyo Lugumu kama Meneja Msaidizi wa Infosys alivyosema. Kwa habari hiyo hapo juu Bio-Metrica LLC ndo waliokuwa main contractor! Mhh?
My Take:This is about so called Damage Control

Mwanahabari anasema kaamua kufanya utafiti wake kupata ukweli. Amekwenda kwenye ofisi ya Infosys (pa kuanzia) na tayari kaamua ku-publish uchunguzi wake na kutoa conclusion kwamba hizo habari zingine mitandaoni si za kweli. Well, nilitegemea angetupa pia mahojiano aliyofanya na Lugumu Enterpries, Mh. Kitwanga na Bio-Metrica. Halafu, mimi hainiingii akilini kwamba major shareholder/Founder hajawahi kuingia ofisini for six years kwa kampuni inayo mlipa faida/dividend kila mwaka, ambayo ina makao makuu Dsm, siyo New York. No doubt, there is something fishy.
 
Fact kwamba Infosys imetajwa katika hilo deal na ni kweli wamekili kushiriki ni wazi kwamba yapo mengi tunayoweza kuyapata kuhusiana na ufedhuli huo. Ingekuwa hawajui chochote juu ya hilo deal, tungesema kuna haja ya kupunguza vidole na sauti kwa Infosys. Kitwanga hachomoki.

Ushauri: Acheni kufanya usanii kwani hamjui kuwa kila kitu kipo mikononi mwa vyombo vya uchunguzi kwa hatua Zaidi. Upuuzi wa kutuletea clip za kujaribu kupoteza ukweli haziwasaidii kwa sasa.
Mkuu, hakuna usanii, kuna nguvu kubwa inatumika kuhakikisha JPM anatengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani, kutokana na sababu kadha wa kadha. Magufuri angeweza mpatia jamaa wake wizara nono, ila alijari ulinzi wake mwenyewe. Wajanja wanataka wamcontrol JPM kupitia wizara ya mambo ya ndani. Kitu ambacho sidhani kama JPM atakiridhia any soon, maana hakuna sababu nzito ya kumuondoa jamaa. Kampuni yake ishaweka wazi kuwa walipewa mkataba wa $74,000.00 tu na si vinginevyo, kazi wamefanya na wamemaliza. Ikumbukwe hiyo $74,000.00 ni installation ya vifaa/site 108. Sasa kwanini asikomaliwe Lugumi mwenye mkataba wa 37bilion na Kashalipwa 34bilion, aje akomaliwe Kitwanga??
Je kuna mtu toka Biometrica Marekani aliyelalamikia poor installation services za infosys? Ushaambiwa infosys haina mkataba na Lugumi, ina mkataba wa kufunga vifaa vya Biometrica ambayo ilipewa kazi na Lugumi. Kwa namna hiyo muulizeni Biometrica kama hamuamini details zilizotolewa na Infosys.
Kwa kuwa swali hili lina involve US based company ni rahisi sana kupata ukweli, haya makampuni yakibanwa na mashirika yao ya kijasusi hayanaga namna, hata kama chenji watarudisha tu.

Inthemeantime kelele zote zingeelekezwa kwa Lugumi, aseme yeye basi kama kashirikiana na Infosys au Biometrica!
 
In the interest of the public, Mh. Kitwanga kwanza, awaite media na kusema anachojua kuhusu habari hizi (kama alivyo fanya J. Makamba kwenye kashifa ya shemeji zake waitaliano). Pili, kama hausiki, aje na taarifa aimbie umma amekwisha fanya nini ndani ya wizara yake kwa mkataba wa kazi iliyo kwisha lipiwa 99% kwa pesa za walipa kodi, lakini haijakamilika mpaka leo (kama anavyo fanya Prof. Mbarawa kwa wakandarasi wa mabarabara). Vingenevyo, hizi taarifa zingine ni za kusafishana tu.
 
Kitwanga ni kweli amewabana wazee wa dili chafu.
Hii kashfa ya Lugumi inanichekesha sana, eti Lugumi kakimbia, kakimbilia wapi? Eti haijulikani......
Swali langu, is Lugumi Invisible person?
Kakamatwa gaidi àliyekimbia (mwenye kofia ya pama) kwenye tukio la ulipuzi wa wamja wa ndege Ubelgiji, huyu Lugumi asiyejua hata kusoma atajifichaje asikamatike?
Mkuu huyo jamaa ameenda kubadili sura na atatoa mafuta kiasi tunboni pale alipoficha B zetu akirudi humjui,anaoa upya mkewe maisha yanakwenda!ni muhimu sasa kuwa na DNA profile ya watanzania wote.
 
Umeshaambiwa Kitwanga ni founder, ila kwa sasa sio Director, hivyo kibiashara anasubili gawio la faida mwisho wa mwaka.

Ok, hata kama Kitwanga angekuwa ni Director kwa sasa, bado wameweka mambo wazi kama infosys, ambayo yako crystal clear.

Watanzania wengi tunapelekwa na matakwa ya wanasiasa, Lowasa alivyokuwa CCM tuliambiwa ni fisadi, tukimuona tumzomee, ameingia CHADEMA amekuwa msafi kama malaika.

Vijana tuache kutumika katika siasa!
Usiitie Chadema kwenye wizi wenu na wala usitafute pa kujifichia CDM
Kama wewe ni mwizi basi ni mwizi tuu
 
Kitaeleweka tu, mmefanya chini ya wamarekani ambao nao walikua wakifanya kazi chini ya Lugumi, bado kidogo tutapata ukweli
Duh, kuna kauhusiano!! Kazi ni moja inawahusu Lugumi, Biometric, Infosys kwa upande mmoja na Polisi kwa upande mwingine. Tusubiri tuone
 
Duh vijana wengi na wachangiaji ni vilaza kwelikweli. Ukweli mmeambiwa kuwa Kitwanga is no longer in the mgt of infosys, yet hawakuingia mkataba na hiyo lugumi, zaidi na zaidi mkurugenzi wa nida siyo shareholder bado watu mnabisha tu! Je watanzania mmerogwa kuamini uongo??????? yaani ni sawa na kipindi kile watu mlimuamini lowasa kuliko magufuli ila baada ya wananchi kuamua mmeanza kujipendekeza kwa magu. In short Magufuli ni mpango wa Mungu, atafeli kila atakayeinuka kumpinga, na wengine mtakufa ili nchi yetu iende mbele, tumechoka kuishi na siasa za kudanganywa na kuamini. Sweki kamaliza kila kitu, na vita iko pale pale, waziri kitwanga ataendelea na nafasi yake, na wauza madawa mtakoma.
 
Lugumi - Biometrica - Infosys ..... Am confused. Sihitaji Masters Degree kuuelewa huu mchezo usiohitaji hasira.
 
"Yesu akamwambia petro, Amin, nakuambia wewe, Leo, usiku huu, kabla ya kuwika jogoo mara mbili,
utanikana mara tatu."
 
Wako watu wanaodai INFOSY ni mali ya kitwangwa hata iwe hivyo kwa makubaliano yao na Biometrica kitwanga ana tatizo gani hapo?
 
Duh vijana wengi na wachangiaji ni vilaza kwelikweli. Ukweli mmeambiwa kuwa Kitwanga is no longer in the mgt of infosys, yet hawakuingia mkataba na hiyo lugumi, zaidi na zaidi mkurugenzi wa nida siyo shareholder bado watu mnabisha tu! Je watanzania mmerogwa kuamini uongo??????? yaani ni sawa na kipindi kile watu mlimuamini lowasa kuliko magufuli ila baada ya wananchi kuamua mmeanza kujipendekeza kwa magu. In short Magufuli ni mpango wa Mungu, atafeli kila atakayeinuka kumpinga, na wengine mtakufa ili nchi yetu iende mbele, tumechoka kuishi na siasa za kudanganywa na kuamini. Sweki kamaliza kila kitu, na vita iko pale pale, waziri kitwanga ataendelea na nafasi yake, na wauza madawa mtakoma.

Thread hii inazungumzia wizi wa pesa za walipa kodi wewe unachanganya mada. Anzisha uzi wako wa kusifia utumbo - watu hatutakaa tusahau jinsi tulivyodhulumiwa, hata JPM mwenyewe anajua hilo ndo maana anafanya kazi kwa kufuata sera za opposition na anazifanya isivyo.
 
Post hii imeongeza chumvi katika kidonda. Infosys imeongeza ushahidi kuwa walitoa mafunzo katika regions 33 (vituo 108). Hoja ya msingi, mafunzo yametolewa katika vituo 108, mkataba unaonyesha mitambo ilitakiwa vituo 108. Mpaka sasa inaonyesha wamefikisha mitambo vituo 14 tu kati ya 108. Hoja kwanini wamelipwa pesa yote wakati hata robo ya kazi hawajamaliza?.

Inashangaza kuona baadhi yetu tumesharidhika na kaushaidi/Utafiti wa mtafiti ambaye hata yeye amekusisitizia kuwa fanya utafiti sio fanyiwa utafiti. Tujiulize kila mtu anaweza kufanya utafiti? Hapa mtafiti anawalaumu walaji wa habari au media? Hata hivyo mtafiti amesema yeye hakutaka kusoma udaku, tujiulize amejuaje kama haya yanasenmwa kwenye udaku? mtafiti asiye soma udaku ni mpofu. Anatakiwa asome udau ila apate source ya habari ila asiamini mpaka afanyie utafiti.

Hatuna haja ya kufurahia mpaka 34 bil za walipa kodi zirudi, tukifurahi mhusika amegundulika na adhabu kali imechukuliwa pamoja na kumfilisi mali zote yeye na washirika wake. Naomba watanzania wenzangu tutambue kuwa udaku, imaginationa pia ni vyanzo vya habari. Kinachotafutwa sio Kitwanga, sio Mag na wala sio CCM, ni bil 34 kodi za watanzania.

Mtafiti ametutaka tuwe watafiti, wadadisi. Tusiridhike na udau na tafiti na ushahidi mmoja. "Imagination is more important than knowledge, knowledge is limited". Siyo vibaya tukahoji dhamira ya ya mtafiti wetu! Lengo kuu ni kutaka kujua uhusiano kati ya Lugumi na Infosys, uhusika wa Infosys katika mkataba au kujua kama kweli polisi waliingia mkataba na lugumi na ameshalipwa 99% ya pesa wakati kazi amefanya 12% tu!.
 
Back
Top Bottom