Interview kwa watoto wanaoingia Nusery School ni haki kweli?

Interview kwa watoto wanaoingia Nusery School ni haki kweli?

Naanto Mushi

JF-Expert Member
Joined
Oct 16, 2015
Posts
6,236
Reaction score
15,677
Mimi nina mwanangu ana miaka 4 alikuwa hajaanza shule kwa kweli maana nilikuwa namuona kama ni mdogo sana bado.

Sasa, sasahivi ndo naona angalau kamekua kidogo, hivo nimeona ni busara aanze rasmi shule.

Ila juzi kati hapa kuna shule ya Nusery ipo karibu na ninapoishi, so nilienda kwa lengo la kumtafutia nafasi ili aanze shule.

Kinyume na fikra zangu kwamba mambo yatakuwa straight forward, ila nimeshangazwa sana baada ya kuambiwa hapa hawapokei mtoto asiyejua kusoma na kuandika, na kwamba eti kabla ya kuingia huwa wanatakiwa wafaulu interview.

Akaendelea kuniambia kwamba, hata kama ni mtoto wa miaka 3. Lazima ajue kusoma na kuandika ndo aingie hapo.

Kwa kweli hapa nimejikuta nipo kwenye hali ya kushangazwa sana na hichi kitu. Yaani naona kabisa hizi ni complication ambazo hazina msingi.

Halafu naona kabisa hawa watoto wadogo wa miaka mitatu wanaolazimishwa kujua kusoma na kuandika, hichi kitu kitakuja kuwaathiri sana miaka ya baadae. Sijui huu utamaduni wa kishenzi umetoka wapi, yaani mtoto wa miaka mitatu au minne, eti humtaki kisa hajui kusoma na kuandika.

Hivi no halali kweli hii issue? Au ni jamii yetu inazidi kupotoka
 
Siku hizi watoto wanateseka sana twa miezi saba nao wanaanza shule,ka miaka miwili kanaamshwa saa kumi na moja kujiandaa kwenda shule. Sasa huyo wa miaka minne wanamkataa wakati wao ndio wenye jukumu la kumfundisha kusoma na kuandika aiseee.

Bora serikali imepiga marufuku watoto boarding ilikuwa balaa hadi wa miezi wanapelekwa boarding
 
Siku hizi watoto wanateseka sana twa miezi saba nao wanaanza shule,ka miaka miwili kanaamshwa saa kumi na moja kujiandaa kwenda shule. Sasa huyo wa miaka minne wanamkataa wakati wao ndio wenye jukumu la kumfundisha kusoma na kuandika aiseee.

Bora serikali imepoga marufuku watoto boarding ilikua balaa hadi wa miezi wanapelekwa boarding
Hawa watoto watachoka ubongo.. ndo maana kuna nchi zimeweka sheria kabisa mtoto haruhusiwi kuanza shule kabla hajafikisha miaka 5... kuna nchi nyingine mpaka miaka 6.

Wataalamu wa ukuaji wa watoto waje hapa... kuna janga linakuja huko mbeleni... Kitoto cha miaka 2 unakiamsha saa 12... aiseee
 
Wana madarasa Yao wameyWeka hapo ya kupiga Hela mtoto anasoma miaka hata 3ndio aanze grade 1,na ni kinyume na mfumo wa elimu yetu
Mimi nilikuwa nataka kukubali aingie tu kwanza achanganyikane na wenzake, ila wananiambia haiwezekani maana hajui kusoma na kuandika.. hapo ndo nimeona hili suala ni zito... ni upuuzi
 
Hapo wanataka kupiga hela tu. hata kwa walioanzisha nursery school wazungu hawana mambo ya kipuuzi kama haya. Ni mikwara tu hakuna lolote hapo. Maana nursery ipo kumjenga mtoto wa miaka 3 kwenda mitano kujua numbers, michezo kusocialize na baadhi ya maandishi na namna ya kutamka. hakuna kustress. Hao ni waongo kabisa.
 
Mimi nina mwanangu ana miaka 4 alikuwa hajaanza shule kwa kweli maana nilikuwa namuona kama ni mdogo sana bado.

Sasa, sasahivi ndo naona angalau kamekua kidogo, hivo nimeona ni busara aanze rasmi shule.

Ila juzi kati hapa kuna shule ya Nusery ipo karibu na ninapoishi, so nilienda kwa lengo la kumtafutia nafasi ili aanze shule.

Kinyume na fikra zangu kwamba mambo yatakuwa straight forward, ila nimeshangazwa sana baada ya kuambiwa hapa hawapokei mtoto asiyejua kusoma na kuandika, na kwamba eti kabla ya kuingia huwa wanatakiwa wafaulu interview.

Akaendelea kuniambia kwamba, hata kama ni mtoto wa miaka 3. Lazima ajue kusoma na kuandika ndo aingie hapo.

Kwa kweli hapa nimejikuta nipo kwenye hali ya kushangazwa sana na hichi kitu. Yaani naona kabisa hizi ni complication ambazo hazina msingi.

Halafu naona kabisa hawa watoto wadogo wa miaka mitatu wanaolazimishwa kujua kusoma na kuandika, hichi kitu kitakuja kuwaathiri sana miaka ya baadae. Sijui huu utamaduni wa kishenzi umetoka wapi, yaani mtoto wa miaka mitatu au minne, eti humtaki kisa hajui kusoma na kuandika.

Hivi no halali kweli hii issue? Au ni jamii yetu inazidi kupotoka
Ni wapuuzi
 
🤣🤣🤣🤣🤣🤣 sijui hata namcheka nani....sijui teacher, sijui wewe
Kwanini mkuu... mimi wao ndo nawaona wana matatizo.. maana huwez kusema eti unaanza kumpima mtoto akiwa na miaka 4... kuna wengine wetu mpaka darasa la saba tulikuwa hatujielewi, ila baada ya hapo tumesonga kielimu kupita hata wale ambao walikuwa wanaonekana ni ma genius wakiwa wadogo
 
Hawa watoto watachoko ubongo.. ndo maana kuna nchi zimeweka sheria kabisa mtoto haruhusiwi kuanza shule kabla hajafikisha miaka 5... kuna nchi nyingine mpaka miaka 6.

Wataalamu wa ukuaji wa watoto waje hapa... kuna janga linakuja huko mbeleni... Kitoto cha miaka 2 unakiamsha saa 12... aiseee
kumuamsha saa kumi na mbili kwa hapa bongo ina make sense. ili mzazi aende kazini mtoto akae sehemu salama si ndio? na pia wadada wa kazi siku hizi sio wakuamini kabisaaa mara mia akae huko.

shida inakuja wanafanya nini hadi saa kumi za jioni?

maana kwa ninavyofahamu watoto at that age wanatakiwa walale sana, kucheza sana na kusoma kiasi sio kama watu wazima. hii nimesoma hapa google kutokana na hii mitaala ya nursery ya wenzetu huko. au wataalam wa mambo haya.
 
Back
Top Bottom