International Schools zina nini cha zaidi?

INGAWA WANANGU WAKO HUKO ILA NAWAZA NILISOMA KAYUMBA MPAKA FORM SIX BAADAE NAKUTANA NA WATOTI WA VIBOSILE WA INTERNS
UDSM NKAAAZA MM NA KICHWA ZAIDI HAWA MADOGOJANJA WANGEJUA MWISHO TUNAKUTANA SEHEMU MOJA WASINGETESA WAZAZI WAO NA WENGINE WALIISHIA NJIAN VYUONI
 
NA HILI VUGUVUGU LA ADA ZA CHUO SEEKL KUAMUA KUTOA KWANZA KWA WALIOSOTA SHULE ZAO LA KUANGALIA SANA SANA

KAMA MTOTO YUKO POA PELEKA SERKALINI USIJETESEKA KAMA JANA WALE VIJANA WALIOTOLEWA UDSM KWENYE MITIHANI KISA ADA KAMAMZAZI KILINIUMA SANA

AWAKUPENDA WAZAZI WALIJIAMINISHA NA INTERN SCHOOL KUFIKA JUU MTAJI UMEKATA SERKL INASAIDIA WALE WA KAYUMBA KWANZA WANAJUA MATESO WALIYOPITIA WAKAFIKA HAPO...ACHEN TU
 

Nadhani umaskini hasa wa fikra unaleta makasiriko sana kwenye maisha , maana mleta mada hata kwa swali lake tayari ameshaonyesha bias . Anyways - hakuna formula kuwa aliyesoma NECTA Vs aliyesoma International schools ni lazima mmoja awe bora au asiwe bora. Kuna factora nyingi sana - na tumeona wengi wamesoma NECTA na wamefanya vyema , HOWEVER tunajua mazingira wezeshi na mtaala na walimu na walezi wana mchango mkubwa sana katika kutengeneza fikra za mwanafunzi akawa tayari kupambana na maisha , soko la ajira, misukosuko ya biashara nk. Kwanza tuelewe shule za kimataifa ni zipi? na shule zinazofundisha kwa Kiingereza ni zipi , na swali lake ni lipi? Nadhani anamaanisha

Shule ya kimataifa ni taasisi za elimu zinazotoa mtaala ulioundwa na kuidhinishwa kwa kiwango cha kimataifa, mara nyingi kwa lengo la kuwafundisha wanafunzi kutoka nchi mbalimbali na kuwaandaa kwa maisha ya kidunia. Shule hizi zinaweza kufuata programu za kielimu kama vile International Baccalaureate (IB), Cambridge International Examinations, au American Advanced Placement (AP), ambazo zinatambulika na kuheshimika kote duniani.

Shule za kimataifa zina manufaa mengi ambayo yanazidi yale ya vifaa vya kawaida vya darasani. Zinawaandaa wanafunzi kwa masoko ya kimataifa kwa kusisitiza kufikiri kwa kina, ujuzi wa kutatua matatizo, na uelewa wa tamaduni tofauti- mwanafunzi hafungwi katika mtazamo wa jamii yake pekee , kusoma na kuishi na tamaduni nyingi kunampanua mawazo.

Mitaala ya kimataifa: Shule nyingi za kimataifa hufuata mitaala inayotambulika kimataifa kama vile International Baccalaureate (IB) au Cambridge International Examinations, ambayo ni ngumu na inaheshimika duniani kote. Basi patatokea wabishi ooh wanafundishwa kuwa vibaraka wa wazungu, labda ndio labda sio ila kwa waliosoma hesabu kuna somo la probability- kuwa aliyekuwa na mtaala wa kimataifa ana nafasi kubwa sana ya kupambana na vijana wengi soko la kimataifa, ana nafasi kubwa kupata scholarship nk .

Uwezo wa Lugha: Ingawa kujifunza lugha ni sehemu ya uzoefu, lengo kuu ni ujuzi wa mawasiliano wa lugha nyingi, ambao ni muhimu sana katika dunia iliyo na muingiliano mkubwa. Bado watatokea wabishi na kukataa (wanaruhusiwa), binafsi nilikuwa na ubishi huu huu , nimesoma NECTA ila naona tabu katika matumizi la lugha nikilinganisha na wengine waliweza kuwa na lugha nyingi- kumbuka hata wengi wetu Kiswahili fasaha kujieleza na kukitumia pia ni changamoto.

Kufikiri kwa Kina na Kutatua Matatizo: Mbinu ya kielimu katika shule za kimataifa mara nyingi husisitiza kujifunza kwa kuuliza maswali, hivyo kuwahamasisha wanafunzi kufikiri kwa kina na kutatua matatizo kwa ubunifu. Tunaona leo , wengi tumekuzwa kwa hofu kuuliza maswali hata kwa walezi, jamii tunaona ni dhambi tumeondolewa kujiamini inapekea kuonewa , kunyanyaswa na kupata misongo ya akili - root cause ni malezi, elimu , dini , mitazamo nk , keyword mojawapo hapa ELIMU

Uwezo wa Kitamaduni: Wanafunzi wanajifunza jinsi ya kuelewa na kuheshimu kanuni na desturi tofauti za kitamaduni, jambo ambalo ni muhimu kwa mafanikio katika jamii iliyo na mchanganyiko wa watu kutoka tamaduni mbalimbali. Watu wameelezea kuwa shule za kimataifa zina mashoga wengi , pengine sina takwimu ila fuatilia vyombo vya habari na chunguza idadi ya shule zetu za kayumba nini kinaendelea , sikiliza vyombo vya habari idadi ya ulawiti , unyanyasaji wa kingono kwa ngazi za familia, jamii, ndugu nk- fuatilia idadi ya mashoga na matumizi ya bangi shule za kata ni hali mbaya . Kubwa ni je elimu imewatengeneza kuchambua lipi bora na lipi si bora katika tamaduni mbalimbali?

Michezo na ujuzi wa maisha: Kuna mengi kama muziki, kuogelea , michezo ambayo bahati mbaya shule zetu hazina miundo mbinu yetu haijawa nazo- siku hizi elimu pekee haitoshi , michezo hujenga uwezo wa kufikiri, na shule hizi humfunza mtoto mengi. Huendi camp wanajifunza hata kujenga vifaa kwa vitendo . Bado utasema mbona hawajui kufua - si dunia inaenda kwenye automation pana mashine, pana vifaa vya kutendea kazi kwa hiyo tujikite mtoto afue au mtoto ajue skills zote

Fursa za Zaidi ya Masomo: Shughuli nyingi za ziada zinawaruhusu wanafunzi kuchunguza maslahi na vipaji vyao, hivyo kukuza elimu iliyo kamili. Msomi wetu nguli Professor Mhongo ametuletea takwimu za kazi na masomo yanayohitakija duniani kwa sasa kama artifical intelligence, machine learning, data science, automation , blockchain technologies - swali ni je vijana wetu wako tayari kwa elimu yetu kupata fursa zaidi kwa hali hii?

Kuwa na mawazo wazi ni muhimu. Badala ya kuwa na hasi dhidi ya wale wanaohudhuria shule za kimataifa, tunapaswa kukubali uzoefu wao wa kipekee na akili kubwa wanazozikuza. Wanafunzi hawa mara nyingi wako tayari zaidi kukabiliana na changamoto za kimataifa na kuchangia kwa maana katika jamii. Bei ni kubwa ila tuwa celebrate wanaoweza - nilikuwa kama wewe mdau nikiona mtu anasomesha watoto wake shule bora naona anaringa, anawaharibu , anachezea pesa , ni kibaraka - ila nilipokutana na hawa watoto kazini nikaanza kubadili mtazamo na wengi hawana makasiriko kama sisi - wako open sana kutusaidia wakati sisi tumejikita kuhukumu, kusikitika na kuhuzunika mafanikio ya wengine. Yani njoo na hoja na mihemuko lakini ukweli utabaki pale pale . Haitoi hoja kuwa wengi wa NECTA wanafanikiwa pia , ila ni kwa msuli sana. Una ruksa kuchukia ila tujenge tabia ya kufuatilia kwa undani na kunchunguza kabla ya kulaumu maana tunaonekana hata hatuelewi nini kinaendelea huko duniani.

Blessings !!
 
Hao ni wangapi wamektaa? , wenzenu wana backup mpaka mtoto analipa ada mil 30 mpaka 100 na kitu unataka kusema ni kajamba 8 kwao? shule hizo hazina uhalisia na mafanikio wote ni madon .

Scenario ni kwamba mzee anaweza kumpa hata bil ya biashara pale wanatafuta connection hakuna jipya , shule hizi kuna dogo amesoma huko Arusha nilimdadiss akasema wanasoma sana ishu pana na maisha ya uhalisia vile mtu anapenda pia wanafurahia maisha ya masomo wakiwa wanaendea hobbies zao , kujumuika na watu mbalimbali kwenda nje mara kwa mara ndio kupata uzoefu.

Mo dewji wakati anatekwa rafiki zake alisoma nao huko nje walikuwa wanamfanyia mpango hata wa interpol ili kumsaidia kuokolewa hapa ishu kubwa ni kujuana na watu zaidi duniania ndio maana ya international , unaweza kupata suppliers au wenye viwanda humo school kama mate wako mambo yakawa safi .

Wengi wakitoka wanaenda kufanya kazi nje baadhi ndio wanakuja kuendeleza biashara nchini mwaa yule wa NALA alikuwa na mtaji wa kutosha kama unamfahamu mzee wake yule mchungaji wa ATN.

Kumbuka : Hakuna mtu wa hali ya chini anasome hapo.
 
Kwanza muhimu kutofautisha kati ya International schools na hizi English Medium zetu.

Tofauti kubwa ni mtaala(syllabus), proper international schools zinafundisha mitaala ya kimataifa mara nyingi (IB). Na zina bei kubwa kwa sababu hata walimu wa hiyo mitaala wengi sio Watanzania na gharama zao zinakubwa kubwa zaidi. Utofauti mkubwa ni namna wanavyofundisha....kuna utofauti mkubwa sana, huku NECTA tunaandaliwa kufanya mitihani; IB wanafunzwa sana namna ya kufikiri na kufanya maamuzi (google lines of inquiry theory), kuongoza, physchology etc. Unaweza kuhisi hiyo elimu haina maana, lakini ndio wanawajiri vijana wetu.
 
Yule binti kasoma international school leo anakata viuno kweny mziki , kwa nn asienda huko nje?

Diamond anapiga show za nje kwa sana hajasoma hata advance ya shule za kata.
Kipupweee kinachangiaqq mkuu tukitaka kuchunguza kilammafanikio ya mtu ama ndugu utakimbia....kunanwachaga wakoo dar na maagorofaa na maalorii mabasi fikaa kwaoo moshi kuna ndondocha kakaa sebulen huyoo akichekaa tu yaan kama unaenda moshi ukifika mbezi unalionaaa basilake tu mengine uchafuu
 
Kuna international school na kuna English medium hizo international school achana nazo hizo zina watu na hadhi zao.

Halafu hizi English medium nadhani ndio unaziongelea wewe of which una point nzuri.
English medium ni utapeli mkubwa sana
 
Ukiona watu wanalipia huduma wakati huduma hiyo hiyo wanaweza kuipata bure basi ujue kuna utofauti mkubwa.
 
Pointless kabisa.
Wengi wenu hamtaki kukubali international schools elimu yao ipo juu. Ni ukweli mchungu kwamba English Medium na hizi shule za msingi hamna lolote.
 
Hiyo international school ina kitu gani cha tofauti sana?
Wewe huna akili kichwani, International school hawatumii mtaala wa Tanzania wala hawafanyi mitihani ya Nacte.

Hivi mwanafunzi wa International school of Tanganyika unadhani unaweza kumshindanisha na mwanafunzi wa mitaala ya Tanzania?

Au mwanafunzi wa English medium kama Feza na Marian utamfananisha na wa Jangwani au Azania?

Bichwa komwe akili kisoda.
 
This is really myopic. Extremely myopic!

Kumbe lengo la kusoma INTERNATIONAL SCHOOL ni kwenda uRaya kufanya interviews na wazungu?

Na kwanini wasome mtaala wa wazungu? ili iweje? wakawe vijakazi wa uRaya?
Elimu yako tafadhali ?

Naona una msururu wa maswali ya kipumbavu hata baada ya kuelekezwa kwa lugha nyepesi.
 
Ukichunguza kwa makini wanaonyimwa viza ubalozi wa Marekani wengi lugha ndio tatizo ingawa zipo interview kwa kiswahili kwa some cases.

Mtoto aliyesoma international school hawezi kukosa viza kwa kushindwa kujieleza kwa kingereza kwa consular.
 
Ukichunguza kwa makini wanaonyimwa viza ubalozi wa Marekani wengi lugha ndio tatizo ingawa zipo interview kwa kiswahili kwa some cases.

Mtoto aliyesoma international school hawezi kukosa viza kwa kushindwa kujieleza kwa kingereza kwa consular.
Na ndilo tunawaambia hapa, unakuta mtu grammar anaelewa n.k tatizo kujiamini kujieleza, hivi ni vitu vinakukosesha fursa kama visa au kazi.

Yaani una majibu mziki ni kujieleza, kayumba confidence hawana wamezoea kupigwa mijeledi kama punda kitu kinamuathiri maisha yame yote.
 
πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
Ukichunguza kwa makini wanaonyimwa viza ubalozi wa Marekani wengi lugha ndio tatizo ingawa zipo interview kwa kiswahili kwa some cases.

Mtoto aliyesoma international school hawezi kukosa viza kwa kushindwa kujieleza kwa kingereza kwa consular.
Sio tu kukosa visa na kupenda kuishi in "victim mentality" kila kitu kuhisi uanonewa unanyanyaswa unasemwa - yani binafsi nasema umaskini hasa umaskini wa fikra ni mbaya sana kuliko uchawi.
 
St.Jude hiyo,bonge la shule kuzidi hata baadhi ya vyuo vikukuu hapa Bongoland.
 
dunia ya sasa inahitaji mtu anaejua vitendo na kujieleza mbele za watu......
Hujanielewa public speaking ni suala la kisaikolojia,tafuta six fears that face human beings. Na ilo la kuongea limo nadhani ni namba mbili Kama sio tatu.
Kujua na kutenda vitu viwili tofauti uelewe
 
Cheki matajiri wa dunia Kama wamesomea Harvard university,
Kuna ishu watu wanachanganya kati ya intuitive mind or sacred and logic brain
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…