Intelijensia ya CHADEMA imefanikiwa kumuhadaa na kumuengua Tundu Lissu kwenye nafasi ya Umakamu Mwenyekiti na ile ya Mwenyekiti Taifa kisayansi sana

Intelijensia ya CHADEMA imefanikiwa kumuhadaa na kumuengua Tundu Lissu kwenye nafasi ya Umakamu Mwenyekiti na ile ya Mwenyekiti Taifa kisayansi sana

Tundu Lisu kuacha nafasi ya umakamu mwenyekiti kirahisi vile haikua bure, bali ilikua mipango mikakati ilopangwa kwa umakini mkubwa na makachero wa Chadema, ili kuhakikisha kwamba mwamba anashawishiwa kwa ustadi mkubwa, kwamba hivi sasa anazo sifa zote, vigezo na uwezo za kua mwenyekiti wa Chadema Taifa na sio makamu mwenyekiti tena, kumbe ni hadaa za kisayansi tu, dhidi ya wenye tamaa na uchu wa madaraka kama wa lisu. Maskini dah. Ama kweli wajinga ndiyo waliwao.

Lengo ni kumuondoa bila utata kwenye nafasi za uongozi Chadema, lakini pia kuondoa ugumu wa kumpata mgombea urasi wa Chadema 2025. Kumuondoa Lisu kwenye uongozi wa Chadema, kumerahisisha sana kumpata mgombea urasi asie Lisu bila chama kutikisika.

Miongoni mwa makachero hao, ni pamoja na hao wanaompigia simu, wanamuhadaa na kumtisha, nae bila kujua kua anarubuniwa. Anaogoma hata kuwataja, kwakua eti watu hao ni wa heshima sana nchi hii, ndio maana wanamtonya na kumshauri eti ajiongezee ulinzi, kwani kuna mipango ovu dhidi yake inapangwa, halafu ikitekelezwa atasingiziwa Mbowe.

Hizo ni hadaa anazofanyiwa na intelijensia ya Chadema bila yeye kujua. Itafika mahali atatishwa na kuikimbia nchi, kumbe ni kwasabb ya kushindwa uchaguzi.

Hata hivyo,
hivyo ndivyo intelijensia katika sayansi ya siasa hufanyika. Unamchochea muhusika aamini jambo lisilokuwepo, ili ajae kwenye 18 na mambo yake yaishe softly akishangaa na kung'aa macho tu.

Intelijensia ya kumshawishi Lisu ajiengue kugombea umakamu mwenyekiti Taifa, imetumika pia na kumuhadaa agombee uenyekiti wa Chadema Taifa, hali ya kua hana uwezo. Haya ni mafanikio makubwa sana kwa intelijensia team ya Chadema, na ni utapeli wa kisayansi sana amefanyiwa Lisu na kumtoa kabisa kwenye reli na medani ya siasa za kitaifa tuendako.

Sote ni mashahidi,
kwamba, kumrubuni mtu mwenye tamaa na uchu wa madarka ni kitu rahisi sana.

Ameruka majivu amekanyaga moto, na mkataa pema pabaya pana muita wahenga walisema hayo.🐒

Mungu Ibariki Tanzania
WEWE kweli ni BUMUNDA,KUBWA JINGA,POPOMA 🤣🤣😀🤣🤣
 
WEWE kweli ni BUMUNDA,KUBWA JINGA,POPOMA 🤣🤣😀🤣🤣
tuliza mawenge gentleman upate uhondo wa ukweli na uhakika kutoka duru za ndani kabisa kutoka korido za ufipa,

kumbafu sana aise dah 🐒
 
Ccm wamepaniki Sana kusikia lissu anagombea uwenyekiti wa chadema
kwakweli amekua na majuto mno,
na kwa kiasi kikubwa yupo lonely na very confused dhidi ya calmness ya chairman Mbowe whether atagombea ama laa..

kinachomuumiza zaidi ni kwamba tayari amejikosea umakamu wenyekiti na iwapo chairman Mbowe atachukua form, ni wazi atamlambisha sakafu vibaya sana..

na hiyo ni kumaanisha Tundu Lisu atabaki mikono mitupu tu kama wewe ulivyo dah!

Tamaa kitu mbaya sana 🐒
 
Mwanzoni maccm yalishangilia,sahivi yamegundua ohoooo ajae ni tabu zaidi yanabadili uelekeo Tena😃😃😃😃😃😃
 
Hapa unapiga tu ramli, unachosema huwezi kukithibitisha.
MOJA YA SIFA KUU YA LISSU SIYO MUOGA. .. ALIKUFA AKARUDI DUNIANI! ANATEMBEA NA RISAS, HAJAWAHI KUWA KIBARAKA WA CCM LAKINI MPAKA LEO ANAZUNGUMZWA KAMA LOWASSA
 
Back
Top Bottom