International Schools zina nini cha zaidi?

International Schools zina nini cha zaidi?

Elimu ni gharama ,asije kukudanganya mtu uwekezaji thabiti kwenye elimu ndio ukombozi wa nchi

Hujiulizi kama ada ya 50M mwalimu anayefundisha hao wanafunzi , nyenzo za kisasa za kujifunzia na viwango vya kimataifa vya mitihani wanaofanya hao wanafunzi.

Maslahi ya mwalimu kuanzia mshahara , malazi , usafiri , chakula na kadhalika mwalimu lazima atakua focused kwa kiasi kikubwa kuendana na viwango vya kimataifa vya hizi shule maana mwisho wa siku anafanyiwa tathmini kwa alichokifanya.

Serikalini huko CCM inawalipa walimu mishahara kiduchu na kuwakamua kwenye vyama visivyo na msaada kutetea maslahi yao ni miaka mingi sana walimu wamekuwa "laughing stock" kwa mishahara na hadhi wanayopewa ilhali hawa ndio watu waliomuandaa kila mmoja wetu hadi kufika hapa tulipo .

Pia mitaala ya hizo shule inaanza kumuandaa mwanafunzi kuwa mtu fulani moja kwa moja na mwisho inawajengea "exposure" kwa safari za mataifa tofauti tofauti ili kuwakutanisha na wenzao wa mataifa tofauti wangali wadogo.

Mtoto akitoka hapo lazima awe wa tofauti sana huwezi kulinganisha na elimu ya anayepata huyo wa elimu bure isiyo na kiwango.

Najua watu watasema mbona nchi zingine wanasoma bure , ndio ni bure ila bure yenye kiwango cha hali ya juu kodi ya mwananchi inatumika 100% kweli na inaonekana kuitoa elimu bure ndio maana hata mataifa hayo ya elimu bure wengi husoma shule za umma kuliko hata za private maana ni bure na ni bure yenye kiwango cha hali ya juu.
 
ANAANDIKA BICHWA KOMWE:-

Hizi shule zinazoitwa "international schools" zinafundisha nini cha ziada sana ambacho hakimo penginepo?

Ni kweli, shule zina mazingira mazuri na yanayofurahisha, lakini je, kile wanachofundishwa wale watoto kina hadhi gani ya kulipiwa mamilioni?

Hapa ieleweke vema kwamba siungi mkono mashule ya kata ambayo kimsingi ni mashule butu yasiyo na sifa wala vigezo vya kuwa shule. Mashule ya kata ni maeneo maalumu ambayo watoto wanaenda kujazwa ujinga na kupoteza wakati.

Hizi international schools pia ni kama mashule ya kata yaliyochangamka tu isipokuwa pale unaenda kununua KIINGEREZA kwa milioni hamsini kwa mwaka.

Zaidi sana mtoto atapewa midoli ya kuchezea na mabembea ya kuning'inia. Of course bila kusahau CHETI CHA KIINGEREZA.

Linapokuja swala la maarifa ni kitu kingine kabisa. Hawa watoto ni makanjanja tu kama watoto wengine wanaosoma kwenye mashule ya kata.

Mpaka sasa sijaona ni kwanini mtoto akanunue Kiingereza kwa shilingi milioni hamsini wakati mtu anaweza kujifunza Kiingereza hata chini ya mti na akabukua vema tu kama makanjanja wengine akina Dayamondi waliojifunza Vingereza magetoni.

Tukiwawezesha hawa walimu wetu uchwara wa shule za Kata wataweza kufundisha kizungu vizuri tu.

Tuanze kudahili walimu ambao wana ufaulu mkubwa badala ya kudahili vilaza wenye MADIVISHENI FOO ati ndio wakawe walimu!

Hili lizingatiwe sana.
Hivi unajua wafunzi wengi wanaotoka hizo shule za international wanaenda kusoma vyuo vikubwa duniani kama

Stanford University

Harvard University, USA

California Institute of Technology, USA

Oxford University, UK

Cambridge University, UK

University of Chicago, USA N.k

Hivyo vyuo watu wengi duniani na kila Taifa wanawish wapite hapo lakini ukifuatilia wanafunzi wengi hasa wa International school of Tanganyika kuwakuta kwenye hivyo vyuo ni jambo la kawaida kabisa.
Sasa utasemaje hizo shule sio bora?
Labda kama unazungumzia English Midiam hapo kidogo ntakuelewa ingiwa na zenyewe zinatofauti na Kayumba pia
 
Kuna international school na kuna English medium hizo international school achana nazo hizo zina watu na hadhi zao.

Halafu hizi English medium nadhani ndio unaziongelea wewe of which una point nzuri.
Bila shaka anazungumzia Internatinal school as international school. Sio EM. Ndio maana kwenye ada kataja 50M
 
Elimu ni gharama ,asije kukudanganya mtu uwekezaji thabiti kwenye elimu ndio ukombozi wa nchi

Hujiulizi kama ada ya 50M mwalimu anayefundisha hao wanafunzi , nyenzo za kisasa za kujifunzia na viwango vya kimataifa vya mitihani wanaofanya hao wanafunzi.

Maslahi ya mwalimu kuanzia mshahara , malazi , usafiri , chakula na kadhalika mwalimu lazima atakua focused kwa kiasi kikubwa kuendana na viwango vya kimataifa vya hizi shule maana mwisho wa siku anafanyiwa tathmini kwa alichokifanya.

Serikalini huko CCM inawalipa walimu mishahara kiduchu na kuwakamua kwenye vyama visivyo na msaada kutetea maslahi yao ni miaka mingi sana walimu wamekuwa "laughing stock" kwa mishahara na hadhi wanayopewa ilhali hawa ndio watu waliomuandaa kila mmoja wetu hadi kufika hapa tulipo .

Pia mitaala ya hizo shule inaanza kumuandaa mwanafunzi kuwa mtu fulani moja kwa moja na mwisho inawajengea "exposure" kwa safari za mataifa tofauti tofauti ili kuwakutanisha na wenzao wa mataifa tofauti wangali wadogo.

Mtoto akitoka hapo lazima awe wa tofauti sana huwezi kulinganisha na elimu ya anayepata huyo wa elimu bure isiyo na kiwango.

Najua watu watasema mbona nchi zingine wanasoma bure , ndio ni bure ila bure yenye kiwango cha hali ya juu kodi ya mwananchi inatumika 100% kweli na inaonekana kuitoa elimu bure ndio maana hata mataifa hayo ya elimu bure wengi husoma shule za umma kuliko hata za private maana ni bure na ni bure yenye kiwango cha hali ya juu.
Nimeipenda hii
 
Hapa ieleweke vema kwamba siungi mkono mashule ya kata ambayo kimsingi ni mashule butu yasiyo na sifa wala vigezo vya kuwa shule. Mashule ya kata ni maeneo maalumu ambayo watoto wanaenda kujazwa ujinga na kupoteza wakati.
Haya mashule ya kata usiyabeze. Ni nafasi kubwa ya kila mwenye nia na uwezo wa kutoboa kupitia shule. Zamani kabla haya mashule hayajaja, Ndoto za wengi zilizimwa kutokana na kukosa nafasi za kuendelea na masomo baada ya Elowai. Japo walifaulu vizuri, lakini hawakwenda popote kutokana na nafasi kujaa mashuleni. Haya mashule ya kata yalikuja kufanya mapinduzi makubwa. Leo kuna madaktari, wahandisi, wahasibu, wanasheria wakubwa wametokea kwenye hayo hayo mashule. Usibeze ST. KAYUMBA zetu mzee, tunajua zilikotutoa hadi leo tupo hapa.



Tuanze kudahili walimu ambao wana ufaulu mkubwa badala ya kudahili vilaza wenye MADIVISHENI FOO ati ndio wakawe walimu!
Nani huyo mwenye ufaulu mkubwa atakubali kudahiliwa ualimu ili aje alipwe laki3 kwa mwezi na manyanyaso kibao?

Yaani mwalimu ni mnyonge kwa kila mtu. wazazi, wanasiasa, mbaya zaidi hadi walimu wenzao wanawanyanyasa.

Imargine. Mratibu kata, Afisa elimu wanawanyanyasa walimu. Achilia mbali madiwani, watendaji wa vijiji/kata. Hapo hawajaja wakaguzi siju wa nini nini huko, hajaja mkurugenzi kuwatishia kumwaga unga, hajaja mkuu wa wilaya kuwacharaza bakora mbele ya wanafunzi. Nani huyo alofaulu vizuri atachagua kuwa mwalimu?!

Ipewe heshima taaluma ya ualimu. Ipewe maslahi mazuri kazi ya ualimu kisha wenye ufaulu mkubwa wataifuata wenyewe. Kitu ambacho pia hakiwezekani kutokana na idadi yao.

MWISHO, uwezo wa mtu kufanya vitu vikubwa hapa duniani, mfano, kuwa kiongozi mzuri, inovator, Fundi mzuri, mfanya biashara mzuri mwenye mafanikio..etc, ni uwezo wa kuzaliwa nao. Shule inakuongezea kitu kidogo sana.

Actually, shule ukishajua kusoma, kuhesabu, na kuandika what else do you need to fit in a sucessiful life?

Ubaya ni kwamba inafika pahala tunazama sana katika shule mpaka tunajikuta tunapoteza our natural abilities kwa kulishwa bookish concerpts ambazo kimsingi ni ideas za watu wengine. Tunakuwa wao, sisi tunajipoteza. School doent let you think oitside the box. Anyway. Ninamengi ya kuandika kuhusu shule lakini basi acha nirudi kwenye mada.....

Tunachagua kuwapeleka watoto kwenye shule za bei mbaya ili tu wawe na mazingira bora ya kusoma. Kufuata mkumbo wakati mwingi. Kutaka uonekane unahela wakati mwingine, kuwaridhisha watu flani wakati mwingine, kuhisi huko ndiko kunaelimu bora wakati mwingine. Yaani sababu ni mingi.
 
ANAANDIKA BICHWA KOMWE:-

Hizi shule zinazoitwa "international schools" zinafundisha nini cha ziada sana ambacho hakimo penginepo?

Ni kweli, shule zina mazingira mazuri na yanayofurahisha, lakini je, kile wanachofundishwa wale watoto kina hadhi gani ya kulipiwa mamilioni?

Hapa ieleweke vema kwamba siungi mkono mashule ya kata ambayo kimsingi ni mashule butu yasiyo na sifa wala vigezo vya kuwa shule. Mashule ya kata ni maeneo maalumu ambayo watoto wanaenda kujazwa ujinga na kupoteza wakati.

Hizi international schools pia ni kama mashule ya kata yaliyochangamka tu isipokuwa pale unaenda kununua KIINGEREZA kwa milioni hamsini kwa mwaka.

Zaidi sana mtoto atapewa midoli ya kuchezea na mabembea ya kuning'inia. Of course bila kusahau CHETI CHA KIINGEREZA.

Linapokuja swala la maarifa ni kitu kingine kabisa. Hawa watoto ni makanjanja tu kama watoto wengine wanaosoma kwenye mashule ya kata.

Mpaka sasa sijaona ni kwanini mtoto akanunue Kiingereza kwa shilingi milioni hamsini wakati mtu anaweza kujifunza Kiingereza hata chini ya mti na akabukua vema tu kama makanjanja wengine akina Dayamondi waliojifunza Vingereza magetoni.

Tukiwawezesha hawa walimu wetu uchwara wa shule za Kata wataweza kufundisha kizungu vizuri tu.

Tuanze kudahili walimu ambao wana ufaulu mkubwa badala ya kudahili vilaza wenye MADIVISHENI FOO ati ndio wakawe walimu!

Hili lizingatiwe sana.
Umeshawahi kujiuliza kwa nini Mwalimu wa English Medium anaweza asiwe na vigezo vya kukidhi kumfundisha International School?

Arusha, kuna shule moja inayomilikiwa na Mzungu mwenye asili ya Australia. Kipindi fulani, alitaka mitaala ya Cambridge kuanza kutumika shuleni kwake lakini alikwama kwa sababu hakuwa na waalimu wanaokidhi vigezo.
 
Hiyo international school ina kitu gani cha tofauti sana?
Kama jina lilivyo walimu wake ni international,mazingira ya shule ni bora kuanzia (madarasa,hostel,vyakula ni kama wako hotelini),wanafunzi wanahudumiwa kwa ukarimu/hospitable,facilities zote za kusomea zinapatikana kuanzia vitabu hadi computers,walimu wanalipwa vizuri kwa hiyo wanajituma sana kufanya kazi yao kiufasaha tofauti na kwenye shule za serikali walimu wanafundisha huku wakiwa na stress kwa hiyo wanalipua kazi yao bora liende,mtoto akielewa somo ni sawa na asipoelewa pia nu sawa potelea mbali hawana hasara.
Kwenye shule za international walimu wana muda mwingi wa kufuatilia maendeleo ya mwanafunzi mmojammoja na kumpa support personally one on one kumbuka kwenye darasa la International school lina wastani wa wanafunzi 40 wakati kwenye shule za serikali kidato kimoja kina wanafunzi 600 kitu ambacho inakuwa ni ngumu sana kuwakagua wote maendeleo yao jumlisha wanafundishwa na walimu wenye makasiriko ambao wakimuadhibu mtoto wanamuadhibu kama wanaua nyoka
 
Ipo siku mtakuja sema
Vyuo kama Havard na Oxford havina vya kuvizidi vyuo vya Bongo....nyie endeleeni tu.
 
Kwanza kuna mitaa na kata hazina hata mwanafunzi mmoja anayesoma au aliyesoma hizo shule....
Yani hata kukutana na hao Graduates wa hizi shule kama marafiki au wapenzi wetu ni ngumu,,,
wake tunaishia kuwaona wakiwa ma C.E.O kama Mob Dewji🤣🤣🤣
 
Ipo siku mtakuja sema
Vyuo kama Havard na Oxford havina vya kuvizidi vyuo vya Bongo....nyie endeleeni tu.
Inawezekana UDSM ikawa ndiyo Chuo Kikuu bora kabisa duniani! Kwani kuna kinachoshindikana Tanzania?

Nilipokuwa "mdogo", nilisikia:
1. JWTZ ndilo Jeshi bora duniani
2. Tanzania inashika nafasi ya pili duniani kwa ukachero.

Lakini baada ya kuwa mtu mzima, ingawa ninaviamini vyombo vyetu vya dola, hasa JWTZ, nimebaini mengine "nilidanganywa"
 
Inawezekana UDSM Ika wa ndiyo Chuo Kikuu Bora duniani! Nini kinashindikana Tanzania?

Nilipokuwa "mdogo", nilimsikia:
1. JWTZ ndilo Jeshi bora duniani
2. Tanzania inashika nafasi ya pili duniani kwa ukachero.

Lakini baada ya kuwa mtu mzima, ingawa ninaviamini vyombo vyetu vya dola, hasa JWTZ, nimebaini mengine "nilidanganywa"
Je,hapa tunaongea na GoldDhahabu Mdogo au mtu mzima...kwanza tujuze tusije ua Mende kwa nyundo.
 
Back
Top Bottom