Inspekta Aveline Temba: Mnaonyimwa unyumba na wake zenu toeni taarifa

Inspekta Aveline Temba: Mnaonyimwa unyumba na wake zenu toeni taarifa

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274

Katika kuhakikisha ulinzi na elimu vinatolewa kwa wananchi, Jeshi la Polisi kupitia kikosi cha Wanamaji nchini kimeendelea kuyafikia makundi mbalimbali ya watumiaji wa vyombo vya majini ambapo leo kimetoa elimu ya ukatili wa kijinsia na mbinu za namna bora za kujiokoa pindi inapotokea ajali katika vyombo hivyo.

Akitoa elimu hiyo leo Agosti 6,2024, katika Boti ya Kilimanjaro, Mkuu wa Dawati la jinsia na Watoto kutoka kikosi cha wanamaji, Mkaguzi wa Polisi Inspekta Avelina Temba amewaomba wananchi hao kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi juu ya vitendo vya ukatili wa kijinsia vinavyofanywa na baadhi ya watu wasio na maadili katika jamii.

Soma Pia: Polisi yahimiza Wananchi wote kuwa waangalizi wa Watoto

Inspekta Avelina ameongeza kuwa wazazi wanapaswa kufuatilia kundi la watoto ambalo tafiti zake zimeonyesha kuwa kundi hilo liko katika hatari ya ukatili ambapo amewataka kuwasikiliza watoto ili kuzitambua changamoto wanazopitia.

Naye Mkaguzi wa Polisi, Inspekta Anna Ugomba amebainisha kuwa lipo kundi la akina baba ambao wanafanyiwa ukatili na wake zao ikiwemo kunyimwa unyumba ambapo amewataka kutoa taarifa hizo kwa Jeshi la Polisi ili wahusika wa vitendo hivyo wachukuliwe hatua za kisheria.
 
lipo kundi la akina baba ambao wanafanyiwa ukatili na wake zao ikiwemo kunyimwa unyumba ambapo amewataka kutoa taarifa hizo kwa Jeshi la Polisi ili wahusika wa vitendo hivyo wachukuliwe hatua za kisheria.

Duuh watajitetea wamechoka na kazi za nyumbani ,wapo red carpet ,kichwa kinauma ,tumbo linauma etc
 
Safi Sana kuna mwanaume mmoja kaoa Polisi
Huyo mke wake Polisi anamyima unyumba mumewe muda mrefu Tu ngoja nikamwambie huyo mwanaume awahi polisi

Mwingine ni mbunge mwanamke anamnyima unyumba mumewe nitamwambia

Mwingine ni jaji Mwanamke muda mrefu mumewe analalamika hajampa unyumba Miaka sasa ngoja nkamwambie awahi polisi
 
Afandee uko serious naomba namba huku kwetu vijana wanatembea wanaongea wenyewe ukikuta bar kanyimwa unyumba tuwasaidie
 
Afandee uko serious naomba namba huku kwetu vijana wanatembea wanaongea wenyewe ukikuta bar kanyimwa unyumba tuwasaidie
 
Back
Top Bottom