International Schools zina nini cha zaidi?

International Schools zina nini cha zaidi?

ANAANDIKA BICHWA KOMWE:-

Hizi shule zinazoitwa "international schools" zinafundisha nini cha ziada sana ambacho hakimo penginepo?

Ni kweli, shule zina mazingira mazuri na yanayofurahisha, lakini je, kile wanachofundishwa wale watoto kina hadhi gani ya kulipiwa mamilioni?

Hapa ieleweke vema kwamba siungi mkono mashule ya kata ambayo kimsingi ni mashule butu yasiyo na sifa wala vigezo vya kuwa shule. Mashule ya kata ni maeneo maalumu ambayo watoto wanaenda kujazwa ujinga na kupoteza wakati.

Hizi international schools pia ni kama mashule ya kata yaliyochangamka tu isipokuwa pale unaenda kununua KIINGEREZA kwa milioni hamsini kwa mwaka.

Zaidi sana mtoto atapewa midoli ya kuchezea na mabembea ya kuning'inia. Of course bila kusahau CHETI CHA KIINGEREZA.

Linapokuja swala la maarifa ni kitu kingine kabisa. Hawa watoto ni makanjanja tu kama watoto wengine wanaosoma kwenye mashule ya kata.

Mpaka sasa sijaona ni kwanini mtoto akanunue Kiingereza kwa shilingi milioni hamsini wakati mtu anaweza kujifunza Kiingereza hata chini ya mti na akabukua vema tu kama makanjanja wengine akina Dayamondi waliojifunza Vingereza magetoni.

Tukiwawezesha hawa walimu wetu uchwara wa shule za Kata wataweza kufundisha kizungu vizuri tu.

Tuanze kudahili walimu ambao wana ufaulu mkubwa badala ya kudahili vilaza wenye MADIVISHENI FOO ati ndio wakawe walimu!

Hili lizingatiwe sana.
LUGHA, ujinga na upumbavu unaotumaliza wa-TZ nikutokujua lugha.
 
Una hoja lakini umeshindwa kuiwasilisha vizuri. lakini pia nimesoma andiko lako nimekuja kugundua kuwa
1. Umeshindwa kutofautisha International na English medium schools

2. Hauna ufahamu wa kutosha juu ya mfumo wa Elimu wa Tanzania na nchi zingine

3. Bado haujafahamu changamoto za elimu ya Tanzania na utatu,I wake. Bado fikra kuwa elimu ya Tanzania ina walimu waliofeli. Sio kweli. Masters ni nyingi huku tatizo ni mfumo unafanya mtu aonekane mwalimu hana analolifahamu kuliko mwanasiasa aliyefeli akapigiwa kura akawa hata diwani.
 
1.Walimu wa hizo International Schools wote lazima wawe na shahada,tena inayoendana na masomo utakayoenda kufundisha.
-Walimu wa Masomo ya Sayansi huwa ni wahandisi

2.Wana maabala ambazo sisi hata vyuoni hatuna.

3.Hawa hujikita kwenye mafunzo ya vitendo kuliko siye.

4.Wanatumia mitaala ya kimataifa ya oxford au Cambridge .

5.Wana maeneo ya kimichezo yenye hadhi.

Yani usije fananisha hao jamaa na siye wa kujifunza vita vya majimaji.
Yani unaringanisha Paso na Bugatti...🤯
Inakuwaje wabongo wanaotaka huku wanaenda kusoma huko oxford university na wametokea public/government schools.
Inabidi tuje na statistics ya watoto wote waliosomea international schools , English medium and st kayumba wako wapi kwa muda huu na wanafanya nini.
Sitaki kuponda kula Serena hotel eti ni sawa na kula kwa mama ntile pale kimboka buguruni.

Ila ueelewe kuwa binadamu sio logic/reason being Bali ni emotions creature anayejaribu kuwa reason logically.

Kuna human ego pia mkumbuke


Sidhani kuwa huko ndiko kunakufanya uwe na uwezo,Kama ni mziki you can learn anything on the internet ishu kubwa ni mtu kuwa na passion


We're emotions creatures we try to be logic or reasoning
 
ukiwa maskini automatikali akili yako inajidifensi kuona hizo shule hazina kitu ila ungekua na pesa nadhani ungeelewa zaidi maana akili i gekua inaona mazuri zaidi kuliko mabaya
Unachoongea ni sahihi Ila Kuna jamaa mmoja akasoma ist Halafu saivi ni it kwa kampuni uchwara Fulani ivi


Ila elewa suala la ego , boastfulness. Kuna vijana wanamaliza udsm wanasepa zao kupiga PhD and masters zao huko uk, Australia, German,USA etc hapo napo inakuwaje
 
U
Mkuu....shida ya mitaala yetu.
  • Nadharia nyingi kuliko vitendo
  • Bado inatupa elimu ya kikoloni ya kuwa vijakazi
  • Haijui hata lugha ipi ni bora kwa ajili kufundishia
  • Unafunzwa vitu vya miaka 40 hadi 50 hamsini nyuma
  • Hata hizo maabala ni za enzi hizo za akina Newton
  • Mwanafunzi anabeba begi kubwa kama anaenda Panda milima
  • Inajikita kwa mwanafunzi kumeza kuliko kuelewa
  • Mwalimu anafundisha masomo yote
Nenda vyuoni sasa
  • Kuna vyuo vya Uhandisi watu tuliosoma hadi masomo 15 kwa semister,,,
  • Watu wa arts walichaguliwa fani za Uhandisi na hadi sasa wapo mtaani
  • Watu wanakopi na kupaste research na wahadhiri hawana hata mda.
  • Maabala hazifanyi kazi
Njoo mtaani
  • Kuna watu wamehitimu lakini tuliosoma nao mpaka tunacheka kama mjaamaa anaenda mtibu mtu
  • Sasa tafuta watu waliogusa hata degree moja huko Ulaya au America uone walivyo moto...
  • Mfano mzuri mtaalam mwenyewe Chenge the Don,kila skendo ya wizi yupo ila hakuna wa kumgusa, uone elimu ya Havard inavyofanya kazi.
Unasifia mwizi wa Havard so Havard inafundisha wizi,kujua kitu sio unitumie kuiba why usifanye mazuri zaidi ukubalike na utangaze jina la chuo chako
 
Hiyo international school ina kitu gani
ANAANDIKA BICHWA KOMWE:-

Hizi shule zinazoitwa "international schools" zinafundisha nini cha ziada sana ambacho hakimo penginepo?

Ni kweli, shule zina mazingira mazuri na yanayofurahisha, lakini je, kile wanachofundishwa wale watoto kina hadhi gani ya kulipiwa mamilioni?

Hapa ieleweke vema kwamba siungi mkono mashule ya kata ambayo kimsingi ni mashule butu yasiyo na sifa wala vigezo vya kuwa shule. Mashule ya kata ni maeneo maalumu ambayo watoto wanaenda kujazwa ujinga na kupoteza wakati.

Hizi international schools pia ni kama mashule ya kata yaliyochangamka tu isipokuwa pale unaenda kununua KIINGEREZA kwa milioni hamsini kwa mwaka.

Zaidi sana mtoto atapewa midoli ya kuchezea na mabembea ya kuning'inia. Of course bila kusahau CHETI CHA KIINGEREZA.

Linapokuja swala la maarifa ni kitu kingine kabisa. Hawa watoto ni makanjanja tu kama watoto wengine wanaosoma kwenye mashule ya kata.

Mpaka sasa sijaona ni kwanini mtoto akanunue Kiingereza kwa shilingi milioni hamsini wakati mtu anaweza kujifunza Kiingereza hata chini ya mti na akabukua vema tu kama makanjanja wengine akina Dayamondi waliojifunza Vingereza magetoni.

Tukiwawezesha hawa walimu wetu uchwara wa shule za Kata wataweza kufundisha kizungu vizuri tu.

Tuanze kudahili walimu ambao wana ufaulu mkubwa badala ya kudahili vilaza wenye MADIVISHENI FOO ati ndio wakawe walimu!

Hili lizingatiwe sana.
 
International schools ni habari nyingine mkuu.

Achana na hizo za ada kubwa ya 50m annual kuna moja ipo morogoro primary ni 4.5m annual, secondary ni 17m annual kama sijakosea, ni mtaala wa cambridge.

Kwa hizo cambridge schools primary mtoto anaanza akiwa na miaka 5 mpaka miaka 11.

secondary anapiga 2 years kuanzia miaka 14 mpaka 16 hapa habari ya shule inakuwa imeisha

likizo anaenda zake marekani, england au canada kula upepo mwanana

chuo anapiga mbele huko kina havard, cambride,oxford
 
Umefanya utaft au unakurubuka kuuliza iv kwanza ww ebu tutajie mojawapo ya international schl labda ujui?
 
Wa
Haya mashule ya kata usiyabeze. Ni nafasi kubwa ya kila mwenye nia na uwezo wa kutoboa kupitia shule. Zamani kabla haya mashule hayajaja, Ndoto za wengi zilizimwa kutokana na kukosa nafasi za kuendelea na masomo baada ya Elowai. Japo walifaulu vizuri, lakini hawakwenda popote kutokana na nafasi kujaa mashuleni. Haya mashule ya kata yalikuja kufanya mapinduzi makubwa. Leo kuna madaktari, wahandisi, wahasibu, wanasheria wakubwa wametokea kwenye hayo hayo mashule. Usibeze ST. KAYUMBA zetu mzee, tunajua zilikotutoa hadi leo tupo hapa.




Nani huyo mwenye ufaulu mkubwa atakubali kudahiliwa ualimu ili aje alipwe laki3 kwa mwezi na manyanyaso kibao?

Yaani mwalimu ni mnyonge kwa kila mtu. wazazi, wanasiasa, mbaya zaidi hadi walimu wenzao wanawanyanyasa.

Imargine. Mratibu kata, Afisa elimu wanawanyanyasa walimu. Achilia mbali madiwani, watendaji wa vijiji/kata. Hapo hawajaja wakaguzi siju wa nini nini huko, hajaja mkurugenzi kuwatishia kumwaga unga, hajaja mkuu wa wilaya kuwacharaza bakora mbele ya wanafunzi. Nani huyo alofaulu vizuri atachagua kuwa mwalimu?!

Ipewe heshima taaluma ya ualimu. Ipewe maslahi mazuri kazi ya ualimu kisha wenye ufaulu mkubwa wataifuata wenyewe. Kitu ambacho pia hakiwezekani kutokana na idadi yao.

MWISHO, uwezo wa mtu kufanya vitu vikubwa hapa duniani, mfano, kuwa kiongozi mzuri, inovator, Fundi mzuri, mfanya biashara mzuri mwenye mafanikio..etc, ni uwezo wa kuzaliwa nao. Shule inakuongezea kitu kidogo sana.

Actually, shule ukishajua kusoma, kuhesabu, na kuandika what else do you need to fit in a sucessiful life?

Ubaya ni kwamba inafika pahala tunazama sana katika shule mpaka tunajikuta tunapoteza our natural abilities kwa kulishwa bookish concerpts ambazo kimsingi ni ideas za watu wengine. Tunakuwa wao, sisi tunajipoteza. School doent let you think oitside the box. Anyway. Ninamengi ya kuandika kuhusu shule lakini basi acha nirudi kwenye mada.....

Tunachagua kuwapeleka watoto kwenye shule za bei mbaya ili tu wawe na mazingira bora ya kusoma. Kufuata mkumbo wakati mwingi. Kutaka uonekane unahela wakati mwingine, kuwaridhisha watu flani wakati mwingine, kuhisi huko ndiko kunaelimu bora wakati mwingine. Yaani sababu ni mingi.
Kidogo wewe hujawa biased ,ishu Kama ni biashara wafanyabiashara wakubwa mno na investors wanakuambia kuwa pamoja na kusoma Havard school of business haikumuandaa kuja kuwa trader mzuri ama entrepreneur wa uhakika Bali amejifunza kwa internet. Mie nachopenda ni mwanangu awe na passion, perseverance, committed, dedicated, desire ya ku achieve ndoto zako .

Mwishowe ama kwanza kabisa awe na emotions intelligence kuliko IQ like mental resilience,composure, yaani aijue intuitive mind than logic reason brain which is faithful servant.
Yaani akiwa na upendo wa kukomaa ama kujifunza kitu mwenyewe akakipenda am sure hii inashinda degree zote duniani.


Warren Buffett ameanza kuwekeza katika stocks akiwa 11 , Elon musk,Bill gate wamesomea vyuo Gani. Lazima tukubali pia kuwa na ego ina influence some of our decision making
 
Back
Top Bottom