Intelijensia ya Rwanda sio ya mchezo mchezo, kinara wa Hotel Rwanda anashangaa kujikuta Kigali Airport

Intelijensia ya Rwanda sio ya mchezo mchezo, kinara wa Hotel Rwanda anashangaa kujikuta Kigali Airport

Serikali ya Rwanda inadai kuna ushahidi wa kutosha kumfungulia mashtaka ya kuhusika na genocide
Kwani mkuu hakunaga ushahidi na mashahidi wa kupikwa?

Miaka yote hadi anapewa 'tuzo ya ukombozi', hatujawahi sikia tuhuma ya mauaji dhidi yake.

Yamezushwa tu alipoonesha nia ya kugombea madaraka na kumpinga PK!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ninadhani kuna kitu haukielewi sawasawa kuhusu siasa za ndani ya Rwanda.

Mtu yeyote anayempinga ama kumkosoa rais Paulo Kagame hubatizwa jina la 'adui wa taifa' awe ndani ama nje ya nchi.

Unapompinga Kagame hata kwa mfano wa upinzani wa kisiasa unaofanywa nchini kwetu, elewa unarisk maisha na mustakabali wako wa uraia kwa ujumla.

Uchaguzi uliopita Rwanda, kuna mama mmoja chama cha upinzani, ile kuonesha nia ya kugombea urais tu, kazushiwa kesi nzito nzito zisizoisha, mpaka leo sijui aliyamalizaje!

Kwa hiyo huyo mtu, usiamini moja kwa moja kwamba ni 'haini' ama muuaji wa kimbari, hizo bado ni tuhuma tu.

Tusubiri tuone kwanza udadavuzi wa kisheria utakavyokuwa mahakamani, maana kashitakiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nakumbuka Binti mmoja mfanyabiashara wa Kitutsi kijana sana (jina limenitoka) alitangaza nia ya kugombea Urais lakini ndoto yake haikutimia kwani alikamatwa yeye na mama yake kwa makosa ya ukwepaji kodi kwenye kiwanda chao walichoachiwa na marehemu baba yao

Pia kuna Mwanamama wa Kihutu anaitwa Victoire Ingambire naye alirudi Rwanda kutokea nje ya nchi hiyo kwa ajili ya kugombea Urais pia akashtakiwa kwa makosa ya uhaini. Aliachiwa baada ya kukaa jela miaka kadhaa

Je ni kweli inawezekana watu wanakua na makosa yao mengi ya jinai ndipo wanataka kujiingiza kwenye siasa washinde kiti cha Urais wafiche madhambi yao au kuna uonevu tu? Lakini kama ni uonevu ni kwa kila mwenye kuonesha nia ya kugombea Urais?
 
Uko sahihi kabisa Mkuu na niombe radhi kwa kukosea hapo. Hata hivyo Paul Rusesabagina ndio alikua Manager mwenyewe(halisi) wa ile Hotel, inawezakana nimekosea kupata facts kwamba aliyeigiza kama yeye ni Mmarekani lakini msingi wake ni kumuonyesha Rusesabagina kua alikua shujaa aliyewakoa Watutsi waliokimbilia hotelini kwake.
Mkuu uzi wako unachanganya sana,sababu hata hiyo hotel haikuitwa hotel Rwanda.Nadhan tatizo umechanganya mambo ya kwenye movie na facts.
 
Mkuu uzi wako unachanganya sana,sababu hata hiyo hotel haikuitwa hotel Rwanda.Nadhan tatizo umechanganya mambo ya kwenye movie na facts.
Ndio Mkuu, movie iliitwa Hotel Rwanda lakini kiuhalisia ni Hotel Des Mille Collines. Mambo mengi nimesahau maana masiku nayo yamekua mengi. Ila uhalisia ni kwamba Rusesabagina ambaye wote tukidhani ni shujaa aliyewaokoa watu wasiuwawe na Intrehamwe sasa na yeye anatuhumiwa kwa ugaidi na yupo Rwanda baada ya kurudi katika njia ya kutatanisha
 
Kwani mkuu hakunaga ushahidi na mashahidi wa kupikwa?

Miaka yote hadi anapewa 'tuzo ya ukombozi', hatujawahi sikia tuhuma ya mauaji dhidi yake.

Yamezushwa tu alipoonesha nia ya kugombea madaraka na kumpinga PK!

Sent using Jamii Forums mobile app
Tena ndugu zake wametoa taarifa kwamba wamegundua Wakili anayemuakilisha yupo kwenye jopo la waendesha mashtaka wanao prosecute case yake!
 
Nakumbuka Binti mmoja mfanyabiashara wa Kitutsi kijana sana (jina limenitoka) alitangaza nia ya kugombea Urais lakini ndoto yake haikutimia kwani alikamatwa yeye na mama yake kwa makosa ya ukwepaji kodi kwenye kiwanda chao walichoachiwa na marehemu baba yao

Pia kuna Mwanamama wa Kihutu anaitwa Victoire Ingambire naye alirudi Rwanda kutokea nje ya nchi hiyo kwa ajili ya kugombea Urais pia akashtakiwa kwa makosa ya uhaini. Aliachiwa baada ya kukaa jela miaka kadhaa

Je ni kweli inawezekana watu wanakua na makosa yao mengi ya jinai ndipo wanataka kujiingiza kwenye siasa washinde kiti cha Urais wafiche madhambi yao au kuna uonevu tu? Lakini kama ni uonevu ni kwa kila mwenye kuonesha nia ya kugombea Urais?
Ndiyo hasa niliotaka kuwaelezea, lakini nikawa sina details za majina yao, shukrani mkuu kwa kuweka kumbukumbu sawa.

Huyo rais ndiyo zake kuzushia mabalaa watu wanaompinga ama kutofautiana naye kimawazo.

Kuna mwanajeshi mwingine pia, kama sikosei alikuwa ni 'director' wa intelligency walipishana kauli akakimbilia SA, mbona alifuatwa kuchinjiwa huko huko?

Hao tunaowafahamu ni wachache, lakini wengi wanaoata misukosuko wanapoinesha nia za upinzani.

Kwa hiyo raia anayetofautiana na watawala, kuzushiwa kesi ni kawaidana ni rahisi sana hasa nchi zetu za kiAfrika.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila tukitoka nje ya mada wazee, huyo muigizaji Don C ni nguli ki noma.

Filamu ya Hotel Rwanda ukianza kuiangalia, ni lazima utaing'ang'ania bila ya kupepesa macho kwingine hadi mwisho.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kabisa Mkuu, wenzetu wametuacha sana kwenye kila fani. Unajua hata ile 'This time in April' aliyocheza Idris Elba nayo ni kiwango na yenye kukuweka roho juu wakati wote
 
Paul Rusesabina aliyekua Manager wa Hotel Rwanda akiwaokoa Watutsi wasivamiwe na kuchinjwa na Interahamwe hatimaye amefikishwa mbele ya sheria kwa makosa ya kuhusika na njama za mauji hayo hayo.

Baada ya filamu ya Hotel Rwanda kueleza kisa cha Rusesabina, wakati wote dunia ilimuona kama shujaa aliyesaidia kuokoa maisha ya makumi ya Watutsi wasio na hatia waliokimbilia Hotel Rwanda hadi pale uchunguzi ulipofanyika na kugundua naye alikua mmoja wa walioshiriki kutekeleza genocide ile. Suala kama ana hatia au la mahakama itaamua lakini kilichoacha watu midomo wazi ni namna alivyofikishwa Rwanda, maana alikua akiishi Ubelgiji na alishachukua urai wa huko.

Inasemekana alikua Dubai na alidanganywa kupanda ndege ambayo labda aliamini inaenda sehemu nyingine. Kuja kutahamaki anajikuta anashuka Kigali Airport na pingu zikimsubiri!. Kabda ya hapo kuna jamaa wa Kinyarwanda aliandika makala akisema alijipa jukumu la kufuatilia nyendo za Rusesabagina duniani kote na alifanya hivyo kwa miaka 15 na kwa kukamatwa kwa Paul Rusesabagina basi ametimiza kazi yake akiwa kama Mzalendo wa nchi yake! Maofisa wa Rwanda wanasema jamaa amerudi mwenyewe kwa hiyari yake jambo ambalo ndugu wanalikanusha wakidai kua ametekwa, na sababu ni kwamba alianza harakati za kumuondoa madarakani Rais Kagame kwa kuongoza kundi la FNL ambalo Kigali inasema ni lakigaidi.

Serikali ya rais PK kama alivyo yeye mwenyewe ina mkono mrefu na wanamsemo wao kua "There is a price to pay in betraying Rwanda" na kwamba hicho ndio kilichomkuta Paul Rusesabagina.

Jamaa pia ameishi Marekani na Afrika Kusini na aka-settle Ubelgiji.

Tatizo hakusoma alama za nyakati na zile safari zake za kutoa lecture kwenye mavyuo mbalimbali duniani.

Hizo lectures zake zilionekana kama vile zapindisha ukweli halisi.

Sasa hawa mazee wa RIB walikuwa na kazi moja tu, ya kusoma uzuri zile dots za kuunganisha pale Dubai.
 
Je, shutuma anazo shutumiwa ni za kweli au ni vile anampinga kiongozi aliyepo madarakani?
Waafrika tuna shida sana kwenye kubadilishana uongozi.

Baadhi ya alokuwa akiwahifadhi ndo wamekuwa wakipinga yale anayoyahubiri kwenye mihadhara na kwenye kitabu alichoandika.

Kuna madai mengine mengi tu ambayo itabidi yawasilishwe mahakamani.
 
All empires are built on blood (Pablo Escobar). But ushauri wangu kwa Rwanda na wanyaruanda tu waanze kufikiria the after Kagame, hatutaki kuona mauaji mengine au kupokea wakimbizi tena. A smooth transition inastahili kuanza kufirikiwa before it is too late. Power vacuum huwa ni mbaya especially when there are many power mongers. Mungu ibariki Africa
 
Wazungu wakampa uraia, akapewa tuzo nyingi kama shujaa kumbe naye ailikuwa "mdhamini" wa mauaji na msaliti wa nchi yake! (Kuna mambo mengi ya kujifunza kutoka kwa huyu jamaa hasa pale unapoona kiongozi anapewa support kubwa na mataifa ya magharibi na Marekani) Ingekuwa Tanzania Paul Rusesabagina angekuwa kiongozi wa chama cha siasa au NGO ya kutetea Haki za raia, na hata urais angegombea tu, ila kwa Rwanda ukiisaliti nchi na kuwatumikia "mabeberu" lazima wakuwinde tu!
View attachment 1568411
Hii ishu ina siri kubwa, Siku zote ukimpinga PK lazima akutafute popote ulipo ndicho kilichotokea
 
Back
Top Bottom