Injinia Masauni, utekaji umemuondoa Mambo ya Ndani?

Acheni huo upumbavu wa kitoto, Abdul Nondo alikuwa na mke wa mtu hapo stendi ya Magufuli?

Watekaji walipokuwa wanampiga na kumuambia aache mdomo ndio kumendea wachumba za watu?

Au tuseme hao watekaji wanaoteka kwa sababu za mapenzi na dhuluma serikali haina uwezo wa kuwakamata au ndio unataka kuniambia yale maigizo ya Deo Bonge?

Hakuna manufaa yeyote serikali ya CCM itayapata kwa sababu ya utekaji.

Taasisi mbalimbali na mashirika ya dini kama CCT na TEC wanapoanza kupigia kelele utakaji serikali inafaidika nini?

Hamuoni kuwa wanaweza kuchochea waumini wao kuchukia CCM?

Hamuoni kuwa matukio ya TRA tegeta yanaweza kuongezeka? Mnataka kuipeleka wapi nchi yetu?

Polisi ni ya CCM, tume ya uchaguzi ni ya CCM, hofu inatokea wapi?

Hao akina Abdul wana nini cha kulitishia chama dola CCM hadi watekwe na kupewa kipigo?

Nyie tawaleni kwa amani tu hakuna mtu wa kuwaondoa madarakani, acheni kusumbua watu wasio na madhara yeyote.
 
gentleman,
drama na maigizo yenu binafs na ndani ya vyama vyenu yataendelea kuwatokea puani,

chukua mawaidha mujarabu hapo juu na utakua salama.

ukishupaza shingo usilaumu wengine,
jutia tamaa zako kwenye mambo ya watu
 
Utekaji inaweza kuwa ni hoja inayokuzwa kisiasa kwa malengo ya kisiasa.

Na kwa namna inavyokuzwa hii mada ni rahisi kuamini kuwa ni masuala ambayo watendaji wanawafahamu hao wahanga.

TRA wakiwa kazini kwa mtu mwenye msimamo wa haki hawezi kuwaweka kwenye kundi la watekaji.
 
Suala la Nondo ni sinema iliyotengenezwa na hao hao kina Zitto Kabwe ndani ya ACT.

Hao huo utekaji unaozungumzwa kwa kiasi kikubwa ni masuala ambayo serikali kuu haihusiani nayo moja kwa moja.

Ni siasa za kuelekea 2025 mwaka wa uchaguzi mkuu. Siasa haramu za kupakana matope na kuchafuana.
 
Mkuu utekaji siyo dhana dhanifu, mambo yametokea kweli na kila mtu ameona na kukubali kuwa utekaji upo.
Hata kama aliyetekwa ni mhalifu, kuna taratibu za kisheria zilizowekwa wazi kikatiba namna ya kumuweka nguvuni mhalifu.

Kuvizia mtu na kumchomoa hadharani bila utaratibu unaoeleweka huo ni uhuni.
Na wananchi wakiona kuwa sheria na taratibu hazifuatwi , wananjua kwamba mlnzi wa kwanza wa maisha yako ni wewe mwenyewe, JITETEE.
Katika kujitetea ukiua sawa, ukiomba msaada kwa wapita njia sawa!

Ndio maana vilio vya utekaji vilipozidi, serikali ilibidi itake note na kuchukua hatua stahiki.
 
Wewe ni miongoni mwa ma vijana wa hovyo ambao hawana mchango wowote kwenye nchi hii.
 
Ni kweli ulichoandika lakini katikati ya unyama huo unaofanyika pia kuna sinema za kisiasa zenye malengo ya kuichafua serikali kuu. Pia nahisi waandaaji wa sinema hii ni serikali hiyo hiyo.

Zitto kukubali kuicheza sinema kwa kumtumia Nondo wakati yeye na Samia wanaiva vizuri, inaonyesha kuwa hilo igizo litakuwa na chimbuko huko serikalini kwa malengo wanayoyajua wao.

Hata huyo Nondo ni mtu wa usalama wa taifa. Ni sawa na baadhi ya vyama vya siasa vyenye ukaribu na CCM unaweza kudhani ni wapinzani kweli lakini ukiwa karibu na wanachokifanya unagundua kuwa ni wale wale makada ya rangi za kijani.
 
Yaani ACT Wazalendo wamteke mtu wao na wampige hadi kumvimbisha mgongo mabega na miguu, kisha wampeleke hospitali kumtibu...

Wanateka hadharani stendi kuu ya mabasi, wakiwa na pingu za polisi!

Halafu vyombo vya dola havina uwezo wa kukamata watu hawa!

Basi hatuna viongozi. serikali ya CCM imeshindwa kuongoza.
 
Drama hii ni kali!
 
Propaganda za kitoto sana, yaani ACT wajiteke alafu polisi na CCM viwaangalie tu? Si wangekifutia usajili siku hiyo hiyo. Kama tu wapinzani wanafungwa kwa kesi za kuokoteza ndio sembuse utekaji!!?
 
Tusizunguke sana, tunapenda tu kukaza vichwa viongozi hata hawajali kuhusu watu kutekwa au kuuwawa. Kitu pekee wanachochukia ni vile hizi story ziipata coverage kubwa na hasa hasa zikivuka mipaka, vyombo vya nje vikianza kuzungumzia.

Ila hawaumii, we jua hilio uishi kwa amani.

Wao wanachotaka ni tuzizoee, tuone kama kawaida tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…